Tuesday, September 2, 2014

MH. BENDERA AFUNGUA WARSHA YA SIKU MBILI YA WAANDISHI WA HABARI INAYOHUSU UMUHIMU WA UTOAJI TAARIFA ZA HALI YA HEWA KWA UMMA,MKOANI MOROGORO LEO


 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Mh. Joel Bendera akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa Warsha ya siku mbili ya Waandishi wa Habari ilinayoendeshwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini kuhusu umuhimu wa huduma za hali ya hewa,ushirikishwaji na usambazaji wa taarifa za hali ya hewa kwa umma,inayofanyika kwenye hoteli ya Oasis mjini Morogoro.Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini,Dkt. Agness Kijazi na kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini,Dkt. Hamza Kabelwa.
 Baadhi ya Waandishi wa Habari wanaoshiriki kwenye Warsha ya siku mbili ya Wanahabari inayoendeshwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini kuhusu umuhimu wa huduma za hali ya hewa,ushirikishwaji na usambazaji wa taarifa za hali ya hewa kwa umma wakisikiliza kwa makini hotuba ya ufunguzi wa warsha hiyo iliyokuwa ikisomwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Mh. Joel Bendera.
 Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini,Dkt. Hamza Kabelwa akizungumza machache wakati akitoa shukrani kwa mgeni rasmi na kwa washiriki wa warsha hiyo inayoendelea kufanyika hivi sasa kwenye ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Oasis,Mkoani Morogoro.
  Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini,Dkt. Hamza Kabelwa akizungumza jambo wakati akichangia moja ya mada zinazoendelea kuwasilishwa kwenye warsha hiyo inayoendelea hivi sasa kwenye ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Oasis,Mkoani Morogoro.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini,Dkt. Agness Kijazi akisisitiza jambo wakati akijubu moja ya maswali yaliyoulizwa na waandishi wa habari wanaoshiriki kwenye Warsha ya siku mbili ya Wanahabari inayoendeshwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini,inayohusu umuhimu wa huduma za hali ya hewa,ushirikishwaji na usambazaji wa taarifa za hali ya hewa kwa umma

Muwasilishaji wa Mada ya kwanza katika warsha hiyo,Bi. Mecklina Merchades akiwasilisha mada iliyohusu Utekelezaji wa programu ya utoaji huduma ya hali ya hewa duniani.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini,Dkt. Agness Kijazi na Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini,Dkt. Hamza Kabelwa wakisikiliza kwa makini uwasilishwaji wa mada mbali mbali zinazoendelea kuwasilishwa kwenye warsha hiyo.
 Baadhi ya Waandishi wa Habari wanaoshiriki kwenye Warsha ya siku mbili ya Wanahabari inayoendeshwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini kuhusu umuhimu wa huduma za hali ya hewa,ushirikishwaji na usambazaji wa taarifa za hali ya hewa kwa umma wakifatilia kwa makini mada zinazoendelea kutolewa kwenye warsha hiyo.
 Picha ya pamoja. 

No comments: