Thursday, December 31, 2015

Waraghbishi wilayani kahama wapania Kumkomboa Mwanamke

Na Krantz Mwantepele .Kahama

Wanawake ni nguzo muhimu sana katika uchumi wa watanzania wengi. Mwanamke ana ushawishi mkubwa na hasa pale anapoamua kuwa chachu ya maendeleo. Na hasa anapowezeshwa kufanya hivyo.

Katika kufanikisha hili waraghbishi wameamua kutoa mafunzo ya uraghbishi kwa makundi mengine ya jamii. Mojawapo ya kundi hilo ni la wanawake. Waraghbishi wapya toka katika kijiji cha Nyandekwa, kati ya hao wapo 9 ambao ni wanawake.
Mmoja wao ni Anna Alphonce, Mwenyekiti wa kitongoji cha Busolo, katika kijiji cha Nyandekwa. Akielezea jinsi alivyoanza uraghbishi alisema:
“Mi niliona kuna kikundi wanakaaga humu karibu kila jioni. Na kila nilipokuwa napita jirani na hapa naona watu wamejaa, basi nikapenda namimi nijiunge nao na hasa baada ya kujua nini wanafanya. Na hapo ndipo nilipoanza uraghbishi,”
Anna Alphonce (katikati) ambaye ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Busolo akifafanua jambo wakati akielezea uraghbishi anaofanya .

Akiwa kama mwenyekiti mwanamke wa kitongoji aliweza kutumia nafasi yake kufanya uraghbishi kwa anaowaongoza. Kwa kuwa kilikuwa ni kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu, aliitisha mikutano kwenye kitongoji chake kwa lengo la kutoa hamasa ya wananchi kujitokeza kwa wingi. Kwa nafasi yake aliweza kuyafikia makundi ya wazee, vijana na wanawake. Ingawa kati ya hawa wanawake ndio walikuwa washiriki wazuri.

“Msisitizo kwenye mikutano yangu ilikuwa ni kupiga kura kwa amani. Niliwasihi Vijana wetu wasiwe chanzo cha vurugu na badala yake wawe walinzi na kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika mazingira ya utulivu,”

Haya ni maelezo ya mwenyekiti huyo akielezea jinsi alivyotumia nafasi yake kwenye kufanya hamasa ya amani. Akaongeza, “Kwangu mimi haya ni mafanikio kwa sababu kweli uchaguzi umefanyika kwa amani katika kitongoji change.”

Mraghabishi mwingine ni Matrida Peter toka katika kijiji cha Nyandekwa, yeye uraghbishi wake alifundishwa na Elizabeth Ngaljalina toka kijiji hicho hicho. Baada ya kufundishwa yeye alichoamua kufanya uraghbishi kwa vijana wa kijiji cha Nyandekwa pamoja na wale waliokuwa mashuleni pia.

Akielezea jinsi ambavyo anafanya uraghbishi kwa vijana, Matrida anasema,
“Nafundisha makuzi ya ujana ili kuweza kutimiza ndoto zao. Kwanza nawaelewesha kuhusu mabadiliko ya miili yao hasa wanapoingia hatua ya kubalehe na kuvunja ungo. Hii inawasaidia jinsi ya kujikinga na maambuzi ya virusi vya ukimwi.”

Uraghbishi wake hauishii kwa vijana walio nje ya shule, hivyo alikwenda kumtembelea ili aweze kupata fursa ya kutoa elimu hiyo hasa kwa wanafunzi ya shule ya msingi. Walengwa wakubwa wakiwa ni wanafunzi wa kuanzia darasa la nne mpaka la saba. Akielezea rika la watoto hao, Matrida anasema:

“Watoto wa siku hizi wana maumbo makubwa, hivyo hao wa darasa la nne mpaka la saba sio wadogo kiumbo na wengi ndio wapo kwenye huo umri. Wanahitaji mwongozo manake makuzi siku hizi yameachwa kwa wazazi na wao mda mwingine wanaona aibu kuongea nao,”

Matokeo ya uraghbishi huu wa mwanamama Matrida ni kuongeza kwa watoto wenye uelewa wa mipango ya uzazi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi. Kwani maambukizi katika wilaya ya Kahama yapo juu kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini.

Uraghbishi una maana tofauti tofauti kwa wanawake hawa wa kijiji cha Nyandekwa, kama anavyoelezea Mariam Stephano aliyeanza uraghbishi mwezi Septemba 2015:

“Uraghbishi kwangu mimi ni kutetea haki za vijana na mabinti, na sio tu kutetea bali kujua na falsafa yake ya jinsi ya kutenda ili kufanikisha lengo hilo ninaloliangalia kama  ndio jukumu langu,”

Wakati Suzan Stephano yeye analinganisha uraghbishi na haki za kikatiba. Huku akisisitiza umuhimu wa kuthaminiwa kwa mwanamke katika kijiji chao na taifa kwa ujumla. Na yeye pia anakiri kwa uraghbishi ni falsafa ya jinsi ya kutenda.
Waraghbishi wanawake toka katika kijiji cha Nyandekwa wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kitongoji cha Busola akielezea uraghbishi wake katika ngazi ya kitongoji

Mraghbishi mwingine ni Mwenyekiti wa kitongoji cha Bujika, Adam Joseph yeye alijiunga na uraghbishi mwezi Septemba 2015, kwa kutumia nafasi yake uwenyekiti alitambulisha uraghbishi kwenye kitongoji chake.

“Cha kwanza nilichofanya ni kuongea na mtendaji wa kijiji na kukubaliana tunahitaji kufanya hamasa kwa vijana ili wawe wanafika katika mikutano ya vijiji. Hivyo nikaanza kupita kwenye vijiwe na kuwahamasisha vijana waweze kufika mikutanoni. Na tuliwalenga vijana wote wa kike na wa kiume,” anaelezea Adam.

Vijana walimwambia mwenyekiti wao kwamba wao hawasikilizwagi wakija kwenye mikutano na hivyo hawaoni umuhimu wa kuja kwenye mikutano ya vijiji. Majibu haya yalimpelekea mwenyekiti kuitisha mkutano uliowausisha vijana na wazee kwa pamoja.

“Nimeshaitisha mikutano miwili, muamko bado si mkubwa sana kwani bado vijana hawaoni umuhimu wa kushiriki mikutano hii. Lakini hili halinikatishi tamaa najua hapa ni mwanzo tu,” anaelezea Adam.


Kwa hakika hizi ni harakati za kweli katika kumwezesha mwanamke na jamii kwa ujumla. Waraghbishi kwa pamoja wanakili kwamba uraghbishi ni falsafa ya kutenda. Swali la msingi kwetu sote, je na sisi tunatenda na kama ndio tunatumia falsafa gani.

                                   CHANZO; MWANAHARAKATI MZALENDO

Wednesday, December 30, 2015

Ligi Kuu ya Zanzibar: JKU yaitandika KVZ bao 2-0 katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Amaan

Wachezaji wa Timu ya JKU wakisalimiana na Wachezaji wa Timu ya KVZ kabla ya kuaza mchezo wao wa Ligi Kuu ya Zanzibar uliofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar Timu ya JKU imeshinda 2-0.

Mchezo uliochezwa jioni mabao ya JKU yamefungwa katika kipindi cha kwanza na katika dakika ya 8 mshambuliaji wa Timu ya JKU Mbarouk Chande ameipatia bao timu yake katika dakika ya nane ya mchezo huo kipindi cha kwanza na Bao la ushindi la JKU limepatikana katika kipindi hicho cha kwanza katika dakika ya 35 ya mchezo huo lililofungwa na mshambuliaji wake Nassor  Mattar.
Kocha Mkuu wa Timu ya KVZ King akifuatilia mchezo huo wakati timu yake ikiwa nyuma kwa mabao 2-0. 
Beki wa timu ya KVZ Juma Abdalla, akijiandaa kumzuiya mshambuliaji wa Timu ya JKU mwenye mpira Nassorv Mattar, wakati wa mchezo wao wa Ligi Kuu ya Zanzibar uliofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar. 
Mshambuliaji wa Timu ya JKU Mbarouk Chande(kulia) akimpita beki wa Timu ya KVZ Emill Wiliam  

Mshambuliaji wa Timu ya JKU Mbarouk Chande, akimiliki mpira huku beki wa timu ya KVZ Emill William akijiandaa kumzuiya.  
Mshambuliaji wa Timu ya JKU Mohammed Abdalla akimpiga chenga golikipa wa timu ya KVZ Yakub Bakari. hatimai mpira huo na kutoka nje ya uwanja. 

Mshambuliaji wa Timu ya KVZ Masoud Abdalla mwenye jezi ya kijani akimpita mchezaji wa timu ya JKU  Mbarouk Chande. 
Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot
Zanzinews.com.

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

Askari wawili wa jeshi la polisi wafariki dunia huku wengine wawili wakijeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakifanyia dori kupinduka.https://youtu.be/41LXwrwVCdQ

Serikali imesema itaanza program maalum ya kitaifa ya upandaji miti kuanzia januari mwakani kwa ajili ya kuendeleza mazingira na uhai.https://youtu.be/JDgVYy-q23E
Siku chache kabla ya mradi wa mabasi ya mwendokasi kuanza kufanya kazi baadhi ya madereva wasio makini waelezwa kuharibu miundombinu ya mradi huo. https://youtu.be/_Umh1_T4qp8

Watuhumiwa 8 walioshitakiwa kwa kuhusika na upotevu wa makontena zaidi ya 249 bila kulipiwa ushuru bandarini wapandishwa kizimbani hii leo.https://youtu.be/KRoA9sQrhdU

Gari pekee la kikosi cha zimamoto manispaa ya Lindi lapata ajali wakati likipeleka huduma ya maji kwenye makazi ya viongozi.https://youtu.be/ED3X3DG52gQ

Rais John Magufuli ametua makatibu wakuu na manaibu katibu wakuu wapya katika ikulu jijini Dar es salaam. https://youtu.be/WKv0B35C8KI

Mchumi wa siku nyingi na mwenyekiti wa mstaafu wa CUF Prof.Lipumba aeleza hofu yake huku akisema huenda Tanzania ikakosa misaada ya wahisani kutokana na mkwamo wa kisiasa Zanzibar. https://youtu.be/vFBMPE21af4

Serikali imesema itahakikisha upatikanaji wa uhakika wa dawa na vifaa tiba katika hospitali za umma ili kuondoa kero za mda mrefu kwa wananchi kununua dawa kwa gharama kubwa. https://youtu.be/K3wCIRxBbzk

Waziri mkuu Kassim Majaliwa awatahadharisha wakimbizi wa Burundi waliohifadhiwa nchini kuacha tabia ya kuingia na silaha nchini kinyemela.https://youtu.be/IjRslLTN_U0

Naibu waziri wa Afya Hamis Kingwala afanya ziara ya kushitukiza katika hospitali ya Kitete mkoani Tabora huku akikuta mapungufu kadhaa na kutoa maagizo. https://youtu.be/e7wKp4m1Sos

Mamlaka ya mapato mkoani Morogoro yagawa mafuta ya kupikia kwa taasisi mbalimbali baada ya kukamatwa yakiingizwa mkoni humo kinyume cha sheria kwa kukosa kodi. https://youtu.be/BsQpYlBheSc

Je unafahamu umuhimu wa Wosia katika kupunguza migogoro katika miradhi? Fuatilia hapa ujuzwe na kuelimika na mengi. https://youtu.be/4ud9bV5cfyE

Waziri mkuu Kassim Majaliwa atoa siku 2 kwa Katibu tawala mkoa wa Kigoma kukamilisha uchunguzi juu ya ubadhilifu wa fedha;https://youtu.be/GhO_pSTthfo

Mamlaka ya mawasiliano nchini TCRA imetoa adhabu kwa kampuni tano za simu za mkononi nchini kwa kushindwa kusimamia usalama wa wateja wao;https://youtu.be/FrUEDd_enag

Wakazi wa kijiji cha Endeshi wilayani Karatu wanakabiliwa na changamoto za ukosefu wa wataalamu wa huduma za afya katika kituo cha afya kilichopo kijijini hapo; https://youtu.be/yfHM24fgyj0
Serikali yashauriwa kubadili sheria ya manunuzi pamoja na kuweka kipaumbele kwa utoaji zabuni kwa viwanda vya ndani kwa lengo la kuendeleza viwanda vilivyopo nchini; https://youtu.be/uEcHs0iIzw0

Mwanauchumi nguli nchini Prof. Ibrahim Lipumba amempongeza Rais mstaafu Jakaya Kikwete kwa kuimarisha uhusiano wa Tanzania na nchi za nje;https://youtu.be/IunWL_rBp88

Klabu ya Simba imesema ipo katika hatua za mwisho za mazungumzo na mwekezaji Mohamed Dewji kuwekeza katika katika klabu hiyo;https://youtu.be/vgYf6ENtC7w

Klabu ya Yanga imekumbwa na bomoa bomoa inayondelea jijini Dar es Salaam kwa uwanja wake wa Kaunda kubomolewa; https://youtu.be/-8q32KS_9G8

Televisheni moja ya nchini marekani imeandaa mdahalo kwa wagombea wa shirikisho la mpira dunia FIFA kwa lengo la kupata kiongozi bora atakayesimamia shirikisho hilo; https://youtu.be/OahMGZa3w58

Watu wanne wamefariki dunia na wengine watatu kunusurika kifo mkoani Mwanza baada ya Mtumbwi waliokuwa wakisafiria kupinduka;https://youtu.be/oxKF-EAcq8g


Rais John Magufuli amefanya mabadiliko ya makatibu wakuu na manaibu wakuu katika baadhi ya wizara na kuteua wengine wapya;https://youtu.be/lM8blu714Bw
Baadhi ya wananchi mkoani Shinyanga wameiomba serikali kuingilia kati tatizo la kupanda kwa gharama ya huduma za maji mkoani humo;https://youtu.be/djysToHXTPA

Wawakilishi wa watu wenye ulemavu wameviomba vyombo vya habari nchini kuajiri wafanyakazi wanaoweza kutafasiri habari pamoja na vipindi kwa kutumia lugha ya alam

Shirika la viwanda vidogo nchini SIDO limeingia makubaliano na serikali ya Canada kuwapatia wataalamu wa kufundisha uanzishwaji wa viwanda vidogo hapa nchini; https://youtu.be/fcQJiwc2OWE

Serikali inatarajia kuanza programu ya kitaifa ya upandaji miti kuanzia januari mwakani ili kuendeleza mazingira na misitu nchini;https://youtu.be/YvD8kW7gf_0

Shirikisho la soka hapa nchini TFF limeiomba serikali kuliruhusu kuendesha michuano ya soka katika shule za misingi na sekondari;https://youtu.be/4LwNUdyLNoI

Klabu ya Azam imerejea kileleni mwa ligi kuu soka Tanzania bara mara baada ya kuitandika Mtibwa Sugar ya mkoani morogoro kwa goli 1 kwa 0;https://youtu.be/Jumt_f8bXdA

Serikali imeaomba watanzania kumuombea dua mchezaji Mbwana Samatta kushinda tuzo ya mchezaji bora Afrika kwa wachezaji wa ndani;https://youtu.be/-AFntsWf9XE

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI INAKUSUDIA KUVIFUTA VYAMA VYA KIJAMII VIFUATAVYO BAADA YA KUKIUKA TARATIBU ZA USAJILI

ORODHA YA VYAMA VINAVYOPEWA KUSUDIO LA KUFUTWA TAREHE 30/12/2015
S/NO.
REG. NO
NAME OF SOCIETY
TAREHE YA USAJILI
MALIPO YA ADA
MABADILIKO YA UONGOZI
MAPATO NA MATUMIZI
MAHALI CHAM KILIPO
1
SO .8629
EBENER MALYI MINISTRY
15/08/1996
-


