Wednesday, April 20, 2011

SHEREHE ZA MIAKA 38 YA OKINAWA GOJU RYU KARATE DO NCHINI TANZANIA

Kepteni mstaafu wa JWTZ Sensei Geoffrey Shoo ambaye ni Chiefanaki Instructor wa Okinawa Den Goju Ryu Arnis, Kali na Escrima ambaye pia ni mwanasheria akielezea historia ujio wa sanaa hii ya kujilinda katika dojo kongwe kuliko yote nchini usiku huu katika hekalu la kujilinda lililopo katika shule ya msingi ya Zanaki jijini Dar es salaam wakati wa sherehe za miaka 38 ya dojo hili
Sensei Geoffrey Shoo akimtambulisha Sensei Brighton Manyau (shoto) ambaye ni mmoja wa wanafunzi wa kwanza wa muasisi wa Goju Ryu karate nchini hayati Namtambu Camara Bomani, akifuatiwa na Sensei Malekia, kiongozi mkuu wa Hekalu la Kujilinda
Sensei Malekia akiwatambulisha Chief Instructors (Sensei) wapya waliopandishwa daraja usiku huu. Toka kulia ni Sensei Geoffrey Mbezi, Sensei Rashi Almasi na Sensei Ndaukile Amri
Sensei Brighton Manyau akimvisha mkanda wa kijani mmoja wa vijana wanne waliopanda daraja toka mkanda mweupe
Sensei Manyau akimpandisha daraja mwanafunzi kijana
Sensei Manyau akimlisha keki Sensei Malekia
Sensei Sawayaeli Geoffrey Shoo akipata keki ya sherehe
Sensei Manyau akikata keki. Chini akimpandisha daraja Sensei Mbezi
Sensei Malekia akieleza jambo
Sensei Ndaukile Amri akipandishwa daraja

Masensei wakiwa na wanafunzi waliopandishwa daraja
Sensei Malekia akiwa na vijana wadogo waliopanda daraja toka mkanda mweupe kwenda wa kijani
Sensei Rashid Almasi akipandishwa daraja
Juu na chini wana Goju Ryu na wageni wakisimama kimya dakika moja kumkumbuka hayati Adam Lusekelo, mmoja wa wanafunzi wa awali hapo dojo

Producer wa muziki Ramal (kulia) akijiandaa kupiga kumite na mmoja wa wanafunzi waandamizi. Wadau toka kila fani ni wanafunzi katika dojo hili
Vijana wengi wanashiriki katika dojo hili
Ankal akiwa na masensei. Yeye pia kapitia mafunzo haya kwa miaka takriban 18





Kata ya Geki Sada Ichi
Kata ya Geki Sada Nii
Juu na chini ni namna ya kumdhibiti adui mwenye kisu
Kisu hakifuagi dau mbele ya mwana Goju Ryu... labda - labda - uje na cha moto...
Kinadada nao wamo kwa sana tu...
Mgeni rasmi Sensei Brighton Manyau akiongoza wanafunzi na wageni waalikwa katika mnuso
Wageni wakipatiwa mlo
Bondia veterani Iraq Hudu naye alikuwepo
Msosi wa nguvu


No comments: