Tuesday, November 27, 2012

WADAU WAJITOKEZA KUCHANGIA HARAMBEE YA UJENZI WA MABWENI YA WANAFUNZI ILIYORATIBIWA NA TEA


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Rosemary Lulabuka (kulia) akiongozana na mgeni rasmi katika harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wasichana, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa mstaafu, Dk. Asha Rose Migiro ambapo katika harambee hiyo jumla ya shilingi milioni 278 zilipatikana.
Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Dk. Naomi Katunzi akizungumza katika harambee hiyo.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa akizungumza wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa mabweni ya wanafunzi.
Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha Rose Migiro akipokea mchango wa shilingi milioni tatu kutoka kwa  Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa ukiwa ni mchangop wake kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa mabweni ya wasichana iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Meneja Mawasiliano wa TCRA, Inocent Mungi akikabidhi mchango wa shilingi milioni tano kwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa mstaafu, Dk. Asha Rose Migiro wakati wa harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwanasheria wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Vupe Ligate akipeana mkono na Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Matifa, Dk. Asha Rose Migiro baada ya kuchangia katika harambee ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike ambapo jumla ya shilingi milioni 278 zilipatikana katika harambee hiyo.
Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha Rose Migiro akimshukuru Mkurugenzi Mkuu wa Rex Energy, Francis Kibisa kwa mchango alioutoa katika harambee ya kuchangia ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike
Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha Rose Migiro (katikati) mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni tano kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Benki ya KCB Tanzania, Christiane Manyeye (kulia) na mwakilishi wa ubalozi wa Kenya, Boniface Makao wakati wa harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike iliyofanyika jijini Dar es Salaam juzi. Wa pili kushoto ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa.
Miss Tanzania 2005, Nancy Sumari akikabidhi mchango wa dola za kimarekani 1,000 kwa  Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha Rose Migiromgeni ambaye alikuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya  ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike iliyofanyika jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, mstaafu Dk. Asha Rose Migiro (kushoto) akimkabidhi cheti cha shukrani, Mkuu wa Kitengo cha mahusiano wa Shirika la Nyumba (NHC), Susan Omari baada ya shiriki hilo kuchangia mabati 1,000 yenye thamani ya shilingi milioni 20 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Wasanii wa kundi la THT wakitumbuiza katika harambee hiyo.
Mkurugenzi wa Radio One, Deogratius Rweyunga akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha Rose Migiro ambaye alikuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya harambee ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike iliyofanyika jijini Dar es Salaam 
Mmiliki wa Blog ya 820,  Shamim Mwasha, akitoa mchango wa shilingi laki 6.5 alizokusanya kutoka kwa wasomaji wa mtandao wake.
Baadhi ya wadau waliojitokeza katika harambee hiyo

No comments: