Thursday, February 7, 2013

JK azindua utoaji wa Vitambulisho vya taifa katika viwanja vya Karimjee leo


 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akibonyesha kitufe kuashiaria kuzindua rasmi mfumo wa usajili na utambuzi wa watu na utoaji wa vitambulisho vya taifa uliofnyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.Watatu kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Bwana Mwaimu na kulia nia Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bwan Said Meck Sadik.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kitambukisho cha Taifa katika hafla ilkiyofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi akimkabidhi mke wa Rais Mama Salma Kikwete kitambulisho chake cha Taifa katika viwanja vya Karimjee leo huku Rais Kikwete akishuhudia.Kushot o Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Bwana Mwaimu
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rais Mstaafu awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kitambulisho chake cha taifa katika viwanja vya Karimjee leo.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rais Mstaafu wa Zanzibar Amani Abeid Karume kitambulisho chake cha taifa katika viwanja vya Karimjee leo.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa kitambulkisho cha taifa katika viwanja vya Karimjee leo.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad kitambilisho cha Taifa katika viwanja vya Karimjee leo wakati wa hafla ya Uzinduzi wa mfumo wa usajili na utambuzi wa watu.
 Rais Kikwete akimkabidhi Kada wa CCM Mzee Kingunge Ngombale Mwiru kitambulisho cha taifa.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Dkt. Alex Malasusa kiongozi wa kanisa la KKKT kitambulisho cha taifa.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Shekhe Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Alhaj Elihad kitambulkisho cha taifa.
 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  akimkabidhi Mwenyekiti wa CUF Professa Ibrahim Lipumba kitambukisho cha taifa.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Dkt.Ramadhani Dau kitambulisho cha taifa leo katika viwanja vya Karimjee.

Rais Dkt.Jakaya Kikwete akimkabidhi mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana William Erio kitambulisho cha taifa.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifurahi na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Bw.William Erio mara baada ya kupokea Kitambulisho cha Taifa
Baadhi ya wageni walioudhuria sherehe za uzinduzi wa Vitambulisho vya Taifa kutoka kushoto ni Kaimu Mhariri Mtendaji wa TSN Bw.Gabriel Nderumaki,Mkurugenzi Mkuu wa NSSF DKt.Ramadhani Dau,Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Bw.William Erio na Mkurugenzi Mkuu wa NHIF Bw.Emanuel Humba

Picha  na Freddy Maro  wa Ikulu

No comments: