Sunday, March 24, 2013

Taifa Stars yaibenjua Morocco 3-1 leo Uwanja wa Taifa

Kikosi cha Taifa Stars.
Kikosi cha Morocco.
Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars),Thomas Ulimwengu akiwatoka Golikipa na Beki wa Timu ya Taifa ya Morocco wakati wa Mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu kucheza Kombe ya Dunia Mwaka 2014 kule nchini Brazil,uliochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa wa Jijini Dar es Salaam.Taifa Stars imeshinda Bao 3 - 1,mabao mawili yaliyotiwa kimiani na Mshambuliaji Machachari,Mbwana Samatha huku moja likifungwa na Thomas Ulimwengu.
Beki wa Timu ya Morocco akiruka juu kuondosha hatari iliyokuwa ikielekeza langoni mwake.
Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars),Thomas Ulimwengu akiwatoka mabeki wa Timu ya Taifa ya Morocco wakati wa Mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu kucheza Kombe ya Dunia Mwaka 2014 kule nchini Brazil,uliochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa wa Jijini Dar es Salaam.
Hatari langoni mwa timu ya Morocco.............
Kiungo Mshambuliaji wa Timu ya Taifa (Taifa Stars),Shomari Kapombe akichuana vikali na Beki wa timu ya Morocco wakati wa Mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu kucheza Kombe ya Dunia Mwaka 2014 kule nchini Brazil,uliochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa wa Jijini Dar es Salaam.
Lango la timu ya Morocco ilikuwa ni hatari muda wote wa mchezo.
 Kipa wa Timu ya Morocco akiusindikiza kwa Macho mpira ulioingia wavuni,baada ta kuigwa na Mchezaji Mbwana Samatta wa Taifa Stars.
Mbwana Samatta akishangilia goli lake.
Mbwana Samatta akiondoka na mpira huku mabeki wa Morocco wakimfukuzia.
Mrisho Ngassa wa Taifa Stars (kushoto) akijiandaa kumtoka beki wa Morocco,Achchakir Abderrahim.
Kapombe akimpiga chenga safi Beki wa Morocco.
Mashabiki wa Taifa Stars wakiendelea kufurahia ushindi wa timu yao.
Wachezaji wa Taifa Stars wakimpongeza mwenzao Thomas Ulimwengu baada ya kufunga bao la kwanza.
Shangwe tupu uwanja wa Taifa.
Ulinzi wa nguvu uwanja wa Taifa.

No comments: