Sunday, July 31, 2011

Uchaguzi Mkuu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Iringa




Uchaguzi ni uchaguzi nimeshindwa kwa kura moja ila naunga mkono matokeo ni Sima Bingileki na Daud Mwangosi ambaye ni mwenyekiti mpya wa IPC
Sulemani Boki amefanikiwa kutetea nafasi yake ya uweka hazina ndani ya IPC kwa kupata kura 16 kati ya 7 alizopata mpinzani wake Mawazo Marembeka(RFA) Iringa
Mwanachama wa TGNP mkoa wa Iringa na mwandishi wa gazeti la Mwananchi mkoa wa Iringa Tumain Msowoya akiomba kura kwa wanachama katika nafasi ya umakamu mwenyekiti japo hakuweza kupita baada ya kupata kura 6 kati ya 23 zilizopigwa
Mwandishi wa Radio Free mkoa wa Iringa Bw.Mawazo Marembeka akiomba kura kwa wanachama wa IPC katika nafasi ya uweka hazina japo hakuweza kupita baada ya kupata kura 7 kati ya 23 zilizopigwa
Mwandishi wa Chanel Ten Iringa Bw.Daud Mwangosi ameshinda nafasi ya uenyekiti IPC kwa kupata kura 12 kwa 11 alizopata mpinzani wake Sima
Afisa habari wa IMTV Iringa Bi.Sima Bingileki aliyekuwa mpinzani mkali wa Mwangosi katika kiti alishindwa kwa kura moja
Mwandishi wa The.Citizen na Radio Country fm Iringa Bw.Clement Sanga aliyekuwa mgombea wa nafasi ya ukatibu na kupata kura 6 kati ya 23 zilizopigwa hivyo kushindwa nafasi hiyo
Mwandishi wa magazeti ya serikali mkoa wa Iringa Bw.Frank Leonard amefanikiwa kutetea nafasi yake ya ukatibu kwa kpindi cha tatu mfululizo kwa kupata kura 17
Zulfa Shomari akijibu maswali ya wanachama ndani ya ukumbi wa Maktaba wakati wa uchaguzi mkuu wa IPC ,alikuwa akigombea nafasi ya umakamu mwenyekiti na kushinda nafasi hiyo kwa kishindo kwa kura 17 kati ya 6 alizopata mpinzani wake

Wanachama wa IPC wakipitia taarifa mbali mbali za chama kabla ya uchaguzi kutoka kushoto mbeli ni Frederick Siwale,Getrudde Madembwe na Anita Boma
Rais wa muungano wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Kenneth Simbaya akifungua mkutano mkuu wa uchaguzi ndani ya klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IPC) Simbaya ndiye alikuwa mwenyekiti wa IPC kabla ya kuamua kustaafu nafasi hiyo ,kushoto ni katibu mtendaji wa IPC Frank Leonard na kulia ni weka hazina wa IPC Sulemani Boki
Baadhi ya wanachama wa IPC wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi waliochaguliwa kuongoza IPC . Mwenye pama katikati ni  Bw Francis Godwin mmiliki wa mtandao mkubwa wa habari wa ambaye alipita bila kupingwa katika nafasi ya ukatibu msaidizi wa IPC

Katika uchaguzi huu viongozi walioanguka katika uchaguzi huo ambao walikuwemo katika safu ya uongozi katika uongozi uliopita ni pamoja na Sima Bingileki ambaye alikuwa makamu mwenyekiti,huku Eliasa Ally ambaye alikuwa mjumbe kipindi kilichopita akijitoa kugombea tena nafasi hiyo na Kenneth Simbaya akiamua kustaafu nafasi ya kiti pamoja na Hakimu Mwafongo ambaye hakugombea tena nafasi ya ukatibu msaidizi .

Katiba nafasi ya uweka hazina msaidizi Vicky Macha wa Nipashe Iringa alipita bila kupingwa huku nafasi ya katibu msaidizi pia Francis Godwin mwandishi wa gazeti la Tanzania daima Irina ,kurugenzi wa kampuni ya Free Community Media's na mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari za jinsia Tanzania (TGNP) mikoa ya kusini akipita bila kupingwa pamoja na wajumbe 13 7 wa kamati ya utendaji ndani ya IPC pia wakipita bila kupingwa kufuatia Eliasa Ally kujitoa katika kinyang'anyiro hicho.

Wajumbe 13 wanaounda kamati ya utendaji ndani ya IPC ni pamoja na Daud Mwangosi, Frank Leonard ,Zulfa Shomary, Francis Godwin, Suleman Boki,Vicky Macha, Getrude Madembwe, Shabani Lupimo, Frederick Siwale,Conard Mpila,Fulgence Malangalila,Janeth Matondo na Jackson Manga .

No comments: