Thursday, December 17, 2015

Mwili wa marehemu Dotto Mzava wa Jamii Forums wasafirishwa kuelekea Same Kilimanjaro kwaajili ya mazishi

 Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Dotto Mzava likishushwa Kwenye gari maalum mara baada ya kuwasili katika kanisa la Wasabato Manzese uzuri kwaajili ya sala ya kuombea kabla ya Mwili kusafirishwa kuelekea Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro.
 Mchungaji wa kanisa la Adventist wasabato akiendelea na ibada wakati wa ibada ya kumuombea marehemu kabla ya kusafirishwa kuelekea Same Kilimanjaro
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Jamii Media Maxence Mello akitoa historia fupi ya Marehemu Dotto Mzava ambae pia alikua mmoja wa watumishi katika kampuni hiyo.
Baba Mkubwa wa marehemu Dotto Mzava akitoa maneno ya shukrani katika kanisa la Kisabato la Manzese Uzuri mara baada ya zoezi la misa kumalizika.
 Heshima za Mwisho zikiendelea kutolewa
 Majonzi na simanzi kwa ndugu wa marehemu
 Mmiliki wa Fullshangwe Blog,John Bukuku akitoa heshima za mwisho
 Heshima za mwisho zikiendelea kutolewa kwa mwili wa marehemu Dotto Mzava kabla haujasafirishwa kuelekea Same Kilimanjaro kwaajili ya mazishi
 Mbunge wa Jimbo la Kibamba, John Mnyika akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu Dotto Mzava kabla ya Kusafirishwa kuelekea Same Kilimanjaro kwa mazishi yanayotarjiwa kufanyika kesho
 Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media akitoa heshima za mwisho kabla ya mwili wa marehemu kusafirishwa Same Mkoani Kilimanjaro mapema leo
 Ibada ikiendelea
 Jeneza lenye mwili wa marehemu Dotto Mzava likipandishwa ndani ya gari tayari kwa safari ya kuelekea Same Mkoa wa Kilimanjaro leo kwaajili ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho
 Ndugu, jamaa na marafiki wakiwa kanisani
 Kwaya ya Angaza ikitoa huduma wakati wa ibada ya kumuombea marehemu Dotto Mzava
Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Dotto Mzava wakiwa kanisani kwenye ibada ya kumuombea marehemu iliyofanyika katika kanisa la Wasabato la Manzese Uzuri kabla ya Mwili kusafirishwa kwaajili ya kwenda kupumzishwa katika nyumba yake ya milele huko Kwao Same Mkoa wa Kilimanjaro.Picha na Pamoja Blog

No comments: