Wednesday, December 30, 2015

NAIBU WAZIRI WA HABARI,UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO, ANNASTAZIA WAMBURA ATEMBELEA TCRA LEO JIJINI DAR.

Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Annastazia Wambura akipewa maelekezo na Naibu Mkurugenzi wa maswala ya utangazaji wa Televisheni wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Frederick Ntobi mara baada ya kutembelea chumba cha maswala ya mawasiliano hasa ya Televisheni  leo jijini Dar es Salaam.
Naibu Mkurugenzi wa maswala ya Posta wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Haruni Lemanya akizungumza na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Annastazia Wambura pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) leo jijini Dar es Salaa mara baada ya Naibu waziri kutembelea katika ofisi ya Maswala ya Posta katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.
 Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) WA kitengo cha TTMS, Mhandisi Gabriel Mruma akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Annastazia Wambura kutembelea katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.  
Baadhi ya Kazi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) kwa upande wa mitandao ya Simu za mkononi na maswala ya Miamala ya Pesa katika mitandao ya simu kilichopo katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Annastazia Wambura akizungumza na wafanyakazi pamoja na wakurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya waandishi wa habari na wakurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wakimsikiliza Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Annastazia Wambura jijini Dar es Salaam leo.

No comments: