Thursday, August 29, 2013

taswira mbalimbali za Maadhimisho ya miaka 50 ya March in Washington

Leo, waMarekani wameadhimisha miaka 50 tangu kufanyika kwa maandamano makubwa ya kudai haki za watu weusi. Katika maadhimisho hayo, kamera ya swahilivilla blog iliegeshwa kando ya mlango wa kuingila na kushuhudia watu maarufu hapa nchini wakipekuliwa kwa sababu za usalama kabla ya kuingia ndani sherehe hizo ambazo ambazo zimehudhuriwa na maelfu ya watu kutoka sehemu mbali mbali nchini hapa.
Tuliobahatika kuwanasa katika kamera hiyo ni pamoja na muigizaji Jamie Foxx, pale alipotolewa ndani ya gari na maofisa kuanza kupekua gari alilolipanda kabla ya kuingia ndani ya eneo la Lincoln Memorial  Washington DC.
Muigizaji wa filamu Jamie  Foxx akishuhudia gari lake likipekuliwa kabla ya kuingia ndani ya tukio la maadhimisho ya miaka 50 ya March on Washington DC
Mwigizaji wa filamu Angelha Bassett Evelyn alipotolewa kwenye gari lake na maofisa kuanza kulipekua kabla ya kuingia ndani ya eneo la Lincoln Memorial  Washington DC
Mshangao mkubwa watu walioupata ni pale mtoto wa Rais wa zamani nchini Marekani John F. Kennedy, Caroline Kennedy ambae ni balozi mteule Nchini Japani, alipoingia na Cab (Taxi). cha kuchangaza pia ni pale gari lake lilipopekuliwa bila ya kujali ukubwa au cheo alichonacho na kufata sheria ya upekuzi kama wengine magari yao yalivyopekuliwa.
Muigizaji maarufu wa filamu nchini Marekani Forest Whitaker nae pia gari lake lilifanyiwa upekuzi na maofisa wa usalama baada ya kuwasili katika endeo la Sherehe za miaka 50 ya March on Washington DC
Forest Whitaker akikionyesha tabasamu baada ya kutolewa ndani ya gari lake na kufanyiwa utaratibu wa kupekuliwa kabla ya tukeo kuanza rasmi.
Vile vile kamera ya swahilivilla blog imemnasa Rajiv “Raj” Shah American Economic development specialist, alipotolewa nje ya gari lake na kufanyiwa upekuzi wa lazima siku ya Jumatano Aug 28, 2013 Washington DC
Watu tupo kazini..: Ofisa Usalama akifanya upekuzi wa magari ya watu maarufu yanayoelekea katika maadhimisho ya miaka 50 ya March on Washington DC siku ya jumatano Aug 28.
Mwanasheria Mkuu wa jimbo la California Kamala Harris pia alishushwa ili kuruhusu upekuzi wa gari kabla ya kuingia  katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya March on Washington
Kamala Harris aliamua kusogea na kusalimiana na baadhi ya watu waliokua karibu yake pamoja na kamera ya swahilivilla wakati gari yake ikipekuliwa kabla ya kuingia katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya March on Washington
Ni Oprah Gail Winfrey pekee ambaye hajatoka kwenye gari lake ambalo lilipekuliwa na kuruhusiwa kuondoka bila ya kutolewa ndani ya gari hilo alilokua amalipanda
Oprah Gail Winfrey akishangaa  kwa mbali flash ya swahilivilla wakati anaelekeaa ndani ya Lincoln Memorial Washington Washington DC 
Chief wa swahilivilla Abou Shatry akiwa katika 50th anniversary March on Washington DC Siku ya Jumatano 28, 2013 Rais Barak Obama, leo ametoa changamoto kwa kizazi kilichopo kuwaenzi mashujaa walioandamana mwaka 1963 kudai haki sawa kwa watu wa rangi zote nchini Marekani. JAMII RADIO ina ripoti kamili.Picha zote na (swahilivilla.blogspot.com)

No comments: