Wednesday, April 30, 2014

Misokoto ya bangi 2,676 yakamatwa Manyara; watuhumiwa waendelea kupeta mtaani!

 JESHI la Polisi hapa nchini, limeshindwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wa madawa ya kulevya katika mkoa wa Manyara, ambapo kwa sasa Polisi wamekamata misokoto ya bangi 2,676 na mirungi bunda 70 katika mkoa huo, huku likishindwa kakabiliana na hali hiyo kutokana na Askari wake kushiriki vitendo hivyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Bangi1
Aidha kumbukumbu zinaonyesha kuwa katika kipindi cha Machi, mwaka 2012, Jeshi hilo mkoani Kilimanjaro lilimshikilia Askari wake (G 842, Konstebo Deogratius), ambaye alikamatwa na misokoto mine ya bangi akiwa katika ukumbi wa disko wa Albeto uliopo mjijni Moshi, huku akifanya vurugu katika ukumbi huo ambapo pamoja na Jeshi la Polisi mkoani humo kuthibitisha tukio hilo, mtuhumiwa huyo akisukwa rumande pamoja na Askari mwingine ambaye aliingia katika ukumbi huo akiwa na bunduki aina ya SMG na kufanyia watu fujo.

Mbali na matukio hayo Jeshi hilo, lilitoa taarifa ya kukamata kwa watuhumiwa 45 wakihusishwa na matukio ya utumiaji wa bangi, mirungi na gongo katika msako wa kuimarisha doria katika maeneo mbalimbali mkoani humo, msako ambao hadi leo Polisi mkoani humo wameshindwa kuwafikisha makahamani watuhumiwa wakidai bado uchunguzi haujakamilika Globu ya Jamii imebaini.

bangi watuhumiwa

Misokoto 2,676 ya bangi yakamatwa


Kamanda wa Polisi mkoani humo, Deusdedit Nsimeki, amemwambia Mwandishi wetu kuwa Aprili 15 saa 11:30 asubuhi katika eneo la Minjingu barabara ya Arusha-Babati, walimkamata, Nassoro Idd (27) mburege mkazi wa Singida mjini akiwa na misikoto ya bangi 2000 akiwa anatumia usafiriwa basi la kampuni ya Mtei lenye namba T.449 CAL, lililokuwa likitokea Arusha kwenda Singida.

Amesema siku hiyo hiyo huko minjingu Kata ya Nkaiti, Askari waliokuwa doria walimkamata, Juma Khatibu (18) Mshilazi na mkulima wa Arusha, akiwa na bangi misokatomo 620, iliyokuwa imehifadhiwa ndani ya mikate iliyokuwa imetobolewa, ambapo mtuhumiwa alikuwa ni abiria wa basi la kampuni ya Kandahar lenye namba T. 391 BUR lililokuwa likitokea Moshi kwenda mkoani Singida.

Bangi msokoto
Aidha Nsimeki, alisema katika Kata ya Nkaiti, wilayani Babati, Riziki Ferisi (18) Mchaga na mkulima wa moshi alikutwa na bangi misokoto 56 akiwa kwenye basi la Mtei lenye namba T.991 ABC, lililokuwa likitokea Moshi kwenda Singida, ambapo Aprili 13 maeneo ya magugu, Edward Mollel (27), Janeth Mollel (27 na Mudi Robert (33) kwa pamoja walikuwa wanasafirisha madawa ya kulevya aina ya Mirungi bunda 70 yaliyokuwa kwenye gari aina ya Noah yenye namba T.339 BYE, inayomilikiwa na Edward Mollel, mkazi wa Singida.

“Pamoja na kuwa kuna mbinu mpya zinatumika kusafirisha madawa haya, ikiwemo kuweka kwenye siti za magari kama Noah,’Tyubu’ za matairi ya magari, mifuko mbalimbali na mabegi, na kuweka ndani ya mikate iliyotobolewa lakini bado tumegundua mbinu hizo” alisema Nsimeki.

Ameiambia FikraPevu kuwa, Jeshi hilo limejizatiti kwa kuhakikisha kuwa hakuna makosa ya uhalifu, yatakayovunja amani katika maeneo yote ya mkoa huo katika kipindi hiki cha sikukuu za Pasaka.

Walimiki wa mabasi kukumbana na mkono wa sheria

Sanjari na watuhumiwa hao kukamatwa,Jeshi hilo limesema litachukua hatua kwa wamiliki wa mabasi, ambayo yatapatikana na madawa hayo yakiwemo yaliyokamatwa katika zoezi hilo, huku akitoa wito kwa wananchi wa mkoa huo kutoa ushirikiano wa dhati kwa Jeshi hilo, ili kuwabaini watuhumiwa mablimbali.

Tuesday, April 29, 2014

Wanamichezo 45 waagwa rasmi kwa ajili ya kwenda nje kufanya maandalizi ya mashindano ya Jumuiya ya Madola

Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe akizungumza na wanamichezo wanaoenda kuweka kambi katika nchi za New Zealand, Ethiopia, China na Uturuki ikiwa ni maandalizi ya mashindano ya Jumuiya ya Madola mapema mwezi julai. Kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Leornard Thadeo.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Leornard Thadeo akifafanua jambo wakati wa hafla ya kuwakabidhi bendera wanamichezo wanaokwenda nje ya nchi kwa ajili ya maandalizi ya mashindano ya Jumuiya ya Madola leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya njeya nchi na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe (wa tatu kutoka kushoto) akifurahia mara baada ya kuwa kabidhi Bendera ya Taifa wawakilishi wa wanamichezo wanaokwenda nchini New Zealand, Ethiopia,China na Uturuki kwa ajili ya kujiandaa na msahindano ya Jumuiya ya Madola. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Masuala ya Asia, Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Leornard Thadeo, Katibu wa Kamati ya Olympic Tanzania Filbert Bayi na mwakilishi wa wana michezo Neema Mwaisyula.
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania Anthony Mtaka akitoa neon la shukrani kwa niaba ya wanamichezo wote wanaoshiriki maandalizi hayo.
Baadhi ya wanamichezo na viongozi wao wakifuatilia kwa karibu hotuba ya Waziri wa mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kuwakabidhi Bendera ya Taifa leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Tanzania Leornard Thadeo akipeana mkono na mwakilishi wa wana michezo wanaoenda nje ya nchi kwa ajili ya maandalizi ya mashindano ya Jumuiya ya Madola mara baada ya kukabidhiwa Bendera ya Taifa na Waziri wa wa Mambo ya nje ya nchi na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe (mwenye shati la njano)
Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe akiwa na mchezaji wa timu ya Taifa ya kuogelea Hilal Hemed Hilal. PICHA ZOTE NA FRANK SHIJA

Tanzania Set to Test New Anti-Malaria Drug

BY ABDUEL ELINAZA, 29 APRIL 2014  ALLAFRICA.COM

Guangzhou — TANZANIA could be headed to a malaria-free country, thanks to Chinese medical research findings that target the disease-causing parasite itself instead of the mosquitoes which carry it. The current approach to deal with malaria is to control mosquitoes, which spread the disease by either killing them with insecticides or by draining bodies of stagnant water in which their larvae live.

However, Dr Li Guoqiao of the Guangzhou University of Chinese Medicine has developed a drug therapy based on artemisinin which attacks the malaria parasite to eradicate the disease.

According to General Manager, Mr Pan Longhua of Artepharm Company which manufactures the drug, after successfully eradicating malaria in the Comoros, a similar project was designed to be extended to Tanzania and talks to that end had reached an encouraging stage.

"I was in Tanzania two months ago where I met with the minister for health. We exchanged ideas and the prospects are good," Mr Pan told the 'Daily News.' "We are still exchanging ideas and other stakeholders are very supportive. Once everything has been agreed the pilot project will take off later this year," he added.

The firm's delegation when in Tanzania, also held talks with the National Malaria Control Programme, according to the GM. "The talks and data collection will take some more time, but we are hopeful that a project similar to one we undertook in the Comoros will be introduced in Tanzania before this year ends," the general manager said.

He said since Tanzania had certified the medicine in 2009, there was no problem in implementing the project in the country. WHO, he said, was yet to certify the drug, claiming it needed more findings especially on its side-effects.

The firm's approach is dubbed "Fast Elimination of Malaria through Source Eradication or FEMSE."

Two drugs, artemisinin and a second antimalarial called piperaquine, are the major ingredients in the combination made and sold under the brand name Artequick by Artepharm, a firm based in Guangdong Province, which Dr Li helped found.

To deny the parasites in their human hosts enough time to exterminate them, the researchers administer three doses of Artequick, spaced a month apart. To add extra power, the first dose is accompanied by a third drug, primaquine.

The drug, after several clinical tests in South East Asian countries, the tests were extended to Moheli, one of the three islands comprising the Comoros in 2007.

The number of malaria cases there subsequently fell by 95 per cent, though reinfection from other islands caused a small rebound. In 2012 the same tests were carried out in Anjouan where the number of malaria cases fell by 97 per cent. In October 2013 the campaign moved to Grande Comore, the most populous island.

When the process comes to completion there nearly all of the 700,000 Comorans will have taken part in FEMSE. The World Health Organisation (WHO) is critical of the experiment's approach for not also focusing on the drug's side-effects in the Comoro archipelago.

Guangzhou University of Chinese Medicine's Dr Qiaobo Ye does not, however, believe the side-effects will be a problem because the dose use is so low.

"We have not noticed evidence of any side-effects so far," he said. Nevertheless, the drug may cause nausea, fever, stomach and back pain, headaches and chills, which, according to researchers, are normal symptoms of red-blood cell rupture and some are also the common side-effects of artemisinin.

The malaria parasite infects only people from female anopheles mosquitoes which transmit the disease. If a population is simultaneously treated using the Chinese drug and the treatment is repeated about 40 days later, the parasite would be cleared from their blood for an extended period, because mosquitoes have a life span of 30 days.

Artemisinin has been in use in China for more than two decades but was more widely from 2001, when the WHO recommended its use in countries where resistance to malaria was undermining the effectiveness of other drugs.

The Minister for Health and Social Welfare, Dr Seif Suleiman Rashid, said recently that the country had during the past five years (2008-2013) witnessed a reduction in malaria transmission by 50 per cent, from 18 per cent in the financial year 2007/8 to nine per cent in 2011/12.

Vodacom yawaunganisha Buhigwe kwenye mtandao wa simu za mkononi

Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Charles Gishuli akiuzindua rasmi mnara wa Vodacom kuashiria kuanza kupatikana huduma za kampuni hiyo ya simu nchini katika kijiji cha Bukuba kilichopo Buhigwe mkoani Kigoma. Pembeni yake ni Meneja wa Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim. Wengine ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo Malcelina Mbehoma na Mwenyekiti wa Halmashauri Abel Kabona. Vodacom inaendeleza mkakati wake wa kuwaunganisha watanzania wa vijijini na huduma za mawasiliano ya simu za mkononi ili kuwawezesha kuboresha maisha yao.
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma Charles Gishuli (mwenye koti) akitumia simu yake ya mkononi kutuma fedha kupitia huduma ya M-pesa mara tu baada ya kuzindua huduma za Vodacom katika kijiji cha Bukuba mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Abel Kabona. Vodacom inaendeleza mkakati wake wa kuwaunganisha watanzania wa vijijini na huduma za mawasiliano ya simu za mkononi ili kuwawezesha kuboresha maisha yao.
Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim akimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Charles Gishuli jinsi ambavyo wakazi wa kijiji cha Bukuba Mkoani Kigoma wanavyoweza kupata huduma za Intaneti kupitia mtandao wa Vodacom mara baada ya Mkuu huyo wa Wilaya kuzindua rasmi huduma za Vodacom kijijini hapo mwishoni mwa wiki. Kushoto (mwenye kofia nyekundu) ni Mhandisi wa Vodacom Mkoa wa Kigoma Adam Nyamgali.
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Charles Gishuli akiongea na wakazi wa kijiji cha Bukuba na vijiji jirani waliofika kushuhudia uzinduzi wa mnara wa mtandao wa Vodacom kijijini hapo mwishoni mwa wiki. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim. Wengine kutoka kuhsoto ni Mhandisi wa Vodacom Adam Nyamgali, Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya Renatus Mkasa na Kaimu Mkurgenzi Mtendaji wa Wilaya Malcelina Mbehoma. Kupatikana kwa huduma za Vodacom kijijini hapo kunatarajiwa kufungua ukurusa mpya wa maendeleo ya kiuchumi an kijamii kijijini hapo.
Mhandisi wa Vodacom Mkoani Kigoma Adam Nyamgali akimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma jenereta inayozalisha umeme wa kuendeshea mnara wa mawasiliano wa kampuni hiyo. Mkuu huyo wa Wiayaa aliuzindua mnara huo uliopo kijiji cha Bukuba mwishoni mwa wiki. Vodacom inaendeleza mkakati wake wa kuwaunganisha watanzania wa vijijini na huduma za mawasiliano ya simu za mkononi ili kuwawezesha kuboresha maisha yao.

Zaidi ya wakazi 17,000 wa kijiji cha Bukuba wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma kunufaika na huduma za mawasiliano ya simu za mkononi za mtandao wa Vodacom baada ya kampuni hiyo kuzindua rasmi huduma zake kijijini hapo.

KIuzinduliwa kwa huduma za Vodacom kijijini hapo kunawapa nafais wakazi hao walio pembezoni mwa wilaya mpya ya Buhigwe kuwa na uwezo na fursa ya kuboresha maisha yao kupitia simu za mkononi ikiwemo kuboresha usalama, kurahisisha biashara n.k.

Huduma hizo zimezinduliwa na Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Charles Gishuli kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya .

Akziundua huduma hizo mwishoni mwa wiki, Mkuu wa Wilaya Gishuli ameelezea matumaini yake ya namna ambavyo maisha ya wakazi hao yanavyoweza kuboreka ikiwemo suala la ulinzi, wepesi na tija kwenye kilimo,ufugaji na biashara.

Amesema jiografia ya kijiji hicho na Wilaya ya Buhigwe kwa ujumla inatoa ulazima wa kuwa na mawasiliano ya uhakika ili kuweza kuistawisha shughuli za kiuchumi hususan biashara ambazo ndio nguzo kuu ya maisha ya wakazi wa hapo.

Amesema  Bukuba ina kiwango kikubwa cha biashara ikihusisha mazo ya ndizi na mifugo ambapo soko kuu ni mikoa ya Tabora, Katavi na nchi jirani ya Burundi.

“Leo ni siku njema kwenu wakazi wa Bukuba kupata huduma za Vodacom zitakazowawezesha kuwa na uhakika wa mawasiliano na kuboresha shughuli zenu z akiuchumi na kijamii tofauti na ilivyokuwa hapo awali .”

Natambua kuwa malori yenye mikungu ya ndizi inatoka hapa kwenda Tabora, Katavi, Rukwa na nchi jirani ya Burundi tumieni mawasilano kupata raatifa za kimasoko ikiwemo aina ya wateja, bei na kiwango cha mahitaji ili kupunguza adha ya kusafirisha mzigo kwa kubahatisha soko, kwa njia hiyo sasa mnayo kila sababu ya kufanya biashara kwa ufanisi na tija zaidi.”

Aidha, amesema ujio wa Vodacom unaombatana na huduma ya M-pesa utasaidia kwa kiwango kikubwa kupunguza changamoto zitokanazo na ukosefu wa huduma za kibenki kwenye kijiji hicho na eneo kubwa la wilaya hiyo mpya ya Buhgwe.

Amesema kupitia M-pesa ni wazi sasa benki zipo kwenye viganja vyao hivyo hawana sabbau ya kuwa na hofu ya kukosa huduma za kibenki kinachpaswa na kujifunza na kuitumia kwa ufasaha kwa maendeleo yao.

“Naamini mtatumia huduma ya M-pesa kuziba pengo la huduma za kibenki kwani kama tulivyoelezwa hapa kupitia M-pesa unaweza kuweka au kutoa fedha kutoka kwenye benki, hii ni nafasi yenu kuounguza gharama mlizokuwa mkiingia kufuata huduam za benki Wilayani Kasulu ama Kigoma Mjini.”

Amesema kwa wastanimakzi wa Bukuba anaekwenda mjini mara mbili au tatu kufuata huduma za benki humgharimua hadi Sh. 30,000 gharama ambayo kwa sasa wanaweza kuipeka na kutumia feha hizo katika shughuli nyengine.

Hata hivyo ametoa rai kwa Vodacom kushirikiana na benki zilzounganishwa na M-pesa kutoa elimu kwa wakazi hao ili waweze kunufaika vema hasa wafanyabaishara ambao wanalazimika kusafiri umbali mrefu na fedha.

Mkuu huyo wa Wilaya pia amezungumzia umuhimu wa Bukuba na Buhigwe kwa ujumla kuwa na huduam za uhakika za mawasiliano ili kuweza kukabiliana na changamoto za kiusalama hasa kutokana na kuwa mpakani.

“Wote tunajua changamoto za kiusalama ambazo maeneo yaliyo mipakani kama sisi yanavyokabiliana nayo, nawaomba tutumie mawasiliano haya ya simu ya mkononi kuongeza uimara wa usalama wetu na kwmaba sasa mnaweza hata kunipata kwa urahisi kutoa taarifa za viasharia vya matukio mabaya.”Aliongeza Mkuu huyo wa Wilaya

Gishuli akizungumzia umuhimu wa mawasiliano katika kuimarisha ulinzi na usalama, amesema ni jambo lililowazi kuwa uwepo wa mawasiliano ya uhakika kunaimarisha ulinzi hasa kwa wilaya kama ya Buhigwe iliyo mpakani.

Amesema mawasiliano ya uhakika yanaviwezesha vyombo vya ulinzi na usalama kupokea taarifa mbalimbali za uhalifu au viashiria vyake kutokana kwa wananchi au hata kubadilishana taarifa na wenao wa nchi jirani.

Amewataka wakazi hao kwa kuwa sasa wana uhakika wa mawasiliano kumpatia taarifa mara moja kupitia simu yake ambayo aliitaja hadharani huku akiiiomba pia Vodacom kuendelea kuimarisha huduma zake wilayani humo kwenye maeneo ambyo bado yana ukorofi.

Kwa upande wake Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim akizungumza kwenye uzinduzi huo alisema usimikwaji wa huduma za Vodacom kijijini hapo ni mwendelezo wa mpango mkakati wake wa kuhakikisha inawaunganisha watanzania wakiwemo wa vijijini kwenye mtadao wa huduma za mawasiliano ya simu za mkononi.

Amesema Vodacom itaendelea  kutilia mkazo mpango huo ikiwemo kwenye maeneo yaliyo pembezoni kama Bukuba kwa kuwa Vodacom inaamini kuwawezesha wananchi kimawasiliano ni kuwapa fursa ya kubadili maisha yao.

"Mhe.Mkuu wa Wilaya, kazi iliyofanywa na Vodacom hapa Bukuba inafanyika pia sehemu mbalimbali za nchi kwa shabaha ya kuwaunganisha watanzania kwenye mtandao wa simu za mkononi.”Alisema Mwalim

“Ni Imani yetu kwmaba sasa maisha ya wakazi wa Bukuba yatabadilika, baishar zitakua zaidi na shughuli za kilimo zitaimarika zaidi ya ilivyokuwa hapo awali, matokeo ya haya yote ni kuboreka kwa maisha ya wananchi, hilo ndio lengo la Vodacom.”Aliongeza Mwalim

Mwalim amesema katika maisha ya sasa huduma za mawsiliano ya simu za mkononi sio tena anasa, kila mmoja anapaswa kufikiwa na huduma hiyo na kwmaba Vodacom itaendelea kuwaunganisha watanzania mijini na vijijini.

“Hatuangalii mijini tu, walio vijijini nao ni sehemu muhimu ya mikakati yetu tukitambua nao wana nafasi kubwa ya kuboresha maisha yao iwapo tutawapatia huduma zetu, kwetu sisi kila mmoja tunampa umuhimu na uwepo wetu Bukuba leo ni matokeo ya kile tunachokiamini na kukitekeleza.”Alisema

Aidha Mwalim amewakumbusha kujiunga na vifurushi vya Vodacom ikiwemo cha cheka ambavyo vinalenga kuwapatia watejahuduma bora na kwa gharama nafuu.

SHEREHE ZA MIAKA 50 YA MUUNGANO ZAFANYIKA PARIS UFARANSA

Watanzania waishio nchini Ufaransa walikutana Jumamosi mchana tarehe 26 Aprili nyumbani kwa Balozi wa Tanzania mjini Paris ili kusherehekea miaka 50 ya muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika.
Balozi wa Tanzania Nchini Ufaranza,Mh. Begum Karim Taj akipokea keki maalum kwa ajili ya sherehe hizo za Muungano wa Tanzania katika hafla iliyofanyika nyumbani kwa Balozi,Mjini Paris Ufaransa.
Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa akiwa na watoto mjini Paris.
Mh. Balozi Begum Taj akiwa na baadhi ya watanzania waishio nchini Ufaranza.
Kutoka kushoto: Ndg John Kimaro (Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Kale), Mh Begum Taj (Balozi wa Tanzania) na Rainfrida Kapela (Mhifadhi Mkuu wa Mambokale Bagamoyo).
Mh Begum Karim Taj akiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Watanzania Ufaransa Mh Delly Makombe.
Ndugu Mohammed Sheya akiimba wimbo wa Taifa.
Mama Delly , Mh Balozi Tah na Mama Matari wakikata keki.
Burudani ya uhakika ikiendelea.
Ndg John Kimaro (katikati) akiongea na wageni wakati wa sherehe za Muungano
Mama Rainfrida Kapela Mhifadhi Mkuu wa Mambo ya Kale Bagamoyo
Vyakula mbalimbali katika kuenzi miaka 50 ya muungano.
Baadaye ikawa kazi ya kufungua 'champaign' kuenzi sherehe za Muungano.Picha na Mdau Simplish Lakshi.

MAMA SALMA KIKWETE AZINDUA WIKI YA CHANJO DUNIANI MKOANI KILIMANJARO

Baadhi ya taasisi a NGO'S mbalimbali zilihudhuria uzinduzi huo.
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za msingi wakisikiliza kwa makini mambo mbalimbali yaliyokuwa yakizungumzwa.
Makundi mbalimbali ya watu yalishiriki uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani iliyozinduliwa mjini Moshi.
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za msingi wakisikiliza kwa makini mambo mbalimbali yaliyokuwa yakizungumzwa.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akizungumza wakati wa uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani.
Mwakilishi  mkazi wa shirika la Afya Duniani (WHO) Dk Rufaro Chatora akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi.
Baadhi ya washiriki katika uzinduzi huo kutoka Asasi mbalimbali mkoani Kilimanjaro.
Mwakilishi wa UNICEF,Sudha Sharma akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi.
Naibu waziri wa Afya,Kebwe Stephen Kebwe akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi.
Mke wa rais Mama Salma Kikwete akiwasalimia wananchi waliofika katika sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi.
Mke wa rais Mama Salma Kikwete akitoa hotuba yake wakati wa sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi.
Mkurugenzi
huduma za Afya toka wizara ya Afya,Dk Neema Rusibamayile akitoa neno la shukrani mara baada ya Mke wa rais,Mama Salma Kikwete kutoa hotuba yake.
Mke wa rais ,Mama Salma Kikwete akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa wiki ya chanjo duniani.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa chanjo ya matone kwa mtoto Ahmad Saleh kuashiria uzinduzi rasmi wa wiki ya chanjo duniani.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.