Monday, December 2, 2013

WAANDISHI WA HABARI ZA MAZINGIRA WAPEWA MWANGA YALIYOJIRI MKUTANO WA MABADILIKO YA TABIANCHI (COP 19)

DSC_0226
Afisa Habari kutoka Kitengo cha Habari Umoja wa Mataifa(UNIC), Usia Nkhoma Ledama akizungumza leo jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari katika hoteli ya Holiday Inn juu ya changamoto na mafanikio ya mkutano wa mwisho wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP 19) na msimamo wa Tanzania na Bara la Afrika kwa ujumla juu ya masuala ya Tabianchi na Mazingira duniani. Kutoka kulia ni Mtaalamu wa mambo ya Nishati na Mabadiliko ya Tabianchi kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Bw. Abbas Kitogo, Mwakilishi kutoka Youth of United Nations Association (YUNA) Adam Anthony na mgeni rasmi Naibu Mkurugenzi Msaidizi wa kitengo cha Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi.
DSC_0305
Naibu Mkurugenzi Msaidizi wa kitengo cha Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi akizungumza na waandishi wa habari juu ya mkutano wa mabadiliko ya Tabianchi (COP 19) amesema kuna ugumu na umuhimu wa mkutano wa mabadiliko ya Tabianchi, na kuongeza kuwa wamekubaliana wawe na mkataba kwa nchi wanachama jinsi ya kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa kwa kiwango ambacho hakitaongeza Madini Joto duniani
Muyungi alisisitiza kwamba kuna umuhimu wa wanachama kukubaliana kwa maandishi na kuandika mkataba vile vile amesema walikubaliana kutokufuta mkataba mama wa 1992, na umuhimu wa kupunguza Gesi Joto na kuangalia uchangiaji wa tatizo la Madini Joto katika duniani.
DSC_0294
Mtaalamu wa mambo ya Nishati na Mabadiliko ya Tabianchi kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Bw. Abbas Kitogo, akizungumzia masuala ya mipango ya serikali kuhusu mabadiliko ya Tabianchi kupewa kipaumbele katika mipango ya serikali kwa maendeleo ya Taifa kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, alisisitiza kwamba UNDP ina nafasi ya kusaidia kuleta maendeleo kwa Taifa kwa kuweka mipango ya maendeleo yenye kuendana na mabadiliko ya Tabianchi.
DSC_0248
Mwakilishi kutoka Youth of United Nations Association (YUNA) Adam Anthony akizungumzia juu ya umuhimu wa kuwashirikisha vijana katika masuala ya Tabianchi na amesema waliafikiana kutengeneza (Task Force Team) ambayo itakuwa na kazi ya kufuatilia mapendekezo na maadhimisho ya mkutano kwa maslahi mapana ya duniani inayowakilisha vijana, vile vile kupata nafasi ya kukaa na vijana wa nchi zingine juu ya matatizo yanayotokana na mabadiliko ya Tabianchi kwenye mazingira, Kilimo na Sekta za Utalii na uhifadhi na Nishati na umuhimu wa vijana kushiriki kikamilifu katika masuala ya kuelimishana mambo ya Tabianchi.
Bw. Anthony amefafanua kuwa baada ya mkutano wa COP 19 uliofanyika Warsaw Poland, hivi karibuni kujipanga kwa vijana na vyombo vya habari katika na mkutano unaokuja wa 2015 wa mabadiliko ya Tabianchi.
DSC_0302
Fazal Issa kutoka Mtandao wa Asasi Zisizo za Kiserikali zinazofanya shughuli zake katika Masuala ya Mabadiliko ya Tabianchi akizungumza kwa undani matokeo ya mabadiliko ya Tabianchi kwa nchi masikini na jinsi zinavyoweza kurudisha nyuma maendelo ya sehemu husika.
DSC_0255
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano wa kufafanua yaliojiri katiak mkutano wa Warsaw, Poland wa Mabadiliko ya Tabianchi.

HOYCE TEMU ALAMBA NONDOZZZ YA SHAHADA YA UZAMILI WA MAWASILIANO YA UMMA ST. AUGUSTINE UNIVERSITY

Picture 019
Aliyekuwa Miss Tanzania 1999, ambaye pia ni Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu akipozi mara baada ya kulamba Nondozzz ya shahada ya Uzamili wa Mawasiliano ya Umma katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine jijini Mwanza.
Picture 018
Hoyce Temu akipata Ukodak na Mdau wa tasnia ya habari nchini.
Picture 013
Hoyce Temu katika pozi na marafiki zake mara baada ya kulamba Nondozz.
Picture 026
Pongezi pia ziende kwa Dada Lulu Musa Afisa Uhusiano wa Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira kwa kulamba Nondozz ya shahada ya Uzamili wa Mawasiliano ya Umma katika chuo cha St. Augustine University kwenye mahafali ya 15 ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Mwanza mwishoni mwa Juma.
Picture 045
Mbali na kula Nondozz kwenye siku hiyo maalum Hoyce Temu ambaye pia ni Mtangazaji wa Kipindi cha Mimi na Tanzania aliamua kufanya mahojiano na baadhi ya wahitimu kwa ajili ya kipindi chake.
Picture 055
Mlimbwende Hoyce Temu akizungumza na mwandishi wa habari wa ITV kuhusiana na taalum aliyoipata itakavyoweza kuboresha utendaji wake kazini pamoja na kuendelea kuisaidia jamii inayomzunguka kupitia kipindi chake cha Mimi na Tanzania.
Picture 070
Mwanandishi wa habari wa kituo cha ITV Shaban Tole akimpongeza Hoyce Temu.
Picture 078
Hoyce Temu katika picha ya kumbukumbu na marafiki.
Picture 071
Hoyce Temu akiondoka eneo la tukio na furaha isiyo na kifani.

MAMIA WAFURIKA KUSHUHUDIA BONANZA LA WAZI LA MASUMBWI NDANI YA KITUO CHA MABASI CHA MWENGE



 Mpambano wa kwanza kati ya Gervas Rogiansion aliyevaa gloves nyekundu akipambana vikali na mpinzani wake John Christian aliyevaa Gloves za rangi ya bluu , ambapo John Christian aliibuka mshindi kwa Makonde mawili kwa moja.
 Umati wa watu waliojitokeza kutazama Bonanza la wazi la Ngumi katika kituo cha mabasi cha Mwenge
 Mashabiki wa Ndondi wakishangilia
 Mpambano wa pili  kati ya Haruna Swanga  aliyevaa gloves nyekundu aliyepambana vikali na na mpinzani wake Kulwa Makenzi  aliyevaa Gloves za rangi ya bluu , ambapo Haruna Swanga aliibuka mshindi kwa kumtandika mpinzani wake makonde matatu kwa sifuli.

 Mpambano wa tatu  kati ya George Costantino   aliyevaa gloves nyekundu aliyepambana vikali na na mpinzani wake Hamadi Furahisha   aliyevaa Gloves za rangi ya bluu , ambapo Hamadi Furahisha  aliibuka mshindi kwa kumtandika mpinzani wake makonde mawili kwa moja.
 Leonard Machichi aliyevaa gloves nyekundu akiwa anajikimu kukwepa ngumi kutoka kwa mpinzani wake Abuu Bakari wakati wa mpambano huo
 Abuu Bakari akipokea kipigo cha nguvu kutoka kwa mpinzani wake Leonard .. ambapo hali ilikuwa mbaya sana kwa Abuu
 Mwamuzi wa Mpambano huo Michael Mwamkenja akisimamisha mpambano huo katika Mzunguko wa pili baada ya Bondia Abuu kunyosha mikono juu ishara ya kushindwa .
 Leonard Machichi akitangazwa mshindi wa pambano hilo kali ambalo wanaliita RDT
 Makamu wa Raisi mpya wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania Lukelo Anderson au Man Power akiwa anatoa Neno la Shukurani Mara baada ya mpambano huo kuisha.
 Kutoka Kushoto ni Bi. Zuena Kipingu ambaye ni Mjumbe wa Maendeleo ya Vijana na wachezaji katika Shirikisho la ngumi za Ridhaa Tanzania,Mutayoba Rwakatale Katibu wa maandalizi hayo, na Bondia Haruna Swanga. 

 Hawa ni wazee wa zamani ambao sasa ni walimu wa mchezo wa Ngumi, Wakati wao ndio walikuwa Mabondia Wakubwa
Wapigangoma wa Kikundi cha Ngoma ya Mchiriku cha Jagwa wakitumbuiza katika Bonanza la Masumbwi
 Mwimbaji wa Kundi la Jagwa akitumbuiza vilivyo katika Bonanza hilo la Masumbwi.
 Afisa habari wa Shirikisho la Ngumi Tanzania Salim Mwiduka akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa Bonanza la wazi la ngumi.
 Mwenyeji wa Maandalizi ya Bonanza la Ngumi Kessy Juma akiwa anafungua Bonanza hilo.
 Mwenyekiti wa kamati ya Tuzo za ngumi Said Masanga akielezea juu ya Tuzo hizo za ngumi.
 Mjumbe wa Shirikisho la Ngumi wanawake Bi. Aisha George Vaniatis akiwa anafuatilia mpambano

Kulia ni Mwalimu mkongwe wa Mchezo wa ngumi bwana Rashid au anafahamika kwa jina la 
Super D.
Picha zote na Dar es salaam yetu.

SAUDI PRINCESS VISIT SERENGETI NATIONAL PARK

Public Relations Manager of TANAPA Mr. Pascal Shelutete (second left) welcomes Princess Haifa Bint AbdulAzizi al Mogrin (in a white blouse) and her delegation soon after landing at Seronera airstrip in Serengeti National Park. Looking on (left) is Chief Park Warden of Serengeti National Park Mr. William Mwakilema.
Saudi Arabian Ambassador to Tanzania H.E. Hani Mominah (black cap) talking to Chief Park Warden of Serengeti National Park Mr. William Mwakilema. Far left is Dr. Robert Fumagwa who is the Head of Tanzania Wildlife Research Institute Centre in Serengeti.
Princess Haifa Bint AbdulAzizi al Mogrin admiring a Hyrax at Serengeti Visitors Information Centre.
What a wonderful hyrax…the delegation seems to ask while taking pictures.
Chief Park Warden of Serengeti National Park Mr. William Mwakilema taking Princess Haifa through the trails of the Visitors Information Centre.
Princess Haifa enjoying the trail walks.
Princess Haifa signing a visitor’s book at the tourist information centre.
A lion heading towards the princess convoy.
Full inspiration by the amazing scenery of Serengeti.
After crossing in the middle of the convoy, this lion went ahead to quench her thirst.
Princess Haifa admiring a “Discovery Centre” at Four Seasons Safari Lodge in the Serengeti National Park.

RC BENDERA NA NAIBU WAZIRI MEDEYE WATUNUKIWA PHD YA HESHIMA

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ( kushoto) akipongezwa na Makamu wa Rais na Mkurugenzi wa Mahusiano wa Masuala yote ya Afrika ya Kielimu ambaye pia ni Kamishina wa Tume ya Haki za Binadamu yenye kutetea matatizo ya Haki za Binadamu Kimataifa , Profesa Edward Lazaro Nasioki, ( kulia) mara baada ya kumtunukisha Shahada ya Uzamivu ya Heshima ( PhD) katika Masuala ya Falsafa ya Jamii ya Chuo Kikuu cha Califonia State Christian kilichopo nchini Marekani, kwa mamlaka aliyopewa na Bodi cha Chuo Kikuu hicho.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera akivishwa kofia ya udaktari wa Heshima .
Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Dk Joel Goodluck Ole Medeye ( kushoto) akipongezwa na Makamu wa Rais na Mkurugenzi wa Mahusiano wa Masuala yote ya Afrika ya Kielimu ambaye pia ni Kamishina wa Tume ya Haki za Binadamu yenye kutetea matatizo ya Haki za Binadamu Kimataifa , Profesa Edward Lazaro Nasioki, ( kulia).kati kati kati ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro, Innocent Kalongeris.
Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Joel Goodluck Ole Medeye ( kushoto) , na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ( kulia ) wakiwa katika picha ya pamoja na na Makamu wa Rais na Mkurugenzi wa Mahusiano wa Masuala yote ya Afrika ya Kielimu ambaye pia ni Kamishina wa Tume ya Haki za Binadamu yenye kutetea matatizo ya Haki za Binadamu Kimataifa , Profesa Edward Lazaro Nasioki, wa Chuo Kikuu cha Califonia State Christian kilichopo nchini Marekani, baada ya kuwatunukishaShahada ya Uzamivu ya Heshima ( PhD) katika Masuala ya Falsafa ya Jamii ,Novemba 30, mwaka huu kutokana na mamlaka aliyopewa na Bodi cha Chuo Kikuu hicho.Picha na John Nditi, Morogoro

Na John Nditi, Morogoro

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera , na Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Joel Goodluck Ole Madeye , wametunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Heshima katika Masuala ya Falsafa ya Jamii ya Chuo Kikuu cha Califonia State Christian kilichopo  nchini Marekani.

Bendera na Medeye walitunukishwa PhD zao ,Novemba  30, mwaka huu  na Makamu wa Rais na Mkurugenzi wa Mahusiano wa Masuala  yote ya  Afrika ya Kielimu ambaye pia ni Kamishina wa Tume ya Haki za Binadamu yenye kutetea matatizo ya Haki  za Binadamu Kimataifa , Profesa Edward Lazaro Nasioki, kwa mujibu wa  mamlaka aliyopewa na Bodi cha Chuo Kikuu hicho.

Kabla ya kuwatunukisha , Profesa Nasioki , alisema moja ya kazi za Vyuo Vikuu Duniani ni kwenda katika jamii kutafuta watu walionasifa mbalimbali , waliobuni na kuchangia maendeleo ya aina mbalimbali katika jamii.

Alisema , PhD hutolewa hasa kwa watu wale waliotumia muda wao kwa miaka mingi kusoma , kufanya utafiti wa mambo mbalimbali katika jamii au kiroho na kupendekeza au kushauri juu ya njia za kuleta mabadiliko yenye manufaa kwa jamii na hao wanatambuliwa kama wataalamu mbalimbali wahusika.

Hivyo alisema , Shahada ya heshima hutolewa hasa kwa wale watu ambao wamatumikia muda na rasilimali zao kubuni na kuchangia michango ili kutatua matatizo yanayoikumba jamii ,hivyo Chuo hicho kimetambua juhudi , elimu , maisha , tabia , utendaji na mchango wa Bendera na Medeye katika jamii ya Tanzania .

“ Tuko hapa leo , Nov emba 30 , mwaka huu kwa ajili ya kutunuku shahada ya heshima kutokana na historiana mchango wenu kwa jamii ya Watanzania” alisema Profesa Nasioki ambaye ni Mtanzania mbele ya wageni waalikwa walihudhuria hafla hiyo katika viwanja vya Ikulu Ndogo ya Mkoani Morogoro.

Kwa mujibu wa Makamu wa Rais wa Chuo hicho,Watanzania 117 wamepata shahada za aina mbalimbali kutoka Vyuo vya Marekani , Canada na Korea , kati ya hao watatu wamepata shahada za heshima na tisa shahada za uzamili.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Bendera, akizungumza baada ya kutunukiwa PhD, aliishukuru Bodi ya Chuo Kikuu hicho kwa  kutambua mchango wake katika taifa na kuweza kumtunukia Udaktari wa Heshima.

 Hivyo alisema  , kupata PhD ni chachu na changamoto kwake  ya kuwatetea mabadiriko ya kimaendeleo mara mbili zaidi ya utendaji kazi kwa Watanzania wakiwemo na  wananchi wa Mkoa huo.

“ Mtu asifirikie kutunukiwa PhD sasa nitakweteka la hasha , hii ni changamoto na kipimo kingine cha kuendeleza kazi ya maendeleo ya wananchi kwa kushirikiana na watendaji wengine wa Wilaya na mkoa “ alisema Dk Bendera.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Medeye ,alisema , Chuo Kikuu hicho kimetambua uwezo wao na sifa zao , hivyo  kazi iliyopo mbele ndani ya  Wizara kwa kushirikiana na watendaji wengine ni kujituma kwa bidii na utendaji unaozintatia haki ,taratibu na sheria.