Thursday, January 29, 2015

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje amwakilisha Rais Kikwete kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa NEPAD

Meza Kuu wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa NEPAD uliofanyika leo jijini Addis Ababa. Wakuu wa Nchi pamoja na mambo mengine walisomewa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya NEPAD kwa kipindi cha mwaka 2014. Kubwa lilihusu uanzishwaji wa Mpango wa Kilimo unaozingatia mabadiliko ya tabianchi ambao unawalenga wakulima wadogo zaidi ya milioni 25 watakaokuwa wanalima kwa kutumia teknolojia isiyokuwa na athari katika tabianchi ifikapo mwaka 2025.
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini naye alishiriki mkutano huo
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb) alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete katika Mkutano huo
Anayefurahia jambo ni Bibi Zulekha Tambwe, Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na nyuma yake ni Bw. Adam Issara, Katibu wa Naibu Waziri.

No comments: