Monday, October 29, 2012

Mh Balozi Kallaghe Asherekea siku kuu ya Iddi na Wanajumuiya za Tanzania nchini -UK

Siku ya Jumamosi tarehe 27.10.12 Mh Balozi wetu wa Tanzania nchini Uingereza,Mh. Peter Kallaghe alishiriki sherehe ya siku kuu ya Iddi iliyofanyika London mashariki.

Sherehe hii ya baraza la EID (IDDI) iliyoandaliwa na Jumuiya ya East African Education Foundation wakishirikiana na Jumuiya ya Wazanzibari waishio UK (ZAWA).

 Wakati akitoa hotuba yake Mh Balozi Peter Kallaghe ambaye ndio aliekua mgeni rasmi siku hiyo, alianza kwa kuwashukuru kwa mualiko huo mzuri alioupata na kuwatakia kila kheri wale wote waliofanikiwa kutekeleza HIJA kwa mwaka huu 2012.

Aidha Mh Balozi aliahidi kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya Ubalozi na Jumuiya mbalimbali za Watanzania zilizopo nchini Uingereza na Ireland.

Pia alivutiwa na kuipongeza hatma ya East African Education Foundation kuazimia kununua Jengo kwa ajili ya shughuli za kijamii na wanajumuiya wote kwa ujumla. Baada ya kumaliza hotuba yake Shekhe Nasssor Haroub nae aliongea na wanajumuiya akitilia mkazo zaidi umuhimu wa Umoja na mshikamano kama Uislamu unavyo sisitiza kupitia Ibada ya HIJA.

Vilevile vijana wa kasida walipata fursa ya kutumbuiza alipomaliza kuongea Shekhe Nassor. Mwishoni Balozi alifanya ziara fupi ya kukagua jengo la Jumuiya hiyo na kupata maelezo kutoka kwa viongozi mbalimbali wa Jumuiya ili kujua namna gani litakavyoweza kutumika mara baada ya hatua za ununuzi zitakapo kamilika rasmi kwa gharama za paundi laki 6 (£600,000)

Asanteni,

Urban Pulse Creative
Mh Balozi katika akipokea zawadi kutoka kwa wanajumuiya
Mh. Balozi Peter Kallaghe akiwa katika Picha ya pamoja na Wanajumuiya ya East African Education Foundation.
Mwenyekiti wa ZAWA,Hassan Khamis akimfafanulia jambo Mh Balozi.
Ustadhi akiongea machache wakati wa chakula.
Vijana wa Kasida wakitumbuiza.
watoto wa Kasida wakisikiliza Hotuba ya Mh Balozi.

Sunday, October 28, 2012

HAFLA YA KUMUAGA KANAL MJENGWA DC MBINGA YAFANA SANA

Kutoka kushoto mkuu wa wilaya ya Nyasa Ernest Kahindi,mkuu wa wilaya ya mbinga mstaafu Kanal Edmund Mjengwa,mkuu wa mkoa wa Ruvuma,Said Mwambungu,mkuu mpya wa wilaya Mbinga Senyi Ngaga na Mama Hanab Mwambungu wakigonga cheers wakati wa sherehe ya kumuaga Kanal Mjengwa jana mjini Mbinga.
Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya Mbinga Shaibu Mnunduma akigonganisha glass na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu wakati wa sherehe ya kumuaga aliyekuwa mkuu wa Wilaya hiyo Kanal mstaafu Edmund Mjengwa.
Askofu wa jimbo la Mbinga John Ndimbo akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu jana mjini Mbinga wakati wa sherehe ya kumuaga Mkuu wa zamani wa wilaya ya Mbinga kanal mstaafu Edmund Mjengwa mjini Mbinga.
Mkuu wa zamani wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma Kanal mstaafu Edmund Mjengwa akizungumza jana mjini Mbinga wakati wa sherehe yake ya kumuaga,katikati mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu na kulia mkuu mpya wa wilaya hiyo Senyi Ngaga.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akizungumza wakati wa sherehe ya kumuaga aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Mbinga kanal mstaafu Edmund Mjengwa,kulia mkuu wa wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga na kushoto kanal Mjengwa.
Mkuu wa zamani wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma Kanal mstaafu Edmund akikata keki huku akishuhudiwa na mkuu mpya wa wilaya hiyo Senyi Ngaga kulia na mkuu wa wilaya mpya ya Nyasa Ernest Kahindi,wakati wa hafla ya kumuaga iliyoandaliwa na baadhi ya wakazi wa wilaya hiyo.
Mkuu wa zamani wa wilaya Mbinga mkoani Ruvuma Kaanl mstaafu Edmund Mjengwa kulia akimlisha keki mkuu mpya wa wilaya hiyo Seniy Ngaga.
Mkuu mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu wa pili kulia na mkewe mama Hanab Mwambungu wakimpa zawadi kanal Mjengwa jana katika sherehe ya kumuaga Mjengwa mjini Mbinga.
Mkuu wa mkoa wa Said Mwambungu mbele jana,akiwaongoza wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya kumuaga mkuu wa zamani wa wilaya mbinga kanal mstaafu Edmund Mjengwa kucheza muziki.
Mkuu wa wilaya ya mbinga Senyi Ngaga kulia akicheza muziki na mkuu wa zamani wa wilaya hiyo Kanal mstaafu Edmund Mjengwa jana mjini Mbinga.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu na mkewe Hanab Mwambungu wakicheza muzik katika sherehe ya kumuaga kanl Mjengwa mjini mbinga.PICHA NA MUHIDIN AMRI

NAPE,MGEJA NA MAIGE WAFUNGA KAMPENI ZA CCM KATA YA BUGARAMA, KAHAMA

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa kufunga kampeni za CCM za udiwani Kata ya Bugarama, Kahama mkoani Shinyanga, jana Oktoba 27.
Madiwani wa Kata za Kahama wakiwa na mgombea Udiwani wa CCM, Kata ya Bugarama katika wilaya hiyo Nixon Ikoko wakati wa mkutano wa kufunga kampeni za udiwani katika kata hiyo, uliohutubiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimsikiliza kwa makini Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige wakati akimuombea kura mgombea udiwani wa CCM Kata ya Bugarama, kwenye mkutano wa kufunga kampeni za CCM uliofanyika mji mdogo wa Bugarama.
Wazee wakifuatilia kwa makini hotuba ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alipohutubia mkutano wa kufunga kampeni za udiwani za CCM Kata ya Bugarama, Kahama mkoani Shinyanga.
Mzee wa miaka 98, Nickson Toma akifuatilia kwa makini mkutano wa kampeni za udiwani Kata ya Bugarama mkoani Shinyanga uliohutubiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akiwa katika mapokezi ya wananchi alipowasili kwenye mkutano wa kufunga kampeni za CCM za udiwani kata ya Bugarama, Kahama mkoani Shinyanga.
Wananchi katika kata ya Bugarama , Kahama mkoani Shinyanga, wakishangilia wakati wa kufunga kampeni za CCM za uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata hiyo.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige wakishiriki kucheza ngoma ya Baswezi, katika kijiji cha Buyange, Kata ya Bugarama, Kahama mkoani Shinyanga wakati wa mkutano wa kufunga kampeni za udiwani za CCM kata ya Bugarama.
Madiwani wa Kata za Kahama wakiwa na mgombea Udiwani wa CCM, Kata ya Bugarama katika wilaya hiyo Nixon Ikoko wakati wa mkutano wa kufunga kampeni za udiwani katika kata hiyo, uliohutubiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.(Picha na Bashir Nkoromo).

MASISTA WA MERYKNOLL WAADHIMISHA MIAKA 100 YA KUANZISHWA KWAO

 Nembo ya Miaka 100 ya kuanzishwa kwa Shirika la Masista la  MaryKnoll,  Shirika ambalo limekuwa likitoa huduma mbalimbali za kijamii  zikiwamo za Elimu, Afya na Kiroho katika nchi 25  Ikiwamo Tanzania. wale waliosoma,  Nganza/Roselin, au Rugambwa, Nyegezi, na shule nyinginezo katika Ukanda wa Ziwa watakuwa wanawakumbuka sana Masista hawa kwa kazi yao nzuri.  Bango hilo limetundikwa katika Makao Makuu ya Shirika hilo yaliyo katika eneo la Ossining nje kidogo ya Jiji la New York Nchini Marekani.
 Maonesho na mauzo ya bidhaa mbalimbali,   hizi ni baadhi  bidhaa  zikiwamo za kutoka Tanzania,  Kenya, Nambia na  Zimbabwe
 Sister Rosalie Larorte amewahi kukaa  Tanzania kwa miaka zaidi ya 14 anazungumza kiswahili safi, anasema " Naipenda sana Tanzania,  nikakumbuka  ugali wa muhogo  kwa samaki,  mlenda na kashumbari, tena kwenye menu yetu  ya leo  kwenye  shughuli hizi msikose kwenda kula kuna Pilau nyama,  kachumbari na  sambusa"

 Sister  Claudette ambaye akimuuzia mteja  Khanga za Tanzania
 Sister Nunzia yeye alifika  Tanzania mwaka 1946 anazumgumza  kiswahili fasaha, amekaa sana  Musoma anasimulizi nzuri kuhusu  namna alivyokuwa wakifika kumtembelea  Mama Maria Nyerere na Familia yake," siku moja tulikuwa tumekwenda kumtembela  Mama Maria, basi tulipokuwa pale nyumbani, Mwalimu Nyerere akaja akatukuta pale alikuwa tu ndiyo amerudi kutoka safari ya nje sikumbuki ilikuwa  ni nchi gani. akatualika kwenye kumbukumbu  ya kuzaliwa  mtoto wake wa kwanza"
 Zilikuwapo pia bidhaa pia kutoka nchi za Asia kama inavyoonekana hapa
 Na Folk Dance ilikuwepo, Waswede wakilimwaga segere lao
 Sehemu ya wageni waalikwa wakiishangilia  Ntuya Mayenje 
 Watanzania  wakiwaongoza wenzao , kulimwaga  segere la Saida  Karoli  katika  nyimbo yake Ntuya Mayenje. kabla ya kuanza kulimwaga segere lililowaacha hoi wageni wengi, watanzania waliohudhuria hafla hiyo kama kawaida yao walianza kwa kuimba  . wimbo wa "Tanzania, Tanzania,  nakupenda kwa moyo wangu wote, nchi yangu    Tanzania  jina lako ni nzuri sana" wimbo ulioitikiwa  kwa shangwe na masista wanaojuka kiswahili na waliowahi kuishi Tanzania.
Wachina nao walikuwepo 
 Mayenu
 Mori unapopanda inakuwa balaa
 Taratiiiibu
 Hata Mimi  Nayaweza ndivyo anavyojaribu kusema mgeni huyu mwalikwa ambaye kama wengine alishindwa kabisa kujiuzuia akajiunga na watanzania kuicheza Ntuya Mayenje pembeni yake ni Sister Immaculata Tegete (Mtanzania)
ahaaa kumbe tunapinda mgongo hivi hahahaha ilikuwa burudani tosha
 Mdundo wa ngoma unaponoga, lazima ufumbe macho, ni Bw. Marcues akiongezea  maraha kwenye  nyimbo ya Ntuya Mayenje
 Palichimbika,  Bwana huyo alishindwa kabisa kujizuia, mmarekani mweusi, lakini wote asili yetu moja akaamua kujimwaya uwanjani kulisakata Ntuya Mayenje
Watanzania waliokuja kuwaunga mkono  Masista wa MaryKnoll katika kuadhimisha  miaka 100 ya kuanzishwa kwa shirika lao.

Saturday, October 27, 2012

Mustafa Hassanali launches AFRILAAL in South Africa

 Pan African Designer from Tanzania, Mustafa Hassanali showcased at the 4TH Edition of The Africa fashion International’s Africa Fashion Week 2012 in Johannesburg, on 26 October.
   “As the only designer based from Tanzania to be invited at this prestigious Fashion Week in The continent of Africa, I am very excited and honoured to launch my new collection called afrilaal, the fifth one this year 2012 stated Mustafa Hassanali .
This Collection is named Afrilaal Collection which consists of Mustafa Hassanali |signature Gown but also some pieces of ready to wear men’s wear. “Afri” a short from of Africa and “Laal” Hindi for Colour red summates however vast and varied Africa is but the Colour of blood flowing through our veins is same. 
This collection in addition will be used to advocate awareness of the reality of HIV/AIDS, thus SEE RED, THINK HIV/AIDS. The collection has been launched at an opportune moment just as we nearing December 1, which is globally known as World Aids Day. 
 Amidst the international models who showcased mustafa Hassanali Afrilaal collection was New York based Tanzanian Model Flaviana Matata, Sweden Based Tanzanian Model Michelle Jeng and mnet face of Africa 2008 Kate mensah from Ghana amongst the many. Mustafa Hassanali has already launched 3 Collection in 2012.Afrikalos collection in Lagos Nigeria, Wedding collection in Dar es Salaam, Ramadhan Collection in Dakar, Senegal and Pink Desert Collection in Gaborone, Botswana. And has shown at Fashion extravaganza in Kampala, Uganda and Bangalore fashion week in India.
 South African Supermodel Cindy showcasing a mustafa hAssanali.
 Sweden Based Tanzanian Model Michelle Jeng showcaing a mUstafa Hassanli Afrilaal collection
 Tanzanian Model Flaviana Matata Wearing a Mustafa Hassanali
 a model strutting a mustafa hassanali afrilaal collection
Mustafa takes the  finale bow during afrilaal
 mnet face of africa 2008 winner kate mensah from ghana
model finale during afrilaal
 Afrilaal menswear by mustafa hassanali
 Afrilaal menswear by mustafa hassanali
 Afrilaal menswear by mustafa hassanali
Afrilaal menswear by mustafa hassanali 

ABOUT MUSTAFA HASSANALI 
 Pan African designer, Mustafa Hassanali pursues fashion as a religion. Being Tanzania’s premier and most celebrated wedding and evening gown designer, with an A-list clientele, Hassanali is considered a fashion guru in the region. Mustafa Hassanali, who having showcased in 16 Countries Globally in 25 Cities and also named One of Africa’s Top Male Fashion designer by UK’s NEW AFRICAN WOMAN, was also selected by the minister of youth information, Culture and Sports as a steering committee member for the selection of Tanzania National attire. Mustafa Hassanali thus is truly a fashionista personified! For more information kindly visit www.mustafahassanali.net