Saturday, April 27, 2013

CENTURY CINEMAX MLIMANI CITY | NOW SHOWING: (26 APRIL – 02 MAY 2013)




[OBLIVION [PG-13]*Tom Cruise
[- 12 pm*/ 2:30 pm / 5 pm / 7:30 pm & 10 pm]

[A HAUNTED HOUSE [R]* Marlon Wayans- 6 pm / 8 pm & 10 pm ]

[OLYMPUS HAS FALLEN [PG-13]*Gerard Butler, Morgan Freeman
-5pm / 7:30 pm & 10 pm]

[G.I. JOE RETALIATION 3D [ALL AGES]*Dwayne Johnson
12 pm*& 2:30 pm]

 [THE CROODS 2D [ALL AGES]*2D ANIMATIONS12 pm*/ 2 pm & 4 pm ]

(*12 pm / 12:30)-Shown on SUN & P-HOLIDAY
(*) - ALL 3D & 2D movies price per ticket tsh 10,000
except Tuesdays & Thursdays Tshs 8,000 per ticket(not applicable on public holidays)


CENTURY CINEMAX - MWENGE BRANCH | NOW SHOWING:
(26 APRIL – 02 MAY 2013)
[NEW WORLD CINEMAS - MWENGE]
*All Shows-Everyday -Price per ticket Tshs 7000 only

[EK THI DAAYAN [ALL AGES] *Emraan Hashmi
 – 2:30 pm / 5 pm / 7:30 pm & 10 pm]

 [COMMANDO – ONE MAN ARMY [ALL AGES] *Vidyut Jamwal
 – 2:30 pm / 5 pm & 7:30 pm]

*Mondays closed, except public holiday


FORTHCOMING MOVIES STARTS FRIDAY 03RD MAY 2013:

[IRON MAN 3 in 3D [PG-13]*Robert Downey Jr.
– CENTURY CINEMAX – MLIMANI CITY MALL]

[ESCAPE FROM THE PLANET EARTH 3D [PG]*3D ANIMATION]
– CENTURY CINEMAX – MLIMANI CITY MALL]

[SHOOTOUT AT WADALA [ALL AGES – HINDI MOVIE]*John Abraham, Priyanka Chopra
– CENTURY CINEMAX – MWENGE BRANCH ( NEW WORLD CIENMAS – MWENGE)]


26 APRIL - 02 MAY 2013  CENTURY CINEMAX.jpg
19 - 25 APRIL 2013 NEW WORLD CINEMAS.jpg
MOVIE REVIEW-CCL -IRON MAN.jpg
MOVIE REVIEW-CCL -OB.jpg

ENJOY!!

Wednesday, April 24, 2013

UNIC Dar yawahamasisha wanafunzi kujijengea utamaduni wa kusoma vitabu


Katika maadhimisho ya siku ya siku ya uandishi wa Vitabu na Hati Miliki Duniani Afisa Habari wa Kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa (katika ngazi ya Kimataifa) UNIC Bi. Stella Vuzo akizungumza na wanafunzi wa shule mbalimbali waliohudhuria semina fupi iliyoandaliwa na UNIC na kuwafafanulia umuhimu wa kusoma vitabu mbalimbali ambapo wanaweza kujifunza mambo tofauti ikiwemo kujua takwimu za ugonjwa hatari wa Malaria hapa nchini ambao umekuwa ukiongoza kwa kusababisha vifo vya watoto wenye umri chiniya miaka 5, hivyo kwa usomaji vitabu wanaweza kujua namna ya kujikinga na wanapogundua dalili kuweza kuwahi kupata matibabu.
Wanafunzi wa darasa la Saba shule ya msingi Oysterbay wakimsikiliza kwa makini Afisa Habari wa UNIC (katika ngazi ya Kimataifa) Bi. Stella Vuzo (hayupo pichani) wakati akielezea kazi zinazofanywa na Shirika la Afya Duniani WHO lililochini ya Umoja wa Mataifa katika kuhakikisha Ugonjwa wa Malaria unatokomezwa duniani katika nchini za kusini mwa Jangwa la Sahara. Ikiwa zimebaki siku mbili kuadhimisha siku ya Malaria duniani inayodhimishwa kila mwaka Aprili 25 wakati wa siku ya kuadhimisha siku ya uandishi wa vitabu na hati miliki duniani.
Msaidizi wa Maktaba ya UNIC Harriet Macha akiendesha chemsha bongo kwa wanafunzi walioshiriki semina hiyo kupima uelewa wao kuhusiana na Ugonjwa wa Malaria.
Picha juu na chini ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Usomaji na Maendeleo Bi. Demere Kitunga ambaye ni mmiliki wa Book Cafe iliyopo maeneo ya Mikocheni jijini Dar akiwaelezea wanafunzi umuhimu wa kuwa na nia na dhamira ya kujenga utamaduni wa kujisomea vitabu vya nyanja mbali mbali ikiwemo vya Kiada, Ziada na vya maarifa ambapo amewapa changamoto kujianzisha Maktaba binafsi na vikundi ambapo wanaweza kuchangishana fedha kidogo kwa uwezo wao ili kuweza kujinunulia kitabu ambacho wanaweza kushirikiana kusoma ambavyo vitawapa uwezo wa kujitambua, kuwa na maamuzi, kupata uelewa wa vitu tofauti vinavyoweza kuwajengea kujiamini na kuwawezesha kubadilisha mfumo wa maisha katika makuzi yao.
Katibu Mkuu wa Mtandao wa Vilabu vya Umoja wa mataifa Tanzania (UNCTN) Bernadetha Mshana akionyesha moja ya kitabu kilichomsaidia kuweza kupata uelewa wa kuongea Kingereza kwa urahisi zaidi ikiwa ni ushuhuda wake kwa vijana wenzake kuwa usomaji vitabu hupanua uelewa wa mtu na kujua mambo mengi.
Msaidizi wa Maktaba ya UNIC Harriet Macha (wa pili kulia) akiwa na baadhi ya walimu waliombatana na wanafunzi kutoka shule za msingi Kumbukumbu, Oysterbay na Hananasif.
Katibu Mkuu wa Mtandao wa Vilabu vya Umoja wa mataifa Tanzania Bernadetha Mshana akishirikiana uzoefu na wanafunzi wa shule za msingi za jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya siku ya usomaji vitabu duniani na Hati miliki ambapo amesema ambapo amewataka wanafunzi hao kujiunga na vilabu vya usomaji vitabu ambavyo vitawapatia uzoefu kama ambavyo yeye vimemwezesha kujiamini kuwa na uelewa na kufikia hapo alipo sasa.
Afisa habari wa UNIC katika ngazi ya Taifa Usia Nkhoma akitoa neno la shukrani kwa wanafunzi walioshiriki semina fupi iliyoandaliwa na kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC katika maadhimisho ya siku ya uandishi wa Vitabu na Hati Miliki Duniani. Siku hii imetengwa rasmi ili kuhamasisha usomaji, auandishi na uchapishaji wa vitabu kupitia hati miliki.
Katibu Mkuu wa Mtandao wa Vilabu vya Umoja wa mataifa Tanzania Bernadetha Mshana (kushoto) akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa Book Cafe iliyopo Mikocheni jijini Dar.
Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi wakisoma vitabu mbalimbali vinavyopatikana katika Maktaba ya Book Cafe yenye mandhari nzuri ya kujisomea ambapo pia panapatikana viytabu vya watu wazima vinavyohusiana na nyanja mbalimbali.

Tuesday, April 23, 2013

MAGIGE FOUNDATION YATOA MSAADA DODOMA

Asasi ya Kijamii ya Catherine Foundation jana imetembelea kituo cha kulelea wa watoto cha Matumaini Village kilichopo mkoani Dodoma ambapo walikwenda kutoa misaada mbalimbali wakiongozwa na Mkurugenzi wa Asasi hiyo, Catherine Magige. 
 Katika Hafla hiyo Mgeni Rasmi alikuwa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda ambapo asasi hiyo ilitoa vitu mbalimbali vikiwemo, Madaftari, Mafuta, Sabuni, Juice, miswaki na dawa zake, mchele, sukari, nguo za watoto, kanga za wakinadada wanaowalea watoto hao na vingine vingi.
Mama Tunu Pinda akihutubia
 Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akihutubia katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Mhe Catherine Magige akihutubia katika hafla hiyo
 Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Catherine Magige akizungumza na watoto wanaolelewa kwenye Kito cha Matumaini Village kilichopo Dodoma alipokwenda kutoa msaada 
Mhe Catherine Magige akicheza na mmoja wa watoto wa kituo hicho
 Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Mhe Catherine Magige akiwa na mtoto mchanga anaye lelewa katika Kituo cha Matumaini Village mjini Dodoma jana.
 Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda na Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Mhe Catherine Magige wakizungumza na watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho.
Mama Tunu Pinda na Mhe Catherine Magige wakiwa na watoto hao
 Mama Tunu Pinda akikabidhi zawadi mbalimbali zilizotolewa na asasi hiyo 
Misaada mbalimbali ikitolewa
Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Catherine Magige akizungumza na watoto wanaolelewa kwenye Kito cha Matumaini Village kilichopo Dodoma alipokwenda kutoa msaada