Tuesday, March 12, 2013

ALIYEKUWA AKITAPELI WATU MTANDAONI KWA JINA LA RAFIKIELIMU AJULIKANA, asakwa na polisi


Ni  Mhitimu  wa  Chuo  Kikuu  Cha  Sokoine  Morogoro  (SUA ), Mkaazi  wa  Njombe! Zawadi   Nono  Ya  Fedha  Taslimu, Shilingi  Laki  Tano  ( Tsh.500,000/=)  Za  Kitanzania, kutolewa  kwa  mtu atakaye  fanikishwa  kukamatwa  kwa  tapeli  hili  la  mtandaoni.

Hatimaye  yule  tapeli  sugu  wa  mtandaoni  aliyekuwa  akiwatapeli wananchi  mbalimbali  kwa  jina  la  RafikiElimu  akiwahadaa kuwapatia  ajira  ajulikana .

INAPOTOKA :   Mnamo  siku  ya  tarehe  11  Machi  2013, tuliripoti kupitia  blogu  yetu  na  katika  blogu  mbalimbali  nchini  kuhusu kuwepo  kwa  mtu  anaye  watapeli  wananchi  fedha  kwa  kutumia  jina  la  taasisi  yetu.  Tapeli  huyu  asiye  na  hata  chembe  ya  huruma  kwa  masikini  wenzake, aliweka  tangazo  katika  mtandao  wa  Zoom Tanzania, mnamo  mwanzoni  mwa  mwezi  February  2013  akitangaza nafasi  za  kazi z a  kuvolunteer  katika  mikoa  mbali mbali  ya Tanzania  bara.  Baada  ya  watu  kutuma  maombi  yao, tapeli  huyo
aliyekuwa  akijitambulisha  kwa  jina  bandia  la  EMMANUEL  ALBERT na  kwamba  yeye  ni  HR  wa  RafikiElimu,  aliwaambia  kuwa  wamepata  nafasi, na  kuwatumia   fomu  za  kujaza  kisha kuwataka  wamtumie
shilingi  elfu Tano ( Tshs. 5,000/=)  za  kitanzania  kwa  mpesa kwenda  namba   0763906931  (  AMBAYO  MBAYA  ZAIDI  AMEISAJILI  KWA JINA  LA  RAFIKIELIMU ).. Baada  ya  kumtumia  pesa , tapeli  huyo  aliwatumia  barua  na kuwaagiza  kuripoti  kazini  katika  taasisi  mbalimbali, huku  mmoja kati  yao  akimuagiza  aje  kuripoti  katika  ofisi  zetu.

Tulibaini  juu  ya  uwepo  wa  utapeli  huu  mara  baada  ya kutembelewa  na  mmoja  kati  ya  wahanga  wa  utapeli  huo.   Dada huyo  aliye jitambulisha  kwa  jina  la   HAWA  MUSSA  ambaye  ni Muhitimu  wa  Chuo  Kikuu  Cha  Dodoma  (  2012 )  aliripoti  katika ofisi  zetu  siku  ya  tarehe  11  Machi  2013  saa  nne  kamili
asubuhi  na  kuomba  kumuona  HR . Baada  ya  kufanya  naye mazungumzo  ndipo  tulipo  baini  kuwepo  kwa  utapeli  unao  fanyika kwa  jina  la  taasisi  yetu. Haraka  haraka  tukaenda  kuripoti uhalifu  huu  kwenye  kituo  kidogo  cha  polisi  cha  Chuo  Kikuu Cha  Dar  Es salaam, na  kukabidhiwa  RB namba   UD/RB/849/2013  WIZI
KWA  NJIA  YA  MTANDAO.

No comments: