Thursday, August 11, 2016

ACTIVISTA TANZANIA WAADHIMISHA SIKU YA VIJANA DUNIANI

Mkurugenzi wa DOT Tanzania, Dawson Luogard akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya siku ya vijana leo katika ukumbi FES Oyster Bay jijini Dar es Salaam.
Mtandao wa Vijana wa Activista Tanzania wakishirikiana na Tanzania Youth Vision Association(TYVA) wameadhimisha siku ya Vijana Duniani kwa kuwakutanisha vijana zaidi ya 120 kutoka maeneo mbalimbali na kujadili mada mbalimbali kuhusu Kodi, Kilimo na Maendeleo Endelevu ya malengo ya millenia.(Picha na Geofrey Adroph)
Mkurugenzi wa Jielimishe Kwanza, Henry Kazure akitoa mafunzo kwa vijana waliofika katika maadhimisho ya siku ya vijana katika ukumbi wa FES yaliyoandaliwa na Activista Tanzania wakishirikiana na TYVA.

Katibu wa Actvista Tanzania, Maria Kayombo ambaye alikuwa mshereheshaji akizungumza jambo wakati wa maadhimisho ya Siku ya vijana yaliyofanyika katika ukumbi wa FES Oyster Bay jijini Dar es Salaam
Baadhi ya vijana wakifuatilia mada
Mratibu wa Kwanza wa Activista Tanzania, Elly Ahimidiwe akizungumza na vijana waliofika katika maadhimisho ya siku ya vijana yaliyoandaliwa na Mtandao wa vijana wa Activista Tanzania wakishirikiana na TYVA.
Baadhi ya Vijana waliofika katika maadhimisho ya siku ya Vijana wakisikiliza mada zinazoendelea katika ukumbi wa FES Oster Bay jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Activista Tanzania, Hatibu Kilenga akifunga mafunzo kwa vijana yaliyoandaliwa na Mtandao wa Vijana wa Activista Tanzania wakishirikiana na Tanzania Youth Vision Association(TYVA) katika maadhimisho ya siku ya Vijana Duniani.
Picha ya Pamoja

No comments: