Friday, July 5, 2013

WAZIRI MKUU PINDA AONGOZA MAZISHI YA DIWANI CHONANGA IRINGA, AJITOLEA KUSOMESHA FAMILIA YAKE HUKu AKISIFU USHIRIKI WA CHADEMA KATIKA MAZISHI

 Mmoja kati ya madiwani  wa Manispaa ya  Iringa akiwa ameshika picha ya marehemu diwani  Chonanga
 Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa (mwenye Suti) na katibu  wa Chadema Iringa mjini Suzana Mgonakulima wa kwanza  kushoto wakiwa na madiwani  wa CCM katika msiba  wa diwani Chonanga leo
 Msaidizi  wa askofu  wa kanisa la  kiinjili  la  kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya  Iringa Blaston Gavile  akiendesha  ibada ya mazishi  ya diwani Chonanga  leo makaburi ya Mtwivila mjini Iringa
 Hili ni gari ambalo  lilkuwa  likiufuata msafara  wa  waziri mkuu jambo ambalo  lingeweza  kusababisha ajali katika msafara  huo hapa ni eneo la Mtwivila mjini Iringa
 Msafara  wa  waziri mkuu Mizengo Pinda  ukielekea makaburi ya Mtwivila kuongoza mazishi ya aliyekuwa  diwani  wa kata ya Nduli Iddi Rashid Chonanga leo
 Mwili  wa marehemu Chonanga  ukishusha kaburini na madiwani  wa Manispaa ya Iringa 




 Mlezi  wa CCM mkoa  wa Iringa  waziri mkuu Mizengo Pinda (kushoto ) mkewe Tunu Pinda wakiweka  shada la maua katika kaburi la diwani  Iddi Chonanga  leo
 Waziri mkuu Pinda  akimsubiri  mke  wake Tunu Pinda aweke shada ya maua   kabla ya kutoa heshima yao ya mwisho leo

 Mkuu  wa mkoa  wa Iringa Dr Christine Ishengoma akiweka shada la maua katika  kaburi ya diwani Chonanga  leo
 Mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (Chadema) na mbunge wa viti maalum mkoa  wa Iringa Ritta Kabati (CCM) wakishirikiana  kuweka shada la maua katika kaburi la diwani Iddi Chonanga ,enzi  za uhai  wake  diwani Chonanga  na  familia  yake walikuwa wakikabiliwa na kesi ya kumtishia  kumuua mbunge Msigwa kwa maneno kesi ambayo bado hukumu yake  kutolewa
 Mbunge  wa  jimbo la Kilolo na MNEC Prof Peter Msolla na mbunge wa viti maalum mkoa  wa Iringa Lediana Mafulu  wakiweka  shada la maua katika kaburi la Chonanga  leo

 Mstahiki meya  wa Manispaa ya  Iringa Amani Mwamwindi akipokea shada  kutoka kwa afisa  habari Manispaa ya Iringa Sima Bingileki  ili kuweka katika kaburi la diwani Chonanga
 Meya  Mwamwindi akiweka  shada la maua katika kaburi la Chonanga 
 Naibu  meya  wa Manispaa ya   Iringa Bw Gervas Ndaki kushoto akiongoza madiwani kuweka mashada ya maua katika kaburi la diwani  Chonanga  leo
 Katibu  wa Chadema Iringa mjini na diwani wa viti maalum Suzana Mgonakulima kushoto akiweka shada la maua katika kaburi la Diwani mwenzake  Chonanga 
Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa Terresia Mahongo akiweka shada la maua  leo kwenye kaburi la diwani  Iddi Chonanga 

Picha na habari na Francis Godwin Blog- Mzee  wa matukio  Daima


WAZIRI  mkuu  Mizengo  Pinda ambae ni mlezi  wa chama  cha mapinduzi (CCM) mkoa  wa Iringa  leo ameongoza wakazi  wa  mkoa  wa Iringa katika mazishi ya  aliyekuwa  diwani  wa kata ya  Nduli marehemu Iddi Rashid Chonanga huku akijitolewa  kusomesha  watoto  wake  wawili na yatima mmoja  aliyekuwa akisomeshwa na marehemu  Chonanga.


Waziri  Pinda alitoa ahadi leo  katika makaburi ya Mtwivila mjini Iringa  wakati  akitoa  salam  zake  za rambi rambi kwa  wakazi  wa kata ya Nduli  na wananchi  wa mkoa wa Iringa  kufuatia  kifo cha  diwani  huyo .


Alisema  kuwa  kifo cha  diwani  Chonanga   kimeacha  pendo ndani ya  familia na hata katika  chama  chake  cha CCM kutokana na  mchango mkubwa ambao  amepata kuutoa katika  kupigania  chama hicho na kuwa kutokana na maombi kusomeshwa  yaliyotolewa na watoto   hao ambao  waliyatoa  jana alipofika  kuhani msiba  huo katika kijiji cha Nduli 


Kuwa kwa upande  wake amejitolea kuisaidia familia  hiyo ya  Chonanga kwa  kusomesha  mtoto mmoja anayeendelea na masomo katika  chuo  cha IFM jijini Dar es Salaam  pia  kumsomesha  kijana  wake  mmoja ambae  yupo  sekondari pamoja na kuendelea  kumsomesha mtoto  mmoja yatima ambae  diwani  Chonanga  alikuwa akimsomesha katika shule ya  Sekondari ya Miyomboni mjini Iringa.


Mbali ya  kujitolea  kusomesha  watoto hao  bado  waziri Pinda  alilitaka  baraza la madiwani  la Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na mkurugenzi  wa Halmashauri  hiyo kuangalia uwezekano  wa  kumuenzi diwani  Chonanga kwa kazi kubwa za maendeleo alizozifanya katika kata  yake kwa  kuisaidia  familia  yake .


“ Mimi  nawashauri madiwani pamoja na mkurugenzi wa Manispaa kutokana na mchango mkubwa ambao  diwani Chonanga  aliutoa katika kuwatumikia  wananchi  wa kata ya Nduli ….sasa kuangalia  uwezekano  wa kuisaidia  familia yake…..sisi  kama  chama leo  tulikuwa na Halmashauri kuu ya  CCM tumechangishana  kiasi cha  zaidi ya Tsh 800,000 ambazo  tunazikabidhi kwa familia”


 Katika hatua  nyingine  waziri Pinda  amekipongeza chama  cha  Demokrasia na maendeleo  (Chadema)   wilaya ya Iringa mjini  chini ya mbunge wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa kwa  kuonyesha  ushirikiano mkubwa katika mazishi hayo .


“ Kweli kwa  moyo  mkunjufu kabisa napenda  kuwashukuru  sana  viongozi  wa Chadema  Iringa chini ya mbunge mchungaji Msigwa kwa  ushiriki mzuri wa mazishi  ya  diwani Chonanga ….nasema  ahsanteni sana mheshimu mbunge Msigwa na  wananchi  wote ambao  leo mmefika hapa”



Awali  akiendesha ibada ya mazishi  hayo msaidizi  wa askofu  wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi  ya  Iringa  Blaston Tuluwene Gavile  alitaka  viongozi  wa  serikali na  kisiasa  kukumbuka  kumcha Mungu  na kuiga mfano  wa Chonanga ambae  mbali ya  kufanya  shughuli za kisiasa  ila katika dini alikuwa mstari  wa mbele akiwa kama mshauri wa usharika wa Nduli .



Alisema   kuwa mara kwa mara  Chonanga  alikuwa akipigania  maendeleo ya  kata yake ya Nduli na  wananchi  wake na kuna  wakati alipata kumtamkia  wazi wazi kuwa yupo tayari  kufa na hata agopa  binadamu yeyote katika  kuwapigania  wananchi  wake.


“ Marehemu  alikuwa mtetezi  wa  kweli  wa maendeleo ya  wananchi  wake  ndani ya chama  chake  na hata katika kanisa  pia  ndio maana leo   umati mkubwa wa  watu  wamejitokeza kumzika ila sisi kama kanisa  tunasema kifo katika Kristo ni furaha kubwa na leo  hii  mama mzazi  wa Chonanga ambae ana miaka  zaidi ya 83 ameomba  kubatizwa  rasmi “



Akisoma histori ya marehemu Chonanga mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa  Terresia Mahongo  alisema  kuwa  Chonanga  alizaliwa mwezi  Februari ,1947 katika  kijiji  cha Malolo  wilaya ya  Kilosa  na  elimu yake ya msingi aliipata  katika  shule ya kati ( Middle School )  Kidodi wilaya ya  Kilolo na kujiunga na mafunzo ya ualimu katika chuo  cha ualimu Songea mkoani Ruvuma mwaka 1970



Katika  uhai  wake  marehemu aliajiriwa kama mwalimu  wa  shule ya msingi mwaka 1972 ambapo  miongoni mwa shule  alizopata  kufundisha ni pamoja na Mwembetogwa ,Kilimani , Nyabula, Nduli na Kitelewasi  zilizopo mkoani Iringa  pia marehemu aliwahi  kuwa  mratibu elimu kata ya kalenga  kuanzia mwaka  1994-1999 alipostaafu kwa mujibu  wa sheria na mwaka  2000 alifanya kazi ya ualimu kwa mkataba  wa mwaka  mmoja 


Katika  uongozi amepata  kuwa mwenyekiti wa CCM  kata ya Nduli  kati ya mwaka 2000-2005 na mwaka  2010 alichaguliwa  kuwa diwani wa kata ya Nduli katika Halmashauri  hiyo ya Manispaa ya Iringa na katika baraza la madiwani  wa Halmashauri  hiyo alikuwa ni mwenyekiti wa kamati ya maadili na mjumbe wa kamati ya  fedha na uongozi .


Mkurugenzi  huyo alisema  kuwa katika  kipindi  cha uongozi  wake alikuwa ni jasiri ,mfuatiliaji wa mambo,mshauri na mjenga hoja katika vikao  vya madiwai .



Marehemu Chonanga  alianza  kusumbuliwa  na maradhi  ya moyo usiku wa tarehe  2/7/2013 na alfajiri  ya tarehe 3/7/2013 alipelekwa Hospital  ya Rufaa ya mkoa  wa Iringa kupata matibabu  na mbali ya  jitihada  zilizofanywa na madaktari  ila zilishindikana na majira ya saa 7;45 mchana alifariki dunia .marehemu Chonanga  ameacha mjane  mmoja  watoto  10 na  wajukuu 9

Mungu ailaze  roho  ya marehemu Iddi Rashid Chonanga mahali pema peponi

AMINA

No comments: