Thursday, May 12, 2016

Watano waingia kwenye fainali za Airtel Trace Music Stars

 Mkufunzi na Mwalimu wa Sauti Tony Joett akitoa mafunzo ya sauti kwa washiriki waliochaguliwa kuingia tano bora katika fainali za  shindano la Airtel Trace Music Stars zilizopangwa kufanyika tarehe 20 mei 2016 hapa jijini Dar es Saalam. . Mshindi ataondoka na zawadi ya shilingi milioni 50 na kupata nafasi ya kuiwakisha Tanzania katika mashindano ya Afrika yatakayofanyika nchini Nigeria
 Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde (wa pili kulia) wakijipongeza kwa pamoja na washiriki waliochaguliwa kuingia tano bora katika  shindano la Airtel Trace Music Stars ambapo fainali zake zitakafanyika tarehe 20 mei 2016 hapa jijini Dar es Saalam. Mshindi ataondoka na zawadi ya shilingi milioni 50 na kupata nafasi ya kuiwakisha Tanzania katika mashindano ya Afrika yatakayofanyika nchini Nigeria
Washiriki waliochaguliwa kuingia tano bora katika  shindano la Airtel Trace Music Stars wakifurahia ushindi huo uliowapa tiketi ya kuingia katika fainali zitakafanyika tarehe 20 mei 2016 hapa jijini Dar es Saalam. Mshindi ataondoka na zawadi ya shilingi milioni 50 na kupata nafasi ya kuiwakisha Tanzania katika mashindano ya Afrika yatakayofanyika nchini Nigeria.  Kutoka kushoto ni Benny Sule, Nicole Grey, Salim Mlindila,  Nandi Charles na Melisa Elina John

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetangaza washiriki waliongia kwenye tano bora katika shindano kubwa Afrika la kusaka vipaji vya muziki lijulikanalo kama Airtel Trace Music Stars.

Ikiwa ni miezi mitatu tangu kuanza kwa msimu wa pili wa shindano la Airtel Trace Music Stars na kushirikisha  maelfu ya vijana wa kitanzania, Airtel imetangaza majina ya washiriki wa tano bora walioingia kwenye fainali za kitaifa ambao ni pamoja na Benny Sule, Nicole Grey, Nandi Charles, Melisa Elina John na Salim Mlindila.

Washiriki hawa walichaguliwa na jopo la majaji  mahiri akiwemo mtangazaji wa TV mahiri, Mwanamuzi, Mwigizaji na msanii aliyejikita katika maeneo mengi, Jokate Urban Mwegelo,  mtunzi wa nyimbo na mwalimu wa sauti Tony Joett pamoja na mtengenezaji wa Muziki na mfanyabiashara Luciano Gadie Tsere.

Akitangaza walioingia tano bora, Afisa Uhusiano wa Airtel , Jane Matinde  aliwapongeza washiriki hao kwa kufika katika hatua ya fainali na kusema “ msimu wa pili wa shindano la Airtel Trace Music Stars umekuwa ni wa mafanikio makubwa na leo tunayo furaha kutangaza majina ya washiriki waliofanya vizuri zaidi na kuwa kwenye nafasi ya kushinda na  kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Airtel Trace Music Stars ya Afrika”.

“Tunaamini Airtel Trace Music Stars ni  Fursa muhimu ya kuwainua wanamuziki chipikizi kuweza kuonyesha vipaji vyao na hatimae kuzifikia ndoto zao. Airtel itaendelea kuwawezesha vijana wa kitanzania kutambua uwezo wao na kuishi ndoto zao na shindano hili la Airtel Trace Music Stars ni kielelezo tosha cha dhamira hii”. Aliongeza Matinde

Kwa upande wake mmoja ya washiriki waliotinga tano bora , Benny Sule alionyesha furaha yake ya kufika katika finali na kusema “ mashindano haya yamenipa Fursa kubwa kiasi ambacho nashindwa kuelezea. Nimejipanga vyema kushiriki katika fainali zinazofanyika wiki ijayo na natumaini kushinda na kuiwakilisha vyema nchi yangu

Aliongeza kwa kusema “Huu ni mwanzo mzuri wa safari yangu ya kuwa mwanamuziki nyota ndani na nje ya nchi. Nawashukuru sana Airtel kwa mpango huu ambao umewawezesha vijana wengi barani Afrika  kuonyesha vipaji vyao na kuzifikia ndoto zao.”

Washiriki waliongia tano bora wanategemea kushindana katika kinyanganyiro cha mshindi wa Airtel Trace Music Stars wa Tanzania katika finali zitakazofanyika tarehe 20 Mei 2016.  Mshindi ataondoka na zawadi ya shilingi milioni 50 na kupata nafasi ya kuiwakisha Tanzania katika mashindano ya Afrika yatakayofanyika nchini Nigeria ambapo atapata nafasi ya kushinda na kusaini mkataba wa  mafunzo.

Tunatoa wito kwa watanzania kuwapiigia kura washiriki ili kupata mshindi atakayetuwakalisha vyema  katika mashindano ya Afrika, ili kupiga kura weka jina la fumbo (nickname) ya mshiriki kisha tuma kwenda namba 15594 .  zifuatazo ni jina la fumbo (nickname ) za washiriki  Beny  Sulle “Ben”, Nicole Grey “Nic, Nandi Charles”Nan”,Melissa John “Mel”na Salim Mlindila “Sal”.

No comments: