Monday, April 29, 2013

Jaji Warioba: Tutatoa rasimu ya katiba yenye maslahi ya Taifa

Jaji Warioba - Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo (Jumatatu, Aprili 29, 2013). Kulia ni Katibu wa Tume, Bw. Assaa
Rashid. (Picha na Tume ya Katiba)

Na Mwandishi Wetu
 Tume ya Mabadiliko ya Katiba imesema imejipanga kuandaa rasimu ya katiba itakayoweka mbele maslahi ya taifa na kuwaomba wananchi waijadili na kutoa maoni yao katika mabaraza ya katiba yatakayokutana kuanzia mwezi Juni mwaka huu (2013).

Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Jospeh Warioba amesema leo (Jumatatu, Aprili 29, 2013) jijini Dar es Salaam kuwa katika kuandaa rasimu hiyo, Tume yake haitapokea shinikizo kutoka taasisi, asasi, makundi au vyama vya siasa.

“Tume haitengenezi katiba ya vikundi au vyama, tunaandaa katiba ya nchi,” amesema Jaji Warioba katika mkutano wake na waandishi wa habari katika ofisi za Tume na kufafanua kuwa Tume inazingatia uzito wa hoja zilizotolewa  na wananchi na sio idadi ya watu waliotoa maoni.

Jaji Warioba amewataka wananchi kutokubali kutumiwa na makundi, asasi, taasisi na vyama wakati wa kujadili na kutoa maoni katika mabaraza ya katiba ya wilaya.

Mabaraza ya Wananchi wenye ulemavu
Akizungumza kuhusu ushiriki wa walemavu katika mabaraza ya katiba, Jaji Warioba amesema Tume yake inatarajia kuunda mabaraza ya Katiba ya watu wenye ulemavu ili kuwapa fursa walemavu kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kutoa maoni yao kuhusu rasimu ya Katiba itakayotolewa na Tume.

Hatua hii inafuatia ombi la Shirikisho la Vyama vya Watu wenye ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) na Umoja wa Watu wenye ulemavu Zanzibar (UWAZA) waliloliwasilisha kwa Tume.

Jaji Warioba amesema Baraza moja litaundwa Tanzania Bara na jingine Zanzibar na kwamba yatashirikisha wananchi kutoka ngazi ya chini ya wilaya hadi Taifa.

“Tunaelewa kuwa watu wenye ulemavu ni karibu asilimia 10 ya watanzania wote na mchakato huu hauwezi kuwatenga katika ngazi yoyote,” amesema Jaji Warioba na kuongeza kuwa taarifa ambazo Tume yake inazo zinaonyesha baadhi ya watu wenye ulemavu wamependekezwa na mitaa, vijiji, vitongoji na shehia kuwa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya.

                                                   Chaguzi za Wajumbe Mabaraza ya Katiba ya Wilaya.
Aidha, Jaji Warioba amezungumzia mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika chaguzi zilizofanyika nchini kote hivi karibuni za kuchagua Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba kuanzia ngazi ya mitaa, vijiji, vitongoji na shehia.

Kwa mujibu wa Jaji Warioba, tathmini ya Tume inaonyesha kuwa kwa kiwango kikubwa viongozi na watendaji katika ngazi za vijiji, mitaa, shehia na kata walizingatia mwongozo uliotolewa na Tume na kuwa maeneo mengi wananchi walichaguana kwa amani na utulivu.

“Kwa mfano jumla ya shehia 323 sawa na asilimia 96.4 kati ya shehia 335 kwa upande wa Zanzibar zimekamilisha vizuri mchakato huu, hali kadhalika jumla ya Kata 3,331 sawa na asilimia 99.8 kati ya Kata 3,339 kwa Tanzania Bara nazo zimekamilisha mchakato wa kuwapata wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya kwa kuzingatia utaratibu uliotolewa kwa mujibu wa Mwongozo,” amesema Jaji Warioba.

Kuhusu hatua inayofuata baada ya chaguzi hizo, Jaji Warioba alisema Tume inaendela kupokea majina kutoka kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa na ya wananchi wote waliopendekezwa kutoka katika Kata na Shehia na kazi hiyo inatarajia kukamilika ifikapo tarehe 30 Aprili mwaka huu (2013).

Changamoto
Akizungumzia kuhusu changamoto zilizojitokeza katika chaguzi hizo, Jaji Warioba amesema kuwa pamoja na mafanikio yaliyopatikana pia kulijitokeza changamoto kadhaa ambazo zilisabishwa na misimamo ya kisiasa na kidini

“Katika baadhi ya maeneo mikutano ya uchaguzi ngazi za vijiji, mitaa na shehia ilishindwa kufanyika kutokana na mivutano ya kisiasa na kidini zilizosababishwa na baadhi ya wananchi kufangamanisha chaguzi za Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya na masuala ya kisiasa na kidini,” amesema Jaji Warioba.

Jaji Warioba ametaja changamoto nyingine kuwa ni pamoja na baadhi ya wananchi kujiingiza katika vitendo vya rushwa katika chaguzi hizo ili wapendekezwe kuwa wajumbe wa mabaraza hayo ya katiba.

“Tumepokea pia malalamiko ya vitendo vya rushwa,” alisema Mwenyekiti huyo na kusema vitendo hivyo ni kinyume cha sheria na kuongeza kuwa taasisi zenye mamlaka ya kupambana na vitendo hivyo zinapaswa kushughulikia malalamiko hayo.

                                                                           Aina na Majukumu ya Mabaraza ya Katiba
Katika mkutano huo uliofanyika katika katika Ofisi za Tume zilizopo mtaa wa Ohio jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti huyo pia alizungumza kuhusu aina na majukumu ya Mabaraza ya Katiba.

Kwa mujibu wa Jaji Warioba, Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 imetoa fursa ya kuundwa kwa mabaraza ya aina mbili ambayo ni Mabaraza yatakayoundwa, kusimamiwa na kuendeshwa na Tume katika muda na tarehe itakayopangwa na Tume.

Aina ya pili, kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo, ni Mabaraza ya Katiba ya Asasi, Taasisi na Makundi mbalimbali yenye malengo yanayofanana. Mabaraza haya yatajiunda, yatajisimamia na kujiendesha yenyewe na kisha kuwasilisha maoni yao kuhusu rasimu ya Katiba ndani ya muda utakaopangwa na Tume.

“Kazi kubwa ya Mabaraza ya Katiba ya aina zote mbili ni kuipitia, kuijadili na kuitolea maoni rasimu ya Katiba itakayokuwa imeandaliwa na Tume kutokana na maoni yaliyokusanywa kutoka kwa wananchi,” alisema Jaji Warioba na kuziomba taasisi, makundi, asasi na vyama mbalimbali kutumia fursa hiyo ya kisheria kuunda mabaraza na kutoa maoni yao kuhusu rasimu ya Katiba itakayotolewa.

FOWARD MOTION ikishirikiana na Doctor's Plaza Heart Clinic pamoja na Lancet Laboratories yazindua kampeni ya kupima afya

 Mapokezi  Doctor's Plaza Heart Clinic
 wadau wakisubiri kupimwa afya zao  Doctor's Plaza Heart Clinic
  Wadau wakijisajili
  Doctor's Plaza Heart Clinic ilihudumia wadau kibao siku hii

 Wafanyakazi wa  Doctor's Plaza Heart Clinic wakijadiliana namna ya kuendesha kazi siku hii
  Mama akijiandikisha Doctor's Plaza Heart Clinic
 Kumbukumbu zinawekwa kwa uangalifu



















GLOBAL 2013 SMART PARTNERSHIP DIALOGUE TO BE HELD IN DAR ES SALAAM FROM 28TH MAY – 1ST JUNE , 2013.


INTRODUCTION
Smart Partnership dialogue is a national and international consultative forum where governments engage with all sectors of the society (called partners) to share information, knowledge and expertise smartly in finding solutions to development challenges. These sectors otherwise called ‘partners’ could be political leaders, civil servants, entrepreneurs, corporate leaders, management, or people in general who plays different roles according to their different clusters in a society, but all operates from the same set of principles in dealing with challenges.
Therefore, the concept Smart Partnership Dialogue (SPD) drives from a unique manner in which stakeholders/partners engage in a dialogue/consultation to solve their challenges - mostly technological – smartly, hence the name Smart Partnership Dialogue.

Smart Partnership Dialogue (SPD) is a brainchild of Commonwealth Partnership for Technology Management (CPTM) which is a social and scientific inters – linkages arm of the Commonwealth, and has since undertaken in collaboration with willing national partners to provide a forum for the discussion of topical subjects in a conducive and inclusive open dialogue. These dialogues can be traced back to 1990s when the first dialogue was held in Malaysia in 1995 under the leadership of the Prime Minister Dr. Mahathir Mohammed.

The vision of SPD is to promote creative cooperation between the government and other sectors contributing to social economic activities. To date, twenty Smart Partnership International Dialogues has been held in different Commonwealth member States countries with different key themes. The last one was held in 2011 Putrajava, Malaysia. It was at this meeting that His Excellency President Jakaya Mrisho Kikwete made a decision to host the next SPD.

GLOBAL 2013 SMART PARTNERSHIP DIALOGUE
Tanzania will host the next Smart Partnership Dialogue. The Host and Patron Advisor for the 2013 Smart Partnership Dialogue, His Excellency Jakaya Mrisho Kikwete, and President of the United Republic of Tanzania officially launched preparations for the 2013 Dialogue in 29th May, 2012. He also introduced the theme of Global 2013 SPD as Leveraging Technology for Africa’s Socio – economic Development and announced the dates for the dialogue to be 28th June - 1st July, 2013 to be held at Julius Nyerere Convention Center, Dar es Salaam.
The decision of His Excellency President Jakaya Kikwete to host the Global 2013 SPD and the choice of the theme for the dialogue were anchored on the realization and conviction that these dialogues provide a unique forum for interaction and equal opportunities for all participants.

WHY TANZANIA IS HOSTING GLOBAL 2913 SPD
Tanzania as a Commonwealth member state is one of the nineteen African countries who are also partners of SPD and has participated in several SPD hosted by other countries. One of our greatest challenges as a developing country striving to pull itself out of poverty and bring development to its people is the inadequate access to appropriate technology. This missing link seems to be otherwise inherent to our national efforts to translate our abundant natural and human resources in to tangible development gains. The Dialogue therefore, is about identifying various forces to stimulate change, spearhead the process and mastermind the change and transformation of the Tanzanian society. Specifically, Global 2013 SPD is intended to achieve the following:
§  Establish sustainable technology links both domestic and foreign.
§  Identify, develop and support youth technological innovation talents
§  Share experiences from different stakeholders and jointly work out the solutions in a participatory manner.
§  Create an inclusive society and promote partnership based on the principle of win – win situation
§  Inspire the development of a roadmap for technological development targeting sector by sector enhancement in the country in hand with the National Vision 2025


NATIONAL PREPARATORY STRUCTURES FOR GLOBAL 2013 SPD
The national preparatory structures consist of three main layers. The first layer is that of the President of the United Republic of Tanzania who is the Patron and Host of the Dialogue. Therefore, the Global 2013 SPD in Tanzania will be hosted under the auspices of His Excellency Jakaya Mrisho kikwete. 

The second layer consists of National Organizing Committee. The Chief Secretary Ambassador Ombeni Sefue – President’s Office - has been appointed by the President of United Republic of Tanzania as Co - Convener of the Dialogue and Head of The National Organizing committee (NOC). Other members of this committee include Permanent Secretaries from some key line ministries, Executive Secretary from Planning Commission, and Chief Executive from Strategic Institutions. The National Organizing Committee has the duty of providing overall guidance of the successful execution of the Global 2013 SPD.
The third layer consists of The Dialogue Resource Team. This group is called The Think Tank.
The Dialogue Resource team is made up of the National and International dialogue resource teams. The National Core Resource Group comprises of experts from the following sectors: Agribusiness, Education, Youth, Social Issues, Energy, Extractive Industries, Health, Manufacturing Industries, Science and Technology, Research & Development, Transportation, Environment, Arts and Culture, Labor, Central Banks and Financial Institutions.
The National Resource Group will interact closely with the International Resource Team on issues of Technology for Socio-economic transformation.
The Dialogue Resource team is expected to influence the agenda and the team will give advice based on their experiences and knowledge to the Host Patron, the Council of Patrons and Advisers and CPTM Fellows on socio-economic transformation programmes and how best appropriate technology can be utilized to bring about sustainable development to the nation and other participating countries.
During the dialogue the Dialogue Resource Team will moderate/participate in discussion on the main theme and the sub themes agreed upon. The Dialogue Resource team through discussion will propel on how best to promote technology in the whole process of transformation for socio economic growth for sustainable development in the local and international context.
This Dialogue also has links known as the Smart Partnership Links whose participants will be categorized according to their interest.  Smart Partnership Links have been formed to feed into the main theme Leveraging Technology in the following areas: Business, Professional and Academia, Youth, otherwise called Smart 29ners, Media, Labor and Civil Service, Social Issues, Community and Tradition, Arts and Culture.

The fourth layer is the Secretariat. It operates under the supervision of Chief Secretary and Co – Convener of Global 2013 SPD. The Secretariat is in charge of the daily preparations and executions of the decisions made by NOC. It also provides the link between the CPTM hub in London, key government sectors, private sectors drawn locally and internationally. It also works with support structures that are considered to be essential for successful carrying out the dialogue.

REVERSE MEDIA DIALOGUE
One of the key features of this year SPD is that at some point in the process of the dialogue, media representatives will engage in a discussion/dialogue with the Joint Executive council of Conveners. During these sessions journalists are expected to share their views on how they position themselves in helping realize the objectives of The Global 2013 SPD.

PARTICIPATION IN THE DIALOGUE
Participation to the dialogue is open to anybody interested in the theme of this year. All one needs to do is to fill the registration form and pay the registration fee of 300,000/=. The registration forms are available at our website whose address is www.globaldialogue2013.go.tz
  
CONTACT DETAILS
For any inquiries, the Contact Details of the Secretariat are hereunder:
Tel: +255 – 22- 2121459/2111906
Fax: +255 – 22 – 2121447/2116600


CRDB YAKABIDHI JENGO LA WODI YA WATOTO HOSPITALI YA MKOA WA MOROGORO

 Jengo la Wodi ya Watoto katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro ikionekana ikiwa katika hali nzuri baada ya kufanyiwa ukarabati na Benki ya CRDB na kugharimu kiasi cha sh. milioni 50.
 Meya wa Manispaa ya Morogoro Amir Nondo (kushoto) akifurahjia jambo na Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja, Tully Mwambapa (kati) na Mkurugenzi wa benki ya CRDB tawi la Morogoro, Pendo Assey. 
Wafanyakazi wa benki ya CRDB wakiwa wameshika miche ya miti tayari kwa kuanza zoezi la upandaji miti kuzunguka katika maeneo ya hospitali ya Mkoa wa Morogoro. 
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid akipanda mti wa kumbukumbu baada ya uongozi wa benki ya CRDB kukabidhi jengo la wodi ya watoto katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro lililofanyiwa ukarabati pamoja na kuwekewa vifaa muhimu katika wodi hiyo. Jumla ya Sh. Milioni 50 zimetumika katika ukarabati huo. 

Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB Dk. Charles Kimei akipanda mti wa kumbukumbu wakati wa hafla ya kukabidhi wodi ya watoto katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.


 Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid (katikati), akishiriki kufanya usafi katika jengo la wodi ya watoto katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro ambayo imefanyiwa ukarabati mkubwa na benki ya CRDB. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Dk. Charles Kimei akishiriki katika zoezi la kufanya usafi. Hafla hiyo ilifanyika mjini Morogoro juzi. Kulia ni Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo.


 Mkurugenzi wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akiteta jambo na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Steven Mashishanga.


 Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid (katikati) akipokea mfano wa ufunguo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB Dk. Charles Kimei wakati wa kukabidhi jengo la wodi ya watoto ya Hospitali ya Mkoa wa  Morogoro,  ambayo imefanyiwa ukarabati mkubwa na benki hiyo. Hafla hiyo imefanyika mjini Morogoro juzi. Kushoto ni Mkurugenzi wa benki ya CRDB tawi la Morogoro, Pendo Assey.


 Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid  akizindua wodi ya watoto katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro.


 Kutembelea wodi ya watoto.


Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid akitandika kitanda baada ya uongozi wa Benki ya CRDB kukabidhi jengo la wodi ya watoto lililofanyiwa ukarabati mkubwa na benki hiyo. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akitandika kitanda baada ya uongozi wa Benki ya CRDB kukabidhi jengo la wodi ya watoto lililofanyiwa ukarabati mkubwa na benki hiyo. 
 Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid (kulia), na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei wakiweka chandarua katika kitanda wakati walipotembelea wodi ya watoto katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro baada ya uongozi wa benki ya CRDB kukabidhi jengo la wodi hiyo ambayo imefanyiwa ukarabati mkubwa na benki hiyo. Kulia aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Juma Ngasongwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akizungumza wakati wa hafla hiyo. 
 Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi jengo la wodi ya watoto katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro baada ya kufanyiwa ukarabati na Benki ya CRDB. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Dk. Charles Kimei.

Picha ya pamoja. 

 Wafanyakazi wa benki ya CRDB Mkoa wa Morogoro.
 Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB Dk. Charles Kimei akiingia ukumbini wakati wa hafla iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wao. 
Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja, Tully Mwambapa akizungumza wakati wa hafla iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wadau wao.
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB Dk. Charles Kimei akizungumza na wadau wa benki hiyo katika ukumbi wa Nashera mjini Morogoro. 
 MC wa hafla hiyo akiwa kazini.
 Msanii Mrisho Mpoto wa Mjomba Band akiimba kwa hisia. Kulia ni mwimbaji wa benki hiyo, Ismail Kipira.
 Aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Juma Ngasongwa ambaye kwa sasa ni mkulima wa Mpunga akiwa na wadau kataika hafla hiyo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akikata keki na Mkurugenzi wa tawi la Morogoro,  Pendo Assey. 
 Mdau wa benki ya CRDB, Naibu Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo akipata keki.
 Wateja mbalimbali wakipa keki.
 Vinywaji kama kawa.
Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB, Godwin Semunyu (kushoto) akiwa na maofisa wa benki hiyo.
 Muziki ulishika kasi