MARANGU -  MOSHI
2
SO. 7290
AFRICA REWEF AND DEVELOPMENT CONSULTANCY ASSOCIATION
1/9/1990



ARUSHA STREET ILALA
3
SO. 6996
CHAKUWAJALI TAWI LA MKOA WA DSM
17/07/1950



DAR ES SALAAM
4
SO. 6220
TANZANIA BULGARIAN SOCIETY FOR CULTURAL RELATION & FRIENDSHIP
24/04/1981



DAR ES SALAAM
5
SO. 9169
TANZANIA ASSOCIATION OF FLORICULTURE (TAFA)
17/10/1997



ARUSHA
6
SO. 9799
MICRO ENTERPRISES AND CREDIT FACILITY POVERTY ALLEVIATIONS
29/03/1999



TUNDUMA
7
SO. 9980
HUMAN ECOLOGY ACTION LEAGUE OF TANZANIA
22/12/1999
2003


MBEYA
8
SO. 8830
MASSAI LIFE FUTURE CARE




ARUSHA
9
SO. 7397
NZEGA - IGUNGA DEVELOPMENT ASSOCIATION (NIDA)
12/12/1991



DAR ES SALAAM
10
SO. 8332
AFRICA HUMAN RIGHTS AND JUSTICE PROTECTIONS NETWORK
1/4/1996



DAR ES SALAAM
11
SO. 9896
YOUTH SOCIAL SECURITY AND ENVIROMENT ORGANIZATION
10/7/1999
1999/10


NYAKATO -  MWANZA
12
SO. 6903
MORI DEVELOPMENT ASSOCIATION
27/11/1987
1987
1996
1995
LUMUMBA DSM
13
SO. 7319
UMOJA WA MAENDELEO WA WILAYA YA PANGANI
2/19/2011
1991


PANGANI
14
SO. 7014
CO-OPERATIVE COLLEGE ACADEMIC STAFF (CCASA)
17/04/1987
1989


MOSHI
15
SO. 8303
WORLD EVANGELISTIC MINISTRIES (WEMI)
6/16/1905
1994


MOSHI
16
SO. 6810
SHREE DAR ES SALAAM LUHARGNATI MANDAL
1987



KISUTU - DSM
17
SO. 5990
BRITAIN - TANZANIA SOCIETY

1976


DAR ES SALAAM
18
SO. 6956
INTERNATIONAL MISSIONARY SOCIETY UNION OF SEVENTH DAY ADVENTIST REFORM MOVEMENT OF TANZANIA
24/11/1990
2009
1996
1997
NKRUMAH - DSM
19
SO. 9362
YOUTH FUTURE CONCERN (YOFCO)




DAR ES SALAAM
20
SO. 7948
AFYA BORA MOBILE MEDICAL UNIT (T)
18/10/1993
2003


ARUSHA
21
SO. 7874
WORLD WIDE EVANGELISTIC CHURCH

1993


ARUSHA
22
SO. 7723
NZEGA EDUCATION TRUST FUND
15/07/1992
1999


NZEGA
23
SO. 7170
TANZANIA ASSOCIATION OF CONSULTANTS (TACO)
21/05/1989
1998


DAR ES SALAAM
24
SO. 7761
TANZANIA MUSIC COPYRIGH ASSOCIATION (TMCA)

2000


DAR ES SALAAM
25
SO. 7934
KIFUNGIRO PARENTS ASSOCIATION
8/10/1993
1998


DAR ES SALAAM
26
SO. 7307
KANISA LA UJUMBE WA WAKATI WA MWISHO
4/6/1990



MBEYA
27
SO. 6923
SHINYANGA REGION EDUCATION TRUST BOARD




SHINYANGA
28
SO. 7940
THE SOCIETY OF THE PRECIOUS BLOOD
18/12/1993



DAR ES SALAAM
29
SO. 7649
THE EASTERN AFRICAN ROCK ART RESEARCH ASSOCIATION




TANZANIA
30
SO. 7063
SPIRITUAL CHURCH OF GOD
26/11/1991



TANZANIA
31
SO. 7626
THE JANE GOOD ALL INSTITUTE FOR WILDLIFE RESEARCH EDUCATION AND CONSERVATION
3/4/1992



DAR ES SALAAM
32
SO. 7962
NYAKATO SOCIAL CLUB MWANZA
3/1/1994



MWANZA
33
SO. 7964
CHAMA CHA USTAWI WA JAMII NA UCHUMI TANZANIA
4/2/1994



DAR ES SALAAM
34
SO. 7722
KOREA AFRICA MISSION SUPPORT
20/10/1992



DAR ES SALAAM
35
SO. 7421
THE BIG NOVEMBER CRUSADE MINISTRIES
3/4/1991



DAR ES SALAAM
36
SO. 127
THE DAR ES SALAAM EUROPEAN RAILWAY CLUB
30/07/1954
1998


DAR ES SALAAM
37
SO. 7304
KORONGORO INTERGRATED PEOPLE ORIENTED TO CONSERVATION
10/10/1990
1999


ARUSHA

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

30/12/2015