Wednesday, October 17, 2012

TANZANIA YASISITIZA UMUHIMU WA WANAWAKE KUSHIRIKI KATIKA UTAFUTAJI WA AMANI

Balozi Dora Msechu akichangia majadiliano kuhusu ajenda ya uwezeshaji wa wanawake wakati wa mkutano wa Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la 67 la Umoja wa Mataifa, katika mchango wake, Balozi Dora Msechu alizungumzia juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali katika kukomboa mwanamke na mtoto wa kike dhidi ya vitendo vya kikatili, unyanyasaji na ukosefu wa huduma za kuridhisha za huduma ya afya ya mama mjamzito. Aidha katika mchango wake, Balozi Msechu amesisitiza haki na fursa ya wanawake kushiriki katika majadiliano ya kutafuta amani ili kuifanya dunia kuwa mahali salama.
Rais wa Baraza Kuu la 67 la Umoja wa Mataifa, Bw. Vuc Jeremic ambaye ameahidi kufanya kazi kwa Karibu na Kamati ya Tatu ya Baraza hilo inayohusika na masuala ya Maendeleo ya Jamii, Haki za Binadamu na Utamaduni katika kusukuma mbele ajenda zinazohusu maendeleo ya wanawake, fursa sawa za kijinsia na uwezeshaji. 
 
Na Mwandishi Maalum 

Wakati Rais wa Baraza Kuu la 67 la Umoja wa Mataifa, Bw Vuc Jeremic akisisitiza haki za wanawake kama nguzo muhimu katika kufikia usawa wa kijinsia. Tanzania kwa upande wake imesisitiza haja na umuhimu wa wanawake kushirikia katika majadiliano ya kutafua amani ili kuifanya dunia kuwa mahali salama. 

Akihutubia kwa mara ya kwanza Kamati ya Tatu ya Baraza hilo inayojihusisha na masuala ya, pamoja na mambo mengine maendeleo ya jamii, haki za binadamu na utamaduni. Bw. Jeramic ameahidi kufanya kazi kwa karibu na kamati hiyo katika kutetea maslahi yanayolenga kumuinua na kumuendeleza mwanamke katika nyaja zote. 

Kwa siku mbili mfululuzo wajumbe wakati hiyo wamekuwa wakijadiliana na kubadiliana mawazo kuhusu ajenda inayohusua maendeleo ya wanawake, huku wakipokea taarifa mbalimbali kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon na Wakuu wa Mashirika yaliyochini ya Umoja huo. 

Rais wa Baraza kuu la 67 la UM akatumia fursa hiyo pia kuwahimiza wajumbe wa Kamati hiyo kufanya kazi kwa karibu na Baraza la Uchumi na Fedha ( ECOSOC) katika masuala mtambuka ambayo yanahusu maendeleo ya wanawake. 

Akasema Kamati hiyo ni muhumi sana katika kushughulikia masuala ya haki za binadamu zikiwamo za wanawake na ndiyo maana aliamua kwenda kuzungumza na kamati hiyo kuihakikishia utayari wake wa kushirikiano nao katika mwaka huu wa urais wake. 

Baadhi ya mambo muhimu yaliyojadiliwa na wajumbe wa kamati hiyo ni pamoja na kuendelea kwa hali ya unyanyasaji na ubaguzi dhidi ya wanawake, kuendelea kwa vitendo vya ukatili dhidi yao kama vile ubakaji, kuendelea kwa tohara za wanawake na ukosekanaji wa fursa mbalimbali za kujiamulia mambo yao wenyewe zikiwamo fursa za uchumi, elimu, ajira na huduma bora na kuridhisha za uzazi salama na biashara haramu ya binadamu. 

Akichangia majadiliano hayo, msemaji wa Tanzania katika Mkutano huo Balozi Dora Msechu alisisitiza pamoja na mambo mengine kwamba, haki za mwanamke ni pamoja na haki ya kushiriki katika majadiliano na michakato ya kutafuta amani ili kuifanya dunia kuwa mahali salama zaidi. 

Balozi Msechu akasema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua kwamba fursa sawa kwa wanawake na watoto wa kike ni haki ya msingi. Na kwamba wanawake wakielimishwa na kuwezeshwa wanaouweza mkubwa wa kuendesha uchumi na kuimarisha jamii katika ujumla wake.

 Akasema kwa kutambua mchango wa wanawake katika utafutaji wa amani na kubwa zaidi katika kukuza uchumi na maendeleo ya jamii, serikali imetoa kipaumbele cha pekee katika ajenda ya usawa wa kijinsi na uwezeshaji wa wanawake. 

Akaeleza pia juhudi mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanyika katika kukomesha aina zote za unyanyasaji na maovu dhidi ya wanawake na kwamba juhudi zimekuwa zikifanyika za kurekebisha baadhi ya sheria zikawamo za ndoa na mirathi ili kuondoa vipengele vinavyomkandamiza mwanake. 

 Kwa upande wa changamoto, Balozi Dora Msechu amezitaja chanagamoto hizo ni pamoja na ukosefu wa huduma za uhakika za afya ya mama wajawazito na kwamba hali hiyo imesababisha kuendelea kupotea kwa maisha wa wanawake na watoto wachanganga chini ya miaka mitano.

No comments: