Thursday, September 22, 2016

Tanzania yaahidi mazingira mazuri ya uwekezaji Sekta ya Madini



Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Japan nchini, Masaharu Yoshida (Wa pili kutoka kulia), Kaimu Kamishna wa Madini, Mhandisi Ally Samaje (Wa kwanza kushoto), Watendaji kutoka Serikali ya Japan na JOGMEC wakati wa semina iliyolenga katika uendelezaji endelevu wa rasilimali madini nchini.
Meneja wa Kanzidata na Uchakataji wa Taarifa za Jiolojia kutoka Wakala wa Jiolojia (GST), Terence Ngole akizungumza wakati wa Semina iliyoandaliwa na Shirika la Umma kutoka Japan linalojishughulisha na Mafuta, Gesi na Metali (JOGMEC), Wizara ya Uchumi, Biashara na Viwanda ya Japan, Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), pamoja na Wizara ya Nishati na Madini iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliyolenga katika uendelezaji Endelevu wa Rasilimali Madini nchini.
Balozi wa Japan nchini, Masaharu Yoshida (wa kwanza kulia) akimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe (hayupo pichani) akifungua Semina iliyoandaliwa na Shirika la Umma kutoka Japan linalojishughulisha na Mafuta, Gesi na Metali (JOGMEC), Wizara ya Uchumi, Biashara na Viwanda ya Japan, Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), pamoja na Wizara ya Nishati na Madini iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliyolenga katika uendelezaji Endelevu wa Rasilimali Madini nchini.
Wadau mbalimbali waliohudhuria Semina iliyoandaliwa na Shirika la Umma kutoka Japan linalojishughulisha na Mafuta, Gesi na Metali (JOGMEC), Wizara ya Uchumi, Biashara na Viwanda ya Japan, Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), pamoja na Wizara ya Nishati na Madini iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliyolenga katika uendelezaji Endelevu wa Rasilimali Madini nchini.
Wadau mbalimbali waliohudhuria Semina iliyoandaliwa na Shirika la Umma kutoka Japan linalojishughulisha na Mafuta, Gesi na Metali (JOGMEC), Wizara ya Uchumi, Biashara na Viwanda ya Japan, Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), pamoja na Wizara ya Nishati na Madini iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliyolenga katika uendelezaji Endelevu wa Rasilimali Madini nchini.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe akifungua Semina iliyoandaliwa na Shirika la Umma kutoka Japan linalojishughulisha na Mafuta, Gesi na Metali (JOGMEC), Wizara ya Uchumi, Biashara na Viwanda ya Japan, Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), pamoja na Wizara ya Nishati na Madini iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliyolenga katika uendelezaji Endelevu wa Rasilimali Madini nchini.


Teresia Mhagama na Devotha Myombe

Tanzania imeahidi kuendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji katika Sekta ya Madini kama ilivyoainishwa katika Sera ya Madini ya mwaka 2009.

Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe wakati wa semina iliyoandaliwa na Shirika la Umma kutoka Japan linalojishughulisha na Mafuta, Gesi na Metali (JOGMEC), Wizara ya Uchumi, Biashara na Viwanda ya Japan, Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), pamoja na Wizara ya Nishati na Madini iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliyolenga katika uendelezaji endelevu wa rasilimali madini nchini.

Alisema kuwa, Dira ya Maendeleo ya Mwaka 2025 imelenga katika kuanzisha migodi mikubwa, ya kati na midogo inayoendeshwa kwa kuzingatia usalama na utunzaji wa mazingira hivyo mazingira mazuri ya uwekezaji yatavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza ili kuendeleza Sekta ya Madini nchini.

Profesa Mdoe alisema kuwa semina hiyo ililenga katika kupata taarifa zilizohuishwa kutoka Japan na Tanzania kuhusu shughuli za utafiti na utunzaji wa mazingira katika Sekta ya Madini nchini na kujadiliana juu ya kuendeleza ushirikiano kati ya nchi husika.

“Semina hii ni muhimu kwani Taasisi hizi zitajadiliana kuhusu kuendeleza ushirikiano katika sekta hii, kufahamu fursa za uwekezaji kwenye Sekta ya Madini kwani wadau kutoka Tanzania na Japan wataweza kupata taarifa za utafiti kuhusu madini yaliyopo nchini na pia Taasisi ya JOGMEC itapata fursa ya kueleza shughuli zake barani Afrika,” alisema Profesa Mdoe.

Akieleza kuhusu Sekta ya Madini nchini, Profesa Mdoe alisema kuwa Sekta hiyo kwa sasa inachangia asilimia 3.5 katika Pato la Taifa na kueleza kuwa asilimia hiyo bado ni ndogo kwani lengo la Serikali ni kuona kuwa Sekta hiyo inachangia mpaka asilimia 10 kufikia mwaka 2025.

Hata hivyo Profesa Mdoe alisema kuwa ili sekta hiyo ichangie ipasavyo katika Uchumi wa Taifa, kutategemea kutoshuka kwa bei ya bidhaa zinazotokana rasilimali madini na uchumi wa dunia kuendelea kukua ili makampuni yanayojishughulisha na utafiti na uchimbaji wa madini yapate fedha kutoka Taasisi za kifedha duniani ili kuanzisha shughuli za utafiti na uchimbaji wa madini.

Aidha Profesa Mdoe aliwaalika wawekezaji kujenga vituo vitakavyotumika katika shughuli za uongezaji thamani madini ya Tanzania kwani alisema kuwa uongezaji thamani madini ndani ya nchi utasaidia kuongeza ajira kwa wananchi, ubadilishanaji wa teknolojia kutoka nchi zilizobobea katika shughuli hizo na kuwezesha ukusanyaji wa kodi ambayo itasaidia katika shughuli nyingine za maendeleo.

Awali Meneja wa Kanzidata na Uchakataji wa Taarifa za Jiolojia kutoka GST, Terence Ngole, alieleza JOGMEC na GST walisaini Mkataba wa Makubaliano mwaka 2010 ambapo mashirikiano kati ya Taasisi hizo yamesaidia kuongeza utaalam na teknolojia katika utafiti wa madini kupitia mafunzo mbalimbali ya muda mrefu na mfupi yanayotolewa na Shirika la JOGMEC.

Alisema kuwa Semina hiyo imeshirikisha wadau mbalimbali kutoka Japan na Tanzania ambao wanajishughulisha na Sekta ya Madini na Mazingira na kwamba ni semina ya kwanza kuendeshwa nchini na Shirika la JOGMEC.


No comments: