Friday, December 25, 2015

SHEREHE YA MAULIDI MAKUU YA MTUME MUHAMMAD(S.A.W) ILIVYOFANA VISIWANI ZANZIBAR

Wanamadrasa wakipiga dufu kukaribisha wageni na Viongozi wakati wa sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja ambayo hufanyika kila mwaka.
Makamo wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dkt.Mohammed Gharib Bilali akisalimiana na Sheikh Kassim Haidar Jabir mjumbe wa Kamati ya Maandalizi alipowasili katika sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na viongozi mbali mbali alipowasili katika sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mwanasheria Mkuu Zanzibar Sheikh Said Hassan Said pamoja na viongozi mbali mbali alipowasili katika sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad alipowasili katika sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohamed Gharib Bilal alipowasili katika sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji Khamis, Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad (kushoto) na Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali wakiwa katika sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji Khamis, Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad (kushoto) na Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali pamoja na Viongozi wengine wakiwa katika sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein (katikati) akiangalia ratiba ya Maulidi ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika Viwanja vya Maisara Suleiman Mjini Unguja akiwa Viongozi mbali mbali na wananchi.
Baadhi ya Akina Mama wa Kiisalmu wakiwa katika sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja ambayo hufanyika kila mwaka.
Wanafunzi wa Madrasa mbali mbali za Zanzibar wakiwa katika sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja,ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein.
Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji Khamis alipokuwa akitoa historia fupi wakati wa ufunguzi wa sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja,ambapo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) akiwa ndio mgeni rasmi katika sherehe hiyo.
Ustadh Juma Seif Said Hamad kutoka Mkoa wa Kaskazini Unguja akisoama Qur'aan Tukufu Surah Luqman Aya 33hadi 34 za ufunguzi wa Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja.

Wanafunzi wa Madrasat Nurul Islamia ya Jang'ombe -Mkoa wa Mjini wakisoma Qasweeda baada ya mlango wa kwanza wa sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja.
Ustadh Rashid Hamadi Bakari kutoka Muungoni Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja akisoma mlango wa kwanza wa Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) pamoja na Viongozi mbali mbali wakisiamama kumswalia Mtume wakati wa Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwake Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akitiliwa marashi pamoja na Viongozi mbali mbali wakati wa kumswalia Mtume katika sherehe za Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwake Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika uwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein (katikati) pamoja na Wake wa Viongozimbali mbali wakisimama kumswalia Mtume wakati wa Maulidi Makuu ya kuzaliwa kwake Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika viwanja wa Maisara Suleiman Mjini Unguja.Picha na Ikulu, Zanzibar.

No comments: