Tuesday, October 29, 2013

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI PROF. SOSPETER MUHONGO AZINDUA RASMI MRADI WA UMEME WA SUMBAWANGA - NAMANYERE

Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo katikati akishirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya kulia kwake, Mbunge wa Nkasi Kusini Ally Kessy kushoto kwake na wazee wawili kulia na kushoto wakiwawakilisha wananchi wa Namanyere (Wilaya ya Nkasi) katika uzinduzi rami wa mradi wa umeme kutoka Sumbawanga hadi Namanyere Wilayani Nkasi leo tarehe 28, Oktoba 2013. Mradi huo uliogharamiwa na Serikali ya Tanzania na kukamilika hivi karibuni una gharama ya Tsh. Bilioni 4.3 na umepitia jumla ya vijiji kumi na mbili vya njiani kabla ya kutua katika Mji huo wa Namanyere uliopo Wialayani Nkasi Mkoani Rukwa. Tangu Tanzania ipate Uhuru mwaka 1961 na tangu kuundwa kwa Mkoa wa Rukwa mwaka 1974 Wilaya hiyo haikuwa na umeme jambo ambalo limepokelewa kwa shangwe na wananchi wa Wilaya hiyo.  
Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo na washirika wake katika uzinduzi huo wakibofya kitufe maalum kama ishara ya kuwasha umeme katika Mji wa Namanyere leo tarehe 28, Oktoba 2013 baada ya Wilaya hiyo kukosa huduma hiyo katika kipindi chote cha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania. Katika uzinduzi huo Prof. Muhongo amesema Mkoa wa Rukwa umetengewa zaidi ya Tsh. bilioni 30 kwa ajili ya umeme vijijini kupitia REA, Wakala wa Umeme Vijijini ambapo jumla ya vijiji 66 katika kipindi cha miezi 20 ijayo kuanzia Novemba mwaka huu 2013 vitanufaika na mradi huo.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akimkaribisha Katibu Tawala Mkoa huo Alhaj Salum Mohammed Chima kuwasalimia wananchi wa Kirando katika ziara ya kikazi ya siku mbili ya Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo Mkoani Rukwa. Katika ziara yake hiyo anatembelea miradi mbalimbali ya umeme pamoja na kuzungumza na wananchi. 
Meneja Mahusiano wa Shirika la Umeme nchini TANESCO Bi. Badra Masoud akisherehesha baadhi ya mambo katika hafla fupi ya uzinduzi wa mradi huo uliofanyika Namanyere Wilayani Nkasi leo tarehe 28, Oktoba 2013.
Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akiongea na baadhi ya viongozi wa Serikali ya Mkoa wa Rukwa na Wilaya ya Nkasi leo tarehe 28, Oktoba 2013 juu ya upatikanaji wa umeme katika bandari mpya inayoendelea kujengwa ya Kipili Wilayani humo. Alisema kupitia REA, Wakala wa umeme vijijini kuanzia mwezi Desemba miradi mbalimbali itaanza kufanya kazi kuweza kufikisha umeme katika maeneo tofauti Mkoani Rukwa ikiwemo bandari hiyo ya Kipili.
Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akiwa ameshikilia kinyago cha mfano wa mtoto na mmoja ya wanakikundi cha ngoma za asili cha Kanondo cha Mkoani Rukwa baada ya kufurahishwa na uchezaji wa ngoma ya kikundi hicho inayoelezea malezi bora kwa watoto. 
Waziri Muhongo katika mikutano yake na wananchi hakusita kuwainua Mameneja wa Tanesco kuelezea juu ya miradi mbalimbali ya umeme Mkoani Rukwa. Kulia ni Meneja wa Tanesco Kanda ya Nyanda za Juu Magharibi Bi. Salome Nkondola na katikati ni Meneja wa Tanesco Mikoa ya Rukwa na Katavi.
Picha ya pamoja kati ya Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo na baadhi ya viongozi wa chama na Serikali wa Mkoa wa Rukwa.
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @Rukwareview.blogspot.com)

No comments: