Sunday, July 31, 2016

RAIS DKT. MAGUFULI AFANYA MKUTANO TINDE, ISAKA NA KAHAMA MKOANI SHINYANGA

Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia wa wakazi wa Kahama mara baada ya kuwasili akitokea Nzega mkoa Tabora.
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akicheza jukwaani wimbo wa kwaya ya Haleluya Kuu kutoka Kanisa la KKKT- Usharika wa Yeru Ndala Shinyanga kabla ya Kuhutubia mamia ya wakazi Kahama mkoani Shinyanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mbunge wa zamani wa Kahama James Lembeli mara baada ya kuwasalimia wananchi waliofika kwa ajili ya kumsikiliza Rais katika viwanja hivyo vya Kahama.
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia wa wakazi wa Isaka mkoani Shinyanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameambatana na Mbunge wa zamani wa Kahama James Lembeli ambaye ni mwanachama wa Chadema mara baada ya kumaliza kuhutubia mkutano mjini Kahama mkoani Shinyanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akicheza pamoja na Wanakwaya wa Haleluya Kuu kutoka Kanisa la KKKT- Usharika wa Yeru Ndala Shinyanga mara baada ya kumaliza kuhutubia mkutano Kahama mjini mkoani Shinyanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia mara baada ya kuoneshwa picha na kijana mmoja aliyeishika picha hiyo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wakazi wa Tinde mkoani Sinyanga. PICHA NA IKULU

DC IKUNGI AMTAKA DED WAKE KUMPA TAARIFA YA KUTOANZA UJENZI WA NYUMBA ZA WALIMU ZINAZOGHARAMIWA NA BENKI YA DUNIA

Mkuu wa wilaya ya Ikungi, Miraji Mtaturu akiwapungia mkono wananchi waliohudhuria kwenye uzinduzi wa uchagiaji wa damu salama,mfuko wa afya ya jamii(CHF) pamoja na daftari la ufuatiliaji akina mama wajawazito uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Minyughe,wilayani Ikungi.
Mkuu wa wilaya ya Ikungi,Mkoani Singida,Miraji Mtaturu(wa kwanza kushoto) akimkabidhi Mbunge wa jimbo la Singida Magharibi(CCM), Elibariki Kingu daftari la ufuatiliaji akina mama wajawazito,mara baada ya kuzindua mpango huo uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Minyughe,wilayani hapa.
Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Minyughe waliohudhuria uzinduzi wa uchangiaji wa damu salama lililofanyika kiwilaya katika kata ya Minyughe,tarafa ya Ihanja,wilaya ya Ikungi.
Mmoja wa wataalamu wa kitengo cha kukusanya damu salama akiwa katika jingo la darasa moja la shule ya msingi Minyughe,tarafa ya Ihanja wakati wa uzinduzi wa uchangiaji wa damu salama,mfuko wa afya ya jamii(CHF) na daftari la ufuatliji wajawazito kuhudhuria kliniki akikusanya chupa za damu zilizotolewa na wanafunzi wa shule ya sekondari ya kata aya Minyughe. (Picha Na Jumbe Ismailly).

Na. Jumbe Ismailly, Ikungi 


MKUU wa Wilaya ya Ikungi,Mkoani Singida amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya hiyo kuwa ifikapo Agosti mwaka huu ampatie taarifa za sababu zilizochangia Mkandarasi aliyepewa kazi ya ujenzi wa nyumba sita za shule ya msingi Minyughe kutoanza kazi kwa wakati uliopangwa ya ujenzi wa nyumba sita za walimu wa shule ya msingi Minyughe licha ya kupokea malipo ya kazi hiyo.

Mkuu huyo wa wilaya, Miraji Mtaturu alitoa agizo hilo katika Kijiji cha Minyughe, muda mfupi baada ya uzinduzi wa uchangiaji wa damu salama, mfuko wa afya ya jamii (CHF) pamoja na daftari la ufuatiliaji akina mama wajawazito uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Minyughe,wilayani Ikungi.

Kwa mujibu wa Mtaturu kuchelewa kuanza kwa shughuli ya ujenzi huo wa nyumba za walimu utasababisha pia ukamilishaji wa nyumba hizo kutokamilika pia kwa wakati na huduma kwa walimu kucheleweshwa.

Akitoa taarifa kwa Mkuu huyo wa wilaya juu ya Mkandarasi kutoanza kazi za ujenzi wa nyumba hizo licha ya kupokea fedha za malipo ya shughuli hiyo, Mbunge wa jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu alisema miradi inayofadhiliwa na Benki ya dunia yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 750 katika Halmashauri hiyo imekwamishwa na Mkandarasi licha ya kulipwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo za walimu, jambo linalosababisha walimu wa shule hizo kuishi katika nyumba zisizo na ubora unaotakiwa.

Hata hivyo Mbunge huyo kijana aliweka bayana kwamba baada ya kuonekana kila Mkandarasi anayetenda anatoa bei ya juu, yeye alimshawishi Waziri wa Tamisemi ili aweze kuiruhusu Halmashauri ifanye taratibu za manunuzi yenyewe ili kufanikisha shughuli hiyo iweze kufanyika mapema badala ya kuendelea kutegemea utaratibu wa wizara ambao unatumia fedha nyingi huku kukiwa na mwanya wa fedha za serikali kuliwa na baadhi ya watendaji wasiokuwa waaminifu.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo,Athumani Salumu akitoa utetezi wa sababu za kutoanza kwa shughuli hizo za ujenzi ni pamoja na ukosefu wa mchanga wa kuanzisha ujenzi wa nyumba hizo.

MWILI WA MAREHEMU JOSEPH SENGA WAANGWA LEO JIJINI DAR

 Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Joseph Senga liwa katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri jijini Dar es salaam wakati wakiamuaga kwenda Kwimba, Mwanza kwa Maziko. Mwili wa Marehemu Joseph Senga unatarajiwa kuzikwa mara baada ya kufika. 
 Jeneza la Mwili wa Joseph Senga likipewa heshima ya mwisho.
 Wanahabari waliofika kumuaga mwenzao.
 Mpiga Picha Mkuu wa Kampuni ya The Guardiun, Suleiman Mpochi akitoa salamu za rambirambi.
 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akiteta jambo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye wakati wakiwa kwenye shughuli ya kuaga Mwili wa Aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, Marehemu Joseph Senga, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam leo.
 Mhariri Mtendaji wa Gazeti ya Tanzania Daima, Neville Meena akizungumza.
 Familia ya Marehemu Joseph Senga ikiwa ni yenye huzuni kubwa kuondokewa na Mpendwa wao.
 Mbunge wa Jimbo la Kibamba, John Mnyika akitoa salamu za Rambirambi.
 Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Said Kubenea akizungumza.
 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe akizungumza.


  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akitoa salamu.
 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Anastazia Wambura akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.







 Baadhi ya Wapiga Picha wa Vyombo mbalimbali vya Habari nchini, wakibeba Jeneza la Marehemu Joseph Senga wakati wakilipeleka kwenye gari tayari kwa safari ya kwenda Kwimba, Jijini Mwanza kwa Mazishi.