Tuesday, August 9, 2016

matukio mbalimbali ya Maonesho ya nanenane yaliyofanyika kitaifa kwenye viwanja vya Ngongo mkoani Lindi

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akipokea maelezo mbalimbali kutoka kwa Mhandisi Diana Munubi, jana katika banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kwenye maonesho ya Nanenane Kitaifa mkoani Lindi, kabla ya kufungwa na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akiwaeleza jambo washiriki wa maonesho ya Nanenane wa banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), alipotembelea jana kwenye viwanja vya Ngongo mkoani Lindi. Maonesho hayo yalifungwa na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Mkuu wa mkoa wa Lindi, Mhe. Geofrey Zambi (wa kwanza kulia) akipokea maelezo mbalimbali kutoka kwa Mhandisi Diana Munubi (wa pili kushoto), wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kwenye maonesho ya Nanenane mkoani Lindi, ambapo yalifikia kilele jana na kufungwa na Mhe. Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan .
Bi. Fatma Matimba (kulia) akitoa maelezo kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Lindi, juu ya ufanyaji wa kazi wa kifaa cha ukaguzi wa abiria kabla ya kuingia eneo la kwenda kupanda ndege, walipotembelea banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), katika maonesho ya Nanenane kitaifa Lindi.
Bi. Nuru Nyoni (kulia) akitoa maelezo ya kifaa cha ukaguzi kwa mkazi wa Lindi, alipotembelea banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika kwenye viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.
Bi. Bahati Mollel (kushoto) akiwafafanulia jambo wanafunzi wa shule ya sekondari ya Ngongo juu ya viwanja vya ndege vilivyo chini ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), walipotembelea banda la mamlaka hiyo katika maonesho ya Nanenane kitaifa mkoani Lindi.
Bi. Janet Mugini (kushoto) akitoa maelezo mbalimbali kwa mkazi wa Kilwa, aliyetembelea banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa mkoani Lindi.
Bw. Edward Kimaro (kulia) akimwelekeza mkazi wa Lindi namna ndege inavyopaa baada ya kutembelea banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, katika maonesho ya Nanenane kitaifa mkoani Lindi, yaliyofungwa na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Wananchi wakipata maelezo mbalimbali kwenye banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mkoani Lindi.
Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Lindi, Bw. Boniface Njanda akitoa maelezo mbalimbali kwa Mwananchi aliyetembelea banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa Lindi.

No comments: