Tuesday, May 26, 2015

MICHEZO YA MAJESHI YA FUNGULIWA RASMI LEO KATIKA UWANJA WA MAJI MAJI SONGEA MKOANI RUVUMA

Vikosi mbali mbali ya Majeshi vikiwa vimejipanga tayari kwa kungia uwanjani kwa ajili ya ufunguzi wa michezo ya majeshi 2015.
 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni mkuu wa Wilaya ya Songea Prof. Nomarn Sigalla King akisalimiana na wachezaji wa timu ya jeshi kutoka Mtwara.
.........................................
Na Amon Mtega ,SONGEA
MICHEZO ya majeshi inayoshirikisha vikosi mbalimbali vya ulinzi na usalama briged ya kanda ya kusini imefunguliwa rasmi na kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Songea ,Pr Noman sigaa King huku benki ya NMB tawi la Songea likiwa limetoa msaada wa jezi za mpira wa miguu seti saba ambazo zenye thamani ya shilingi 3,000,000.
Akiongea kwenye ufunguzi  huo  uliyofanyika leo katika uwanja wa michezo wa majimaji uliyopo Songea ,Sigara alisema kuwa  michezo hiyo itaimarisha mahusiano ya kiulinzi baina ya mipaka yetu ya Tanzania kwa kuwa vyombo vyote vya ulinzi na usalama vitakuwa na ushirikiano.
Alisema kuwa ulinzi wa Tanzania katika mipaka yetu  hautegemei jeshi moja tuu bali ni ushirikiano wa vikosi vya majeshi mbalimbali kama vikosi hivi ambavyo vimeshirikishwa kwenye michezo hii iliyozinduliwa na ambayo itarajiwa kufanyika kwa wiki mbili.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Prof. Norman Sigalla King akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya The Might Elephant .

Aidha Pr, Noman alizitaka taasisi za kifedha zilizopo hapa nchini kuwamstari wa mbele katika kudumisha mahusiano ya mambo mbalimbali ikiwemo ya michezo kwa kuwatoa misaada kama ilivyo kwa benki ya NMB.

“Taasisi za kifedha zinauwezo mkubwa wa kutoa misaada ya ushirikiano kwa kuwa zimekuwa na frunsa nyingi katika kufanikisha  mahitaji yanayotakiwa na wahitaji “alisema Noman Sigara ambaye ni kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma.

 Kwa upande wake kamanda Briged ya Tembo kanda ya kusini John Chacha awali kabla ya uzinduzi huo alisema kuwa licha ya kufanyika kwa michezo ya mpira wa miguu pamoja na mpira wa pete na wa kikapu toka kwenye vikosi mbalimbali vinavyoshiriki alisema kuwa kutakuwemo na mchezo wa kulenga shabaha ambao alidai kuwa ni mhimu kwa upande wa jeshi hilo.

Chacha alisema kuwa mchezo wa ulengaji shabaa ni mchezo mhimu sana kwa jeshi kwa kuwa ndio unaomfanya mwanajeshi kuwa tayari mda wote katika utendaji wao wa kazi ambao huendana na shughuli hizo.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Prof. Norman Sigalla King akionyesha ufundi wake wa kumiliki mpira katika ufunguzi wa michezo ya majeshi.



 Kwa upande wake meneja wa benki ya NMB tawi la Songea Rehema  Nasib akikabidhi msaada huo wa jezi alisema kuwa benki hiyo imejijengea utaratibu wa kuungana na jamii katika kutekeleza mambo mbalimbali ambayo yanayo hitajika.

 Rehema alisema kuwa licha ya benki hiyo kujijengea tabia hiyo lakini bado imekuwa ikithamini michango inoayotolewa na jamii pamoja na jeshi kwa kuwa wamekuwa wateja wakubwa ndani ya benki hiyo.
Katika michezo hiyo zaida ya vikosi tisa vinashiriki michezo hiyo na tayari imeshaanza kuchezwa katika uwanja wa maji maji.
  

 Baadhi ya washiriki wakifatilia mchezo
 Katoka kulia kwako wa pili ni Katibu wa SUFA  akifatilia mashindano ya majeshi na wa kwanza kulia kwako ni mtangazaji wa Jogoo FM Bw. Onesmo Emilani.




No comments: