Tuesday, October 8, 2013

CRDB BENKI YAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA DUNIANI

 Afisa wa Benki ya CRDB tawi la Azikiwe Premier jijini Dar es Salaam,Veronica Kivuyo akitoa huduma kwa mteja wa Benki hiyo,aliyefika katika tawi hilo.Huu ni utaratibu wa Benki ya CRDB unaokwenda sambamba na Madhimisho ya Wiki ya Mteja Duniani yanayoadhimishwa kila ifikapo wiki ya kwanza ya Mwezi Oktoba ya kila mwaka.
 Afisa wa Benki ya CRDB tawi la Azikiwe Premier - Kitengo cha Wateja Maalum - Augusta Mfuru (kushoto) akimhuduma Mteja wa Benki hiyo,ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Nkenge, Mhe. Assumpta Mshama.
 Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB tawi la Azikiwe Premier 
 Wateja wa Tawi hilo wakiwa wameketi kwa utaratibu unaotakiwa wakati wakisubiria kupatiwa huduma.
 Afisa wa Benki ya CRDB tawi la Azikiwe Premier - Kitengo cha Akaunti za Serikali - Ibrahim Mgorow (kushoto) akifafanua jambo mbele ya Meneja wa Tawi hilo, Fabiola Mussula (wa pili kushoto) pamoja na wafanyakazi wengine  wa Benki hiyo wakati wa muendelezo wa Kuadhimisha Wiki ya Mteja Duniani, inayoadhimishwa kila ifikapo wiki ya kwanza ya Mwezi Oktoba ya kila mwaka.
 Meneja Mikopo kwa Wafanyabiashara wa Benki ya CRDB tawi la Azikiwe Premier, Mary Kimasa (kushoto) akimsaidia mteja kutumia Mashine ya kutolea pesa  alipofika kwenye benki hiyo, ikiwa ni sehemu ya  wiki ya mteja duniani ambayo huadhimishwa kila wiki ya kwanza ya Mwezi Oktoba ya kila mwaka.
 Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Azikiwe Premiera, Fabiola Mussula (wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wafanyakazi wa tawi hilo.
 Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Azikiwe Premier, Fabiola Mussula (pili kulia) akisaidia kutoa huduma kwa mmoja wa wateja wa benki hiyo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Mteja Duniani 
 Meneja wa Utawala wa Benki ya CRDB tawi la Azikiwe Premier, Asha Mtambalike (kushoto) akiwonyesha Wenzaje kitu kwenye kompyuta.
 Afisa wa Benki ya CRDB tawi la Azikiwe Premier - Kitengo cha Akaunti za Serikali - Ibrahim Mgorow akihudumia wateja wake.
 Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Azikiwe Premiera, Fabiola Mussula (kulia) akisalimiana na mmoja wa Wateja Maalum wa Benki hiyo, Cosmas Takule.
 Picha ya pamoja na baadhi ya Wafanyakazi na Wateja.

 Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (wa pili kushoto) akimsikiliza mmoja wa wateja wa benki hiyo waliofika katika Tawi la Lumumba jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja inayoendelea nchi nzima.
 Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (kulia) akiangalia kwa makini taarifa za kibenki. 
 Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (wa pili kulia) akimsikiliza mmoja wa wateja wa benki hiyo waliofika katika Tawi la Lumumba jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja inayoendelea nchi nzima.
 Baadhi ya Wateja waliofika katika Benki ya CRDB, Tawi la Azikiwe wakipata huduma wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja inayoendelea nchi nzima.
Wateja wakipata huduma.
 Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwakaribisha wateja wao kwa nyuso za furaha, ikiwa ni siku ya kwanza ya Wiki ya Huduma kwa Wateja katika matawi yote ya benki ya CRDB.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (wa pili kushoto) akimsikiliza mmoja wa wateja wa benki hiyo waliofika katika Tawi la Lumumba jijini Dar es Salaam jana, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja inayoendelea nchi nzima. 
 Mkurugenzi wa Wateja Wadogo Wadogo wa Benki ya CRDB, Nellie Ndosa (kulia) akiwahudumia wateja wa beki hiyo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja inayoendelea nchi nzima.
 Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Saugata Bandyadhiyay akisalimiana na Bolozi Mwanaidi Maajar wakati alipofika katika tawi la PPF Tower jijini Dar es Salaam jana, ambapo viongozi wa benki hiyo walikuwa katika matawi ya benki hiyo kusikiliza kero za wateja wao katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja. Wa pili kulia ni Meneja wa tawi hilo, Can Maseyeck   
 Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Saugata Bandyadhiyay akisalimiana na baadhi ya wateja wa benki hiyo alipotembelea tawi la Premier jijini Dar es Salaam, ambapo viongozi wa benki hiyo hiyo walikuwa katika matawi ya benki hiyo kusikiliza kero za wateja pamoja na kupata maoni ya wateja juu ya huduma wanazotoa, wakati maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja.
 Baadhi ya Maofisa wa benki wa CRDB wakiwa wamepozi kwa picha.
 Maofisa wa Benki ya CRDB, tawi la Lumumba wakitoa msaada kwa mteja wa benki hiyo mwenye ulemavu wa miguu na mikono.
Ofisa wa Benki ya CRDB, Abella Wilson katika tawi la Lumumba jijini Dar es Salaam, akimsaidia kujaza fomu mteja wa benki hiyo, Selema Said Rajab ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja. 

No comments: