Saturday, July 4, 2015

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM MH. MECK SADICK AONGOZA ZOEZI LA KUOSHA MAGARI LA MEDIA CAR WASH FOR CANCER LEADERS CLUB LEO

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Meck Sadick akizindua zoezi la kuosha Magari katika viwanja vya Leaders Club kwa ajili ya kuchangia Fedha kwa waandishi wa Habari ambao wanamatatizo ya Kiafya ikiwemo Saratani .
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO),Nd.Assah Mwambene akikabidhi kiasi cha fedha kwa Mmoja wa Waratibu wa MEDIA CAR WASH FOR CANCER Bwa.Benjamin Kasenyenda,zilizochangwa na Idara hiyo kupitia chama chao cha Maofisa Habari wa Serikali ,walijitolea kuchanga kiasi cha shilingi Milioni 1,680,000=.Pichani kati anaeshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh.Paul Makonda

Kama vile haitoshi nayo Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na michezo pia walifanikisha kuchangia kiasi cha shilingi 1,350,000/= kufuatia kuguswa kwa namna moja nyingine kwa kampeni  hiyo adhimu ya kuwachangia waandishi wa Habari wenye Matatizo mbalimbali yakiwemo na ya Saratani.

Mbali ya fedha hizo kupatikana pia walijitokeza watu mbalimbali kuunga mkono kampeni hiyo ya MEDIA CAR WASH FOR CANCER,ambalo kwa kiasi kikubwa bado linahitaji kuongeza hamasa zaidi ili wadau wazidi kujitokeza na kuchangia.

Kampeni hiyo imefanyika leo katika viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar,ambapo viongozi mbalimbali wakiwemo na wadau wa habari walishiriki zoezi la kuosha magari kwa kuchangia kiasi chochote cha fedha,huku mgeni rasmi akiwa Mkuu wa Mkoa Dar Es Salaam Mh Meck  Sadick. 
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makonda akiendelea Kuosha moja ya Magari yaliyofika kuoshwa katika Media Car Wash for Cancer. Ikiwa ni kuchangia waandishi wa habari wenye magonjwa mbalimbali ikiwemo Saratani.

 Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe akiosha Gari wakati wa  Shughuli hiyo maalum kwa ajili ya Kuchangia waandishi wenye udhoofu wa afya zao.
Ankali Issa Michuzi wa Libeneke la Michuzi Blog na Michuzi Media Group na Mwana TBN  akiwa Bizeee... Anaosha Moja ya Magari kwa ajili ya kuchangie waandishi wa habari ambao wanamaradhi ya Saratani
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO,Assah Mwambene akizungumza jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh.Paul Makonda mara baada ya kushiriki zoezi zima la kuwachangia waandishi wa Habari wenye Matatizo mbalimbali yakiwemo na ya Saratani (MEDIA CAR WASH FOR CANCER).
 Picha ya pamoja ya waandishi wa Habari pamoja na Baadhi ya Viongozi 

Unaweza Changia pia kupitia M-Pesa 0766 970240
au Tigo Pesa 0653 155 808.

Picha ya pamoja ya waandishi wa Habari pamoja na Baadhi ya Viongozi 

Unaweza Changia pia kupitia M-Pesa 0766 970240
au
Tigo Pesa 0653 155 808

(Picha zote na Fredy Tony Njeje wa Blogs za Mikoa.)

 Mkuu wa Wilaya ya Kinomdoni Paul Makonda akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kuongea na Waandishi wa Habari pamoja na wadau 
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Meck Sadick akiongea na waandishi wa Habari pamoja na Wadau mbalimbali waliofika kuosha Magari yao kwa ajili ya kuwachangia waandishi wa Habari wenye Matatizo ya Saratani
 Wakielekea kuosha Magari
Mkurugenzi Mkuu wa Habari Maelezo(wa kwanza kushoto)  Athur Mwambene Akiosha Gari
Mzee wa Father Kidevu Blog  Ambaye pia ni mwana TBN  akiendelea na yake....
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makonda akiosha Pikipiki wakati wa shughuli hiyo
 Watu wanazidi kuchangia .....
Hapa ni zaidi ya Tsh 1,600,000 zimechangishwa na kukabidhiwa 
Chezea Changizo wewe
 Waandishi wakichukua kwa Makini Tukio zima

No comments: