Monday, April 4, 2016

KAMANDA SIRO AZUNGUMZIA MIKAKATI YA OPERESHINI YA KUPAMBANA NA UHALIFU PAMOJA NA BODA BODA

Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro  akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo kuhusina na Operesheni ya kukamata Pikipiki519 pamoja na gari lililokuwa na Vitenge marobota 10 na Pampers katoni17 katika eneo la Gezaulole pemeni mwa ufukwe wa bahari ya hindi ambapo eneo hilo linatumika kupitisha mali zisizolipiwa ushuru.

Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro akionyesha Baadhi ya Vitenge na Pempers zilizokamatwa katika operesheni ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro akionyesha gari lilokamatwa na vitenge na Pampers.
Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro akionesha pikipiki 519 ambazo zimekamatwa ja jeshi la Polisi kanda Maalum ya Dar es Salaam.
Kamanda Sirro akionesha mali zilizokamatwa katika Operesheni hiyo ya kupambana na Uhalifu,mbele ya Waandishi wa Habari,leo jijini Dar.
Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro akizungumza mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo jijini Dar,kuhusiana na suala zima la Operesheni ya kupambana na Uhalifu pamoja na Bodaboda.

.....UPDATES......
Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
JESHI la Polisi kanda Maalumu ya Dar es Salaam limekamata Marobota 10 ya vitenge na Katoni 17 za Pampers  pamoja na Gari lililotumika kubebea hitu hivyo katika eneo ya Gezaulole lililopo pembezoni mwa ufukwe wa bahari ya Hindi.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, amesema kuwa kukamatwa kwa gari lenye vitu hivyo ni mara baada ya kupewa taarifa na Raia wema kwa kuwa katika eneo hilo kunapitishiwa mali zisizotolewa ushuru.

Siro amesema kuwa Gari lililo kamatwa na Vitenge na Pampers ni aina ya Suzuki Carry lenye namba za usajili T490 CQB ambalo nalo linashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam.

Pia Sirro amesema kuwa mwananchi anaeona kuwa alitelekeza gari hilo lililo na vitu hivyo ajisalimishe Polisi ili apelekwe Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) akalipie ushuru wa vitu hivyo.

Katika Operesheni nyingine Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam lilifanikiwa kukamata gari moja la wizi aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T 314 DFH  ambapo kabla ya kuibwa lilikuwa na namba za usajili T 622 DDR  ikiwa gari hilo ni Mali ya Hellen Michael liliibwa maeneo ya Kitunda Kivule ambapo lililuwa limeegeshwa nyumbani kwake. Pia Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam limkamata watu wawili wakiwa na Pikipiki mbili zenye namba za usajili MC343 ASL aina ya Boxer na MC 606 ex aina ya Fercon ambazo ni za wizi na watuhumiwa hao kukuli kuwa wameziiba Pikipiki hizo.


Jeshi la Polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam kwa kipindi cha wiki moja limefanikiwa kukamata Pikipiki 519 katika Operesheni ya ukamataji wa Pikipiki kwa makosa mbalimbali operesheni hiyo ilifanywa katika mikoa ya Ilala piki[iki 183,Kinondoni pikipiki 139 na Temeke pikipiki 197.

No comments: