Friday, September 13, 2013

Madaktari Bingwa waokoa maisha ya wakulima wa Kilimanjaro.

·    Mpango wa Afya wa KNCU unapeleka vijijini madaktari bingwa wa magonjwa ya watoto, kinamama na sugu.
·    Madaktari bingwa waliotajwa hapo juu wamefanya kliniki 203 na kuona wagonjwa 1887 tangu Juni 2011 mpaka juni 2013.
·    Madaktari bingwa waliotajwa hapo juu huenda kwenye vituo 20 vilivyopo kwenye Mpango wa Afya wa KNCU walau mara mbili kwa mwezi.
·    Wagonjwa wenye matatizo sugu 66 waligundulika na kupewa rufaa ya kwenda KCMC.
·    Mpango wa Afya KNCU una wanachama zaidi ya 16,000 wanaopata huduma za Afya katika vituo 20  vya Afya vilivyopo kwenye mpango huo wa Afya.
·    Mafundisho ya nadharia na vitendo kuhusu jinsi ya kutambua ishara za hatarishi za magonjwa sugu yametolewa na madaktari bingwa hao kwa wahudumu wa afya wa vituo 20.
·    Wanakijiji wenye magonjwa sugu wamepata huduma kwa gharama nafuu bila kulazimika kuja mjini kwa matibabu, hivyo kuwapunguzia gharama na usumbufu
·    Watu wengi wamegunduliwa na matatizo (yaliyokuwa hatua za awali) ambayo yalishindwa kugundulika katika zahanati. Mf. Ugonjwa wa ini, cerebral palsy etc.
·    Kwa maelezo zaidi kuhusu Mpango wa afya KNCU piga namba ya bure (kwa watumiaji wa Vodacom Tanzania) 0800 754 002
Miaka miwili ya Mpango wa kupeleka madaktari bingwa vijijini unaoratibiwa na  Mpango wa Afya- KNCU (Juni 2011 mpaka Juni 2013)
                                                                                                      
Utangulizi
Mpango wa Afya KNCU ulianzishwa Aprili 2011, ukiwa na lengo kuu la kuhakikisha wakulima wa kahawa mkoani Kilimanjaro wanapata huduma ya Afya wakati wowote wanapoihitaji. Mpango huu unasimamiwa kwa karibu na PharmAccess, ambao kupitia serikali ya Uholanzi ndio wadhamini wakuu wa mradi. KNCU wanashirikiana kuhakikisha kuwa wanachama wao wanashiriki kwa wingi na wanapata huduma stahiki.

Mpaka sasa, jumla ya watu 16,000 ambao ni wakulima na wategemezi wao wamejiunga na mpango huu. Wanachama hawa wanapata huduma katika vituo 20 vya Afya vilivyoteuliwa na mpango wa afya – KNCU.


Mpango wa kupeleka madaktari bingwa vijijini

Mara baada ya mpango wa Afya KNCU kuanzishwa, PharmAccess kwa kushirikiana na hospitali ya rufaa KCMC walianza kutoa huduma ya madaktari bingwa kwenda kutoa huduma vijijini. Utaratibu huu ulianza Juni 2011. Sababu kuu zilizopelekea huduma hizi vijijini ni kama zifuatazo;

i.             Kuwajengea uwezo watoa huduma wa Afya walioko vijijini, kwa njia ya kufundisha kwa vitendo (clinical mentoring),kuendesha semina kila wanapowatembelea na kupitia mafaili ya wagonjwa ili kuelekeza matibabu sahihi ya wagonjwa.
ii.            Kutoa matibabu ya magonjwa sugu (mf. kisukari, shinikizo la damu, magonjwa ya mifupa kama gout n.k) kwa watu wanaoishi vijijini (wanachama na wasio wanachama wa mpango wa Afya KNCU)
iii.           Kuendesha kliniki kwa watoto wenye magonjwa ambayo yameshindwa kugundulika au kutibika na madaktari wa zahanati (mf. Cerebral palsy, kifafa n.k)

Wanakijiji wanalazimika kulipia angalau sh. 3,000 kuweza kumuona daktari kama sio mwanachama wa mfuko wa afya KNCU, na bila kulipia gharama yoyote ikiwa yeye ni mwanachama.

Baada ya kuendeshwa kwa mafanikio kwa kipindi cha miaka miwili, madaktari bingwa wa magonjwa ya wanawake na uzazi waliongezwa kwenye mpango, ambako huenda kutoa mafunzo, kuwapima na kuwashauri wajawazito na kutibu magonjwa ya kawaida ya wanawake.






Mafanikio yaliyopatikana

Kwa ujumla, wagonjwa 1,887 wamepewa matibabu na madaktari bingwa  katika mahudhurio 203 kwa kipindi cha miaka miwili, kama jedwali la chini linavyoonyesha



June to Dec 2011
Jan to Dec 2012
Jan to June 2013
Speciality
Visits
Patients seen
Visits
Patients seen
Visits
Patients seen
Paediatrics
26
72
39
308
18
208
Physician
34
123
60
777
23
375
Gynaecologists
0
0
0
0
3
24
Total
60
195
99
1085
44
607

Faida zilizopatikana

Licha ya faida nyingi za moja kwa moja na zisizoonekana moja kwa moja, taarifa hii itaorodhesha faida chache

i.             Wanakijiji wenye magonjwa sugu wamepata huduma kwa gharama nafuu bila kulazimika kuja mjini kwa matibabu, hivyo kuwapunguzia gharama na usumbufu
ii.            Watu wengi wamegunduliwa na matatizo (yaliyokuwa hatua za awali) ambayo yalishindwa kugundulika katika zahanati. Mf. Ugonjwa wa ini, cerebral palsy etc.
iii.           Baadhi ya wagonjwa waliokuwa na matatizo yaliyoshindikana, wamepata rufaa kuja KCMC kwa matibabu zaidi. Kwa mwaka 2012, jumla ya wagonjwa 66 walipewa rufaa.
iv.          Mafunzo ya matibabu kwa nadharia na vitendo yametolewa kwa madaktari wa zahanati vijijini.
v.            Kumekuwa na mtandao kati ya madaktari bingwa wa KCMC na madaktari wa vijijini, ambapo wamekuwa wakiwasiliana kwa simu pale daktari wa kijijini anapohitaji ushauri wa kutoa matibabu.

Changamoto

i.             Gharama za kuwapeleka madaktari bingwa ni kubwa.
ii.            Upungufu wa madaktari bingwa, hasa wakati huu ambapo vituo vya mradi vinaongezeka.
iii.           Ufahamu wa wanakijiji kuhusu ujio wa madaktari wa KCMC.
iv.          Mahudhurio ya wagonjwa wa kawaida, wasiohitaji matibabu ya daktari bingwa.


Dondoo kwa Wahariri na Bloggers:
  • Mpango wa Afya wa KNCU ni rafiki, hutoa huduma za afya ya msingi, pamoja na magonjwa sugu katika kituo kilicho karibu na pale mwanachama anapoishi.
  •  wamama wengi wamekuwa awakipoteza uhai wao na watoto wao wakati wa kujifungua kutokana na matatizo ya uzazi. Mpango wa Afya wa KNCU katika kulinda maisha ya mama na motto inatoa huduma ya salama ya kujifungua katika vituo vya msingi, na rufaa wilayani na hata KCMC pale inapobidi.
  • Mpaka sasa kinamama 21 wamepata huduma hii chini ya mpango wa afya wa KNCU, baadhi ya ni Mama Krismata kutoka chama cha msingi Marangu Marangu Magharibi, Mama Flaviana Mboya kutoka  chama cha msingi Marangu Mashariki, Grace Gilbert Lema kutoka chama cha msingi Machame Wari, Hellen William Lyimo kutoka chama cha msingi Kilema South, Etyefose Noel Massawe kutoka chama cha msingi Masama Mula, Haikael Jackson kutoka chama cha msingi Marangu Mashariki na Anna Paul Urassa kutoka chama cha msingi Mrimbo Uuwo.


 Uboreshaji huduma.
  • Mpango wa Afya wa KNCU kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) unaendelea na juhudi za kuboresha huduma katika vituo vinavyotoa huduma katika mpango huu chini ya mpango wa huduma salama (SafeCare).
  • Vituo hivi ni  zahanati za Mango, Mrimbo Uuwo, Mamba Mboni, Umbwe, Lole, Rauya, Mbahe, Mango , Makomu,  Sanya Juu, Mashati na Lemira vituo vya afya vya Masama Government, Masama Lutheran na Mwika Msae. Pia Hospitali za Marangu, Kilema, Kibosho na Ngoyoni.
  • Vituo  vilivyotajwa hapo juu  vimefanyiwa ukarabati kabla ya wanachama wa Mpango wa Afya wa KNCU kuanza kupata huduma. Mara nyingi ukarabati hugharimu si chini ya Tshs milioni 50 kwa kituo kwa wastani.
  • Zahanati ya Rauya, Mrimbo Uuwo, Lole na kituo cha Afya cha Mwika Msae vimefuzu na kupata daraja la hatua ya kwanza ya uboreshaji huduma chini ya mpango wa huduma salama (SafeCare).
  • Mafunzo mbalimbali yenye lengo la kuboresha huduma za kitabibu yanaendelea kutolewa na wataalamu wa PharmAccess na MicroEnsure.
  • Tathmini mbalimbali za utoaji huduma na mtazamo wa huduma hizo zinaendelewa kukusanywa na huingizwa moja kwa moja kwenye mpango wa kuboresha huduma.
  • Wataalamu kutoka KCMC wanatembelea vituo vilivyopo kwenye mpango wa Afya wa KNCU walau mara mbili kwa mwezi. Kwa mfano kwa mwaka 2012 madaktari wataalamu kutoka KCMC walitembelea vituo vilivyopo katika mpango wa Afya wa KNCU zaidi ya mara 99.


No comments: