Tuesday, December 1, 2015

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

Baadhi ya wakazi waliokuwa wakifata miili ya ndugu zao katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya mkoa wa Kilimanjaro watishia kususia miili ya ndugu zao kufuatia kukuta miili hiyo ikiwa imeharibika. https://youtu.be/NEid_i3cmG8

Vijana waojihusisha na uchimbaji mchanga na kuponda kokoto katika manispaa ya Lindi walalamikia agizo la mkuu wa wilaya ya Lindi la kufunga machimbo kwa sababu za kiusalama. https://youtu.be/EkM00PlfV2s

Mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji EWURA yatangaza punguzo la bei ya mafuta huku bei ya mafuta ya taa ikipanda zaidi. https://youtu.be/lkZ-vXXvO5U

Imeelezwa kuwa hivi karibuni wanawake ndio wanao jihusisha na biashara zaidi kuliko wanaume mkoani Kilimanjaro https://youtu.be/wEyKHHdbHU0

Makamo wa kwanza wa rais visiwani Zanzibar Balozi Seif Idd atembelea eneo la mradi mkubwa wa kitalii visiwani humo unaomilikiwa na kampuni ya Bakhressa Group.https://youtu.be/e57f7zmfATc

Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM na mbunge wa Mtama Nape Nauye azungumzia kasi ya Rais Magufuli huku akisisitiza chama hicho kinamuunga mkono na kumtaka aendelee zaidi. https://youtu.be/V6-whGYuYEg

Baadhi ya wananchi mkoani Mwanza wanaishutumu hospitali ya Sekou Toure kwa kufanya uzembe wa kuhifadhi chini mwili marehemu Baraka Hamisihttps://youtu.be/llp423vJmfQ

Leo siku ya maadhimisho ya Ukimwi duniani,wataalamu waeleza kuwa jitihada za kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI nchini bado zinahitajika ili kufanikisha lengo; https://youtu.be/i400NH3V0h0

Kampuni ya uchimbaji madini ya SASUMUA imegundua uwepo wa kiasi kikubwa cha madini aina ya Graphite wilayani Handeni mkoani Tanga; https://youtu.be/iXXzCUh5L-0

Mashabiki wa soka nchini wametoa maoni yao kuhusu Kilimanjaro Stars kuondolewa katika michuano ya Challenge inayoendelea nchini Ethiopia;https://youtu.be/yc2gbCd60pI

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro amepiga marufuku uuzaji wa samaki wadogo katika soko la Manyema akidai kuwa inahatarisha ukuaji wa samaki hao katika bwawa la nyumba ya Mungu; https://youtu.be/HshkLpCiFLI

Kampuni ya uchambaji wa madini ya Tanzanite one ya mkoani Manyara inatarajia kupunguza wafanyakazi takribani 635 kufutia kupungua kwa uzalishajihttps://youtu.be/gcpPhJv5qMQ

Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mhe.Rajabu Rutengwe amewataka watumishi wa umma kununua nyumba zilizojengwa na kampuni ya watumishi housing;https://youtu.be/-2PMLg5H8jo

Waumini wa dini ya kiislam katika msikiti wa Mtambani jijini Dar es salaam wamlaki kwa furaha katibu wa jumuiya na taasisi za kiislam, Sheikh Issa Ponda baada ya kushinda kesi. https://youtu.be/y6kEHlaTDtI

Katibu mkuu wizara ya uchukuzi Shaban Mwinjaka aiagiza kampuni ya reli ya TRL kufufua kiwanda cha kutengeneza vipuli badala ya utaratibu wa sasa wa kuagiza vipuli hivyo kutoka Afrika kusini. https://youtu.be/Ikz6JD9FpTo

Serikali imeanza uchunguzi dhidi ya benki ya Stanbic ya hapa nchini pamoja na kampuni ya Egma inayomilikiwa na kamishna wa zamani wa TRA kufuatia benki hiyo kuongeza malipo yenye utata kwa kampuni ya Egma https://youtu.be/RipBwRepcU8

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadick azindua wiki ya usafi wa mazingira kwa mkoa wa Dar es salaam ikiwa ni kuelekea kilele cha maadhimisho ya uhuru.https://youtu.be/3u-dCsN-ePw

Zoezi la upanuzi wa barabara ya Mwenge mpaka Morroco laanza kutekelezwa kufuatia agizo la Rais Magufuli kuelekeza fedha zilizotengwa kwa ajili sherehe za uhuru zitumike kujenga barabara hiyo. https://youtu.be/Gwd_bSgmVj4

Mamlaka ya mapato Tanzania kwa kushirikiana na TPA pamoja na jeshi la wapolisi wakamata makontena 9 yanayosadikiwa kukwepa kodi.https://youtu.be/CDg3u79bZ0E

No comments: