Tuesday, May 29, 2012

TANZANIA YAUNGANA NA NCHI NYINGINEZO DUNIANI KUADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA WALINDA AMANI WA UMOJA WA MATAIFA

Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) hapa nchini Bibi. Hopolang Phororo akizungumza machache wakati wa maadhimisho hayo ambapo pia alisoma ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-Moon kuwa leo tunatoa heshima kwa Walinda Amani zaidi ya 2900 ambao wamepoteza maisha wakiwa kazini katika miaka iliyopita na kuahidi kuendeleza kazi yo kurejesha Amani katika nchi zenye vita.Amesema katika siku hii ya Umoja wa Mataifa ya Walinda Amani tuitumie kukumbuka jinsi watu walivyojitolea maisha yao, na tuahidi kuimarisha ushirikiano wa kidunia ambao unawafanya hawa wavaa kofia za Bluu waonekane kama alama ya Amani duniani kote.
Mgeni rasmi Naibu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Mahadhi Juma Maalim akitoa hotuba wakati wa maadhimisho ya Siku ya Walinda Amani Duniani 2012 ambapo amesema Kauli mbiu ya Mwaka huu imelenga kuunganisha majeshi yote ya kulinda amani ya Umoja wa Mataifa katika kuhakikisha bara la Afrika linakuwa na Amani na Utulivu.
Mgeni rasmi Naibu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Mahadhi Juma Maalim akisalimiana na baadhi ya Maafisa wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa.
Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) hapa nchini Bibi. Hopolang Phororo akisalimiana na baadhi ya Maafisa wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa. 
Brass Bendi ikiingia katika Uwanja wa Mashujaa Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam wakati wa Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa inayoadhimishwa kila Mwaka tarehe 29 Mei.
Baadhi ya Mabalozi, Maafisa wa Ubalozi, Wakuu wa vitengo mbalimbali vya Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Wanadiplomasia, Maafisa wa Serikali na Maafisa kutoka jeshi la ulinzi la Wanachi wa Tanzania (JWTZ).
Baadhi ya Wanajeshi wa Kulinda Amani wa Umoja wa Mataifa katika maadhimisho hayo.
Baadhi ya Wanafunzi kutoka Shule ya Sekondari Benjamini Mkapa ya jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Mabalozi, Maafisa wa Ubalozi, Wakuu wa vitengo mbalimbali vya Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Wanadiplomasia, Maafisa wa Serikali na Maafisa kutoka jeshi la ulinzi la Wanachi wa Tanzania (JWTZ).
"Mungu Ibariki Afrika, Wabariki Viongozi Wote.......!!!
Mgeni rasmi Naibu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Mahadhi Juma Maalim akijongea na kuweka shada la maua katika mnara wa kumbukumbu ya mashujaa.
Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) hapa nchini Bibi. Hopolang Phororo akiweka Shada la Maua kama ishara ya kuwakumbuka walinda Amani wa Afrika.
General Officer Commanding (GOC) Meja Jenerali Hassan Vuai Chema akitoa heshima zake.
Usia Nkhoma-Ledama kutoka Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) ambao ndio waandaaji wa maadhimisho hayo hapa nchini.
Zainab Abdalah kutoka Mtandao wa Vilabu vya Umoja wa Mataifa Tanzania akighani Mashairi wakati wa Sherehe za maadhimisho hayo.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Azania wakitoa burudani za nyimbo za kuhamasisha Amani na Upendo.Picha zote na MO BLOG.

No comments: