Saturday, August 23, 2014

MAMA SALMA KIKWETE AONGOZA SHUGHULI YA MAZISHI YA JAJI LEWIS MAKAME KIJIJINI KWAKE HUKO TONGWE - MUHEZA

 Mama Salma Kikwete akimfarijiMama Mary Mbaga Makame, mke wa Marehemu Jaji Lewis Mhina Makame mara baada ya kuwasili kijijini Tongwe, wilayani Muheza  kwa ajili ya mazishi leo
 Mama Salma Kikwete akimfarijiMama Mary Mbaga Makame, mke wa Marehemu Jaji Lewis Mhina Makame mara baada ya kuwasili kijijini Tongwe, wilayani Muheza  kwa ajili ya mazishi .leo
  Mama Salma Kikwete akiaga mwili wa Marehemu Jaji Lewis Makame kijijini kwake huko Tongwe, wilayani Muhez

 Mama Salma Kikwete akimpa pole Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva muda mfupi kabla ya kuanza ibada ya mazishi ya Marehemu Jaji Lewis Makame iliyofanyika katika Kanisa  Anglikana la Mtakatifu Yusuf huko Tongwe, wilayani Muheza.
 Mama Salma Kikwete akifuatana na Mama Mary Makame, mjane wa Marehemu Jaji Lewis Makame kuelekea kwenye ibada ya mazishi iliyofanyika katika kanisa Anglikana Tongwe huko Wilayani Muheza
 Mama Salma Kikwete akifuatana na Mama Mary Makame na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mheshimiwa Angela Kairuki (kwa kwanza kulia) wakielekea kanisani.
 Mama Salma Kikwete akiongozana na Mama Mary Makame wakiingia katika kanisa Anglikana  huko Tongwe kwa ajili ya ibada ya mazishi ya marehemu Jaji  Lewis Makame.
 Mwili wa Marehemu Jaji Lewis Makame ukiingizwa kanisani kwa ajili ya ibada.
  Sehemu ya waumini na watu mbalimbali waliohudhuria ibada ya mazishi ya Marehemu Jaji Lewis Makame huko kijijini kwake Tongwe wilayani Muheza.
 Mama Salma nKikwete akitoa neno la faraja kwa wafiwa mwishoni mwa ibada ya kumuombea marehemu Jaji Lewis Makame iliyofanyika katika kanisa Angilkana Tongwe huko Muheza.
 Mama Salma Kikwete akiongoza mamia ya waombolezaji kwenda makaburini kwa ajili ya mazishi.
 Jaji Mkuu Mheshimiwa Chande Othman alikuwa ni miongoni mwa majaji wa Mahakama Kuu na Rufaa waliobeba mwili wa Marehemu Jaji Lewis Makame kuupeleka kwenye nyumba yake ya milele huko kijijini kwake Tongwe katika wilaya ya Muheza.
 Askofu wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Tanga Dr. Williama Mndolwa akiwaongoza maaskofu, makasisi na mashemasi kuweka udongo kwenye kaburi la Marehemu Jaji Lewis Makame.
 Mama Salma Kikwete akimsindikiza Mjane wa Marehemu Jaji Lewis Makame, Mama Mary Makame kuweka udongo kwenye kaburi.
 Mama Salma Kikwete akiwa na  Mjane wa Marehemu Jaji Lewis Makame, Mama Mary Makame 
 Mama Salma Kikwete akitoa salamu ya pole kwa wafiwa mara baada ya shughuli ya utiaji udongo kaburini kukamilika.
 Mjane wa Marehemu Jaji Lewis Makame, Mama Mary akiweka shada la maua kwenye kaburi la mume wake Marehemu Jaji Lewis Makame wakati nwa ibada ya mazishi iliyofanyika huko Tongwe katika wilaya ya Muheza
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea shada la maua kutoka kwa msaidizi wake tayari kuliweka kwenye kaburi la marehemu Jaji Lewis Makame aliyezikwa kijijini kwake huko Tongwe.


Mama Salma Kikwete akiweka shada la maua kwenye kaburi la hayati Jaji Lewis Makame wakati wa mazishi yaliyofanyika katika kijiji cha Tongwe katika wilaya ya Muheza, mkoani Tanga tarehe 23.8.2014. 
PICHA NA JOHN  LUKUWI 

No comments: