Thursday, June 2, 2016

YALIYOJIRI BUNGENI MJINI DODOMA LEO JUNI 3, 2016

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (kushoto), Mhe. Margaret Sitta Mbunge wa Urambo (katikati) na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura wakielekea ndani ya Ukumbi wa Bunge, Dodoma leo.
Baadhi ya Waheshimiwa wabunge wakiingia ndani ya Ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma.

Baadhi ya Waheshimiwa wabunge wakiingia ndani ya Ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Tulia Ackson akiendesha kikao cha 35 cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo mjini Dodoma.
Mchezaji wa kulipwa wa mpira wa kikapu nchini Marekani kutoka Tanzania Hasheem Thabeet (kulia) akiwa na baadhi ya wageni mbalimbali waliolitembelea Bunge leo.
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe akichangia jambo wakati wa kikao cha 35 cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo.
Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Masauni akijibu maswali ya wabunge wakati wa kipindi cha maswali na majibu Bungeni Dodoma.
Baadhi ya Wabunge na Mawaziri wakifuatilia masuala mbalimbali ndani ya ukumbi wa Bunge wakati wa kikao cha 35 cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Tulia Ackson (kulia) akisalimiana na Meneja wa VETA mkoa wa Iringa Bw. Maganga nje ya Ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma.Katikati ni Mbunge wa Kilolo Mhe. Venance Mwamoto.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Tulia Ackson (kulia) akizungumza jambo na Meneja wa VETA mkoa wa Iringa Bw. Maganga (kushoto) na Mbunge wa Kilolo Mhe. Venance Mwamoto nje ya Ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma.
Mchezaji wa kulipwa wa mpira wa kikapu nchini Marekani kutoka Tanzania Hasheem Thabeet (kushoto) akifurahia jambo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju (wa pili kutoka kushoto) na baadhi ya Wabunge nje ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Haki , Maadili na Madaraka ya Bunge na Mbunge wa Newala Mhe. George Mkuchika (katikati) akizungumza jambo na Mbunge wa Iringa Mjini Mhe. Peter Msigwa nje ya Ukumbi wa Bunge Dodoma.Kulia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimsisitiza jambo Meneja wa VETA mkoa wa Iringa Bw. Maganga nje ya Ukumbi wa Bunge Dodoma.
Kiongozi wa Kambi ya Upinzania Bungeni Mhe. Freeman Mbowe akifurahia jambo na Mbunge wa Mtera Mhe. Livingstone Lusinde nje ya Ukumbi wa Bunge, Dodoma.
Wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Venance Mwamoto (wa pili kutoka kulia), , Mhe. Livingstone Lusinde (wa tatu kutoka kulia) na Mhe. Joseph Kasheku Msukuma ( pili kutoka kushoto)wakifurahia jambo na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Mhe. Freeman Mbowe nje ya Ukumbi wa Bunge leo.
Mbunge wa Kilolo Mhe. Venance Mwamoto (wa pili kutoka kulia), Mbunge wa Mtera Mhe. Livingstone Lusinde (wa tatu kutoka kulia) na Mbunge wa Geita vijijini Mhe. Joseph Kasheku Msukuma ( pili kutoka kushoto)wakimweleza jambo Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Mhe. Freeman Mbowe nje ya Ukumbi wa Bunge leo.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi (Kulia) akizungumza jambo na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni leo mjini Dodoma.Picha na Aron Msigwa na Fatma Salum–MAELEZO, DODOMA.

No comments: