Friday, April 27, 2012

DR. MARY NAGU AFUNGUA KONGAMANO LA MAKATIBU MUHTASI NCHINI,JIJINI MWANZA LEO

Mgeni Rasmi katika Kongamano la Makatibu Muhtasi nchini linalofanyika leo kwenue Ukumbi wa Hoteli ya Malaika Jijini Mwanza,Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu (katikati) akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Eng.Evarist Ndikilo pamoja na wadau wengine wa Kongamano hilo wakati akiwasili.
Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu Muhtasi Tanzania (TAPSEA),Pili Penda akitoa maelezo mafupi ya Kongamano hilo kwa Mgeni rasmi ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu wakati wa ufunguzi uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika Beach Resort,Jijini Mwanza.
Mkuu wa Mkoa Mwanza,Eng.Evarist Ndikilo akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Pili la Makatibu Muhtasi nchini Tanzania (2th National Secretarial Confrerence) linaloendelea hivi sasa kwenye ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika Beach Resort,Jijini Mwanza.
Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu Muhtasi Tanzania (TAPSEA),Pili Penda (kulia) akimpokea Mgeni Rasmi katika Kongamano la Makatibu Muhtasi nchini linalofanyika leo kwenue Ukumbi wa Hoteli ya Malaika Jijini Mwanza,Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Pili la Makatibu Muhtasi nchini Tanzania (2th National Secretarial Confrerence) linaloendelea hivi sasa kwenye ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika Beach Resort,Jijini Mwanza.
 Muwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma,Mama Wanderage akitoa salamu za Mkuu huyo wa Chuo kwa Makatibu Muhtasi waliopo kwenye Kongamano hilo.
Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu Muhtasi Tanzania (TAPSEA),Pili Penda akimpatia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu Tuzo ya heshima kwa uwepo wake kwenye Kongamano hilo leo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu akiionyesha tuzo ya heshima aliyokabidhiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu Muhtasi Tanzania (TAPSEA),Pili Penda
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Biz Logic,Carl Bosser  akitoa somo kwa Makatibu Muhtasi waliohudhulia Kongamano hilo leo jijini Mwanza.
Dk. Mary Nagu akisalimiana na Baadhi ya washiriki wa Mkutano huo.
Ephraim Kibonde ambaye ndie Mc wa Kongamano hili akifungua rasmi
 Mdau Albert G. Sengo (kushoto) akibadirishana kadi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu.

1 comment:

Anonymous said...

Hiki chama cha Masekretari huwa kinawasaidia watu gani??? Kutoka wapi!! ofisi za watu binafsi au wizara au mashirika ya umma???
Tulio wengi hatukijui!!!!!