Monday, April 11, 2016

MRADI WA KAIZEN KUTOKA JAPAN KUKUZA UZALISHAJI NA UBORA WA BIDHAA NCHINI

Waziri wa Viwanda na Biashara Mh. Charles Mwijage akizungumza na kukaribisha Ujumbu wa Wataalamu kutoka nchini Japani katika mradi wa ushauri wa kuwekeza katika Rasirimali watu na vitendeakazi ili kuzalisha kwa tija na ubora wa bidhaa kupitia mradi wa KAIZEN ili kuwekeza zaidi kwa namna unavyozalisha na kufanya kazi kwa tija, wakati wataalamu hao walipokutana na Waziri huyo wataalamu mbalimbali wa Wizara ya Viwanda na Biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo mwishoni mwa wiki.

Waziri Mwijage amesema wataalamu hao wanashauri mambo mengi katika uzalishaji wa bidhaa na kilimo kama vile kuwapa uelewa zaidi wataalamu na wajasiriamali wenyewe ili kuwekeza katika viwanda na kilimo kwa tija na ubora ili kufikia malengo ya kuwafanya watu kuwekeza kwa tija na ufanisi, Ukielewa namna nzuri ya uwekezaji wenye tija na ubora utaweza kufaidika na uwekezaji wako bila kutumia nguvu na gharama kubwa sana bila mafanikio.

Katika picha kulia ni Profesa Tetsushi Sonobe Makamu wa rais wa Shirika la GRIPS la Japan na katikati ni Profesa Toshio Nagase Mwakilishi wa shirika la JICA nchini Tanzania.
Profesa Toshio Nagase Mwakilishi wa shirika la JICA nchini Tanzania akitoa utambulisho wa ujumbe aliofuatana nao katika mkutano huo uliofanyika katika Wizara ya Viwanda na Biashara mwishoni mwa wiki.
Profesa Tetsushi Sonobe Makamu wa rais wa Shirika la GRIPS la Japan akiwasilisha maelezo ya mradi huo kwa wataalamu wa Wizara ya Viwanda na biashara. 
Bw. Takao Kikuchi Mshauri Mkuu wa mradi wa KAIZEN nchini akichangia jambo katika mkutano huo uliohudhuriwa na wataalamu mbalimbali kutoka wizara ya viwanda na biashara na Japan.
Wataalamu mbalimbali kutoka Shirika la Maendeleo la Japan JICA na Mradi wa KAIZEN wakifuatilia mazungumza katika mkutano huo.
Wataalamu kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara wakisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa wataalamu wa Japan wakati mkutano huo ukiendelea.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)

No comments: