Friday, September 4, 2015

MPIGIENI KURA MAGUFURI-MAMA SALMA KIKWETE




 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi, (CCM) wa Wilaya ya Lindi na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongozana na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini Ndugu Hassan Suleiman Kaunje wakiwapungia mikino mamia ya wananchi waliohudhuria sherehe ya uzinduzi rasmi wa kampeni kwenye Jimbo kwenye uwanja wa Fisi uliopo Manispaa ya Lindi tarehe 3,9.2015.
 Baadhi ya wanachama na wananchi katika Manispaa ya Lindi wakishangilia wakati Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM anayewakilisha Manispaa hiyo Mama Salma Kikwete na viongozi wengine wakiingia uwanjani hapo.
 Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM anayewakilisha Lindi Manispaa Mama Salma Kikwete akipokea kadi kutoka kwa aliyekuwa mwanachama wa CUF na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mitandi Ndugu Laibu Kaisi aliyeamua kurejea Chama Cha Mapinduzi wakati wa sherehe za uzinduzi rami za kampeni za Chama hicho katika Manispaa hiyo.

 Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa ya Chama cha Mapinduzi Mama Salma Kikwete akihutubia mamia ya wananchi wa Lindi Manispaa wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na Madiwani utakaofanyika tarehe 25.10.2015 
  Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimtambilisha rasmi Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi katika Manispaa ya Lindi Ndugu Hassan Suleiman Kaunje kwa wanachama wa CCM na wananchi wakati akizindua rasmi kampeni hizo kwenye uwanja wa Fisi huko Lindi tarehe 3.9.2015.
 Mke wa Rais MamaSalma Kikwete akimkabidhi Ndugu Hassan Kaunje ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni hizo tarehe 3.9.2015.
 Baadhi ya vijana wakimshangilia kwa vifijo Ndugu Hassan Kaunje, Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi mara baada ya kumalizika kwa sherehe za uzinduzi rasmi wa kampeni hizo katika Wilaya ya Lindi Mjini tarehe 3.9.2015.

 Na Magreth Kinabo –Maelezo,Lindi
MKE wa Rais Mama Salma Kikwete amewataka wananchi wa Jimbo la Lindi Mjini  kuhakikisha kwamba wanapiga kura ya ndiyo kwa mgombea wa kiti cha urais,Dkt. John Magufuli , mgombea kiti cha Ubunge Hassan Kaunje na wagombea viti cha udiwani  ili waweze kupata maendeleo.
Kauli hiyo imetolewa jana jioni na Mama   Kikwete ,ambaye  pia  ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya     Taifa ya  Chama Cha Mapinduzi(NEC) wa Wilaya Lindi ,wakati wa uzinduzi  wa kampeni ya chama hicho ya wilaya hiyo ili  iliyoambatana na uzinduzi wa Ilani ya CCM kwa lengo la kuinadi  na kuwanadi wagombea hao iliyofanyika kwenye uwanja wa Fisi.
“Leo nimekuja kufanya kazi hii moja  ya kuhakikisha mgombea wa kiti cha urais,  anashinda akiwemo  mgombea wa kiti cha ubunge na wagombea  wa viti  vya  udiwani,” alisema Mama Kikwete huku akiinadi picha ya mgombea wa kiti cha urais  na kumnadi mgombea wa kiti cha Ubunge  na wagombea viti vya  udiwani katika kata mbalimbali kupitia chama hicho.
 Mama Kikwete  aliongeza kwamba  ikiwa kila mtu atatoka na kufanya kampeni ya nguvu jimbo hilo litapata kura ya ndiyo viti hivyo. 
Alisema  wananchi hao endapo  watafanya hivyo ifikapo Oktoba 25, mwaka huu, watakuwa wamefanya kazi iliyokamilika na watapata maendeleo kwani amani inapatikana  mahali ambapo kuna maendeleo. 
Pia aliwataka wananchi hao kuhakikisha watunza kadi zao za kupigia kura, wasije wakapoteza nafasi hiyo muhimu. 
Mama Kikwete aliwataka wananchi hao, kukipa chama hicho kura ya ndiyo kwa sababu kina ilani, ni chama makini  na kinafanya kazi kwa mipango.
Akizungumzia kuhusu ilani ya chama hicho,Mama Kikwete alisema,ina mambo makubwa manne, ambayo ni kuondoa umasikini, kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira, kuendeleza vita ya kupambana na rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma.
Katika uzinduzi huo, Mama Kikwete alimkabidhi  vitendea kazi mgombea wa kiti cha Ubunge  ,ambavyo  ni Katiba ya CCM na ilani hiyo ili  aweze kufanya kazi  huku akishangiliwa na mamia ya watu walijitokeza uwanjani hapo wengi wao wakiwa ni vijana.
 
Kaisi na  waliokuwa wagombea wenzake wa kiti cha Ubunge 10 wameungana ili kumwuunga mkono Kaunje, hatua ambayo ilipongenzwa na Mama Kikwete.
“ Kura zipotosha huwezi kuhama kwenda chama kingine, bali mnaungana na kuwa kitu kimoja ni maneno mazuri ya kuiga mfano,” alisisitiza Mama Kikwete.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM, mkoa wa Lindi, Mzee Ally Mtopa aliwakemea watu wanaosema kuwa chama hicho hakijafanya  maendeleo, ambapo  alisema mtu anayesema  hivyo, sawa na kumdharau baba yake aliyempeleka shule.

No comments: