Timu ya Kagera Sugar ndiyo iliyotangulia kupata bao kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, kupitia mchezaji Themi Felix Buhaja aliyefunga bao la kichwa baada ya kupigwa kona katika dakika ya 25 ya kipindi cha kwanza. Kipindi cha pili dakika ya 55 Khamis Mcha ‘Vialli’ aliisawazishia Azam FC bao na kufanya mpira kuisha kwa matokeo hayo hayo mpaka dakika 90 za mchezo.
Katika mechi nyingine Coastal Union ilitoka sare ya bila kufungana na Tanzania Prisons Uwanja wa Mkwakwani, Tanga wakati Ruvu Shooting iliifunga 1-0 Mgambo Shooting kwa bao pekee la Elias Maguri dakika ya 53 Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani
Katika mechi nyingine Coastal Union ilitoka sare ya bila kufungana na Tanzania Prisons Uwanja wa Mkwakwani, Tanga wakati Ruvu Shooting iliifunga 1-0 Mgambo Shooting kwa bao pekee la Elias Maguri dakika ya 53 Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani
Oljoro JKT ilitoka sare ya 1-1 na Rhino Rangers Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha, wenyeji wakilazimika kusawazisha dakika ya 27 kupitia kwa Amiri Hamad baada ya Saad Kipanga kutangulia kuwafungia wageni dakika ya tano, wakati Ashanti United ililala 1-0 mbele ya JKT Ruvu,
Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam bao pekee la Amos Mgisa dakika ya 81.
Matokeo hayo, yanamaanisha JKT Ruvu inaendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi zake tisa baada ya kushinda mechi zote tatu, ikifuatiwa na Simba SC katika nafasi ya pili yenye pointi saba.
Timu nyingi zimefungana kwa pointi tano katika nafasi ya tatu, zikiwemo Yanga, Azam na Coastal Union.
No comments:
Post a Comment