Monday, May 9, 2011

MAMLAKA YA USIMAMAMIZI WA BIMA NCHINI (TANZANIA INSURANCE REGULATORY AUTHORITY) YAFUNGUA OFISI KANDA YA KASKAZINI.

Kamishna wa Bima Tanzania Bw. Israel Kamuzora akiongea na wafanyabiashara ya bima , ikiwa ni pamoja na mameneja na maofisa mwaandamizi wa makampun imbalimbali ya bima,mkoani Arusha ambapo alisisitiza umuhimu wa kufanyakazi kwa kufuata sheria,kanuni na taratibu zilizowekwa na nchi. Kamishna alisisitiza zaidi juu ya umuhimu wa kutoa huduma bora kwa wateja wa bima nchini.
Mkutano ukiendelea
Baadhi ya waliohudhuria
wana Bima wa Arusha
Wana Bima wa Arusha mkutanoni
Mkutano ukiendelea
Maofisa wa kanda
Wadau wa Bima
Mkutano
WafanyakaziwamamlakayaBimanchinikandayakaskazini kutoka kushoto ni Bw. Soud Sadique, Sigfrida Zacharia, Stella Rutaguza na DerickOwawa

Picha ya pamoja baada ya mkutano

mazishi ya mama mzazi wa Spika Anne Makinda leo

Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda na Mama Tunu Pinda wakiweka shada la maua kwenye kaburi la Mama Mzazi wa Spika Anne Makinda leo

Rais Jakaya Kikwete akiweka mchanga kaburini
Mama Salma Kikwete akiweka mchanga kaburini
Rais Jakaya Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiomba dua kaburini kwa Mama Mzazi wa Spika Anne Makinda
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda na Mama Tunu
Pinda wakiweka mchanga kaburini
Katibu Mkuu wa CCM Mh. Wilson Mkama
Mh. William Lukuvi


Mwenyekiti wa CHADEMA na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni Mh. Freeman Mbowe akitoa heshima zake
Mh. Freeman Mbowe akiweka shada la maua kaburini
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda na Mama Tunu Pinda wakiweka shada la maua kaburini
Sehemu ya umati mkubwa wa wananchi mazishini


Mwakilishi wa mgodi wa Barick Deo
Mwanyika akiweka shada la maua

Kaburi la Mama mzazi wa Makinda
Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter
Msigwa akiweka shada la maua. Picha zote na Francis Godwin

Sunday, May 8, 2011

Mkutano wa Diaspora III wamalizika

Kutoka kushoto Mh. Ibrahim Sanya (Mbunge - CUF) ,Mh. Vicky Kamata (Mbunge - CCM), na Balozi wa Tanzania - UK,Mh. Peter Kallaghe wakifuatilia mkutano hupo.
Balozi wa Tanzania - UK,Mh. Peter Kallaghe akifunga Mkutano wa tatu wa Diaspora III uliokuwa ukifanyika huko nchini Uingereza.
Bw. Salum Shamte Kutoka kilimo kwanza akizungumza katika mkutano huo.
Bi. Rehema Chuma akizungumza katika mkutano wa Diaspora III.
Hassan Katibu wa Zawa akichangia mada mkutanoni hapo.
Mdau Abu Faraji kutoka Swift Freight akizungumza.
Bw. Aron Luanga toka benki ya CBA akifanya majadiliano na moja ya vyombo vya habari vilivyohudhulia mkutano huo.
Bw. Ally Kondo ambaye ni afisa Mawasiliani Wizara ya Mambo ya Nje akifanya majadiliano.
Bw. Daniel Mrutu wa Kilimo Kwanza akiwa mkutanoni.
Oparesheni Meneja wa NSSF Mr Magore nae alikuwepo pia.
Dada Patricia toka TIC.
Jopo la wataalam wakijipanga kabla ya mkutano.
kutoka kushoto Frank,Baraka, Asha Baraka, Salum Shamte na Mariam mara baada ya mkutano kumalizika.
Balozi akiwa na ugeni kutoka PPF.

Saturday, May 7, 2011

Pre-wedding party ya Angela Mwiki ukumbi wa Mwika, Dar

Angela (shoto) akiwa na mpambe wake
Angela akimchoropoa mtarajiwa mezani pake
Malavidavi kwa kwenda mbele
MC akiwatambulisha watarajiwa
I-ringi kama kawa
Angela na wazazi wake na mpambe
Baba anatoa ng'ombe wa maziwa
Angela na mpambe wake wakipozi na wazaai
Angela na mpambe wake wakiwa na mama mkwe
Angela na kamati ya maandalizi wakila twisti
Angela na kaka, dada, wadogo na wifie
Mwenyekiti wa kamati (kulia) na wanakamati
wanakamati
Wadau

Orodha kamili ya wanamichezo bora wa 2010

Riadha
1. Wanaume: Marco Joseph- Alishika nafasi ya nne katika mbio za meta 10,000 michuano ya Jumuiya ya Madola New Delhi, India.

2.Wanawake: Mary Naali –Alikuwa Mtanzania pekee aliyefuzu mashindano ya dunia ya junior yaliyofanyika Canada na kuwa katika kumi bora.
-Alishiriki Safari International Half Marathon-Arusha na kushika nafasi ya pili
-Alishiriki Wachau Int Half Marathon Austria na kuwa wa kwanza akiweka rekodi yake mpya na nzuri zaidi kwa mwaka wote wa 2010 ya saa 1:12:16.
WAVU
1: Wanaume: Kevin Peter
-Ni mchezaji wa Magereza Wanaume. Aliipa ubingwa wa Muungano timu ya Magereza mwaka 2010
-Alikuwa mchezaji nyota wa michuano hiyo.
-Alichangia ubingwa wa vyuo timu yake ya IFM alikokuwa akisoma.
-Alichanguliwa Mchezaji Bora (MVP) wa Kombaini ya Afrika Mashariki na Kati akiwa pia ni kocha kitaaluma wa mchezo mwenye cheti cha ukocha Level 1.

2: Wanawake: Hellen Richard Mwegoha (Magereza Wanawake).
Ni nahodha wa Magereza aliyewaongoza wenzake kutwaa mfululizo ubingwa wa Tanzania Bara.
-Aling’ara katika mashindano ya wavu Bara na Muungano mwaka jana.
-Pia ni nahodha wa timu ya taifa.
Netiboli
Mwanaid Hassan (JKT Mbweni)
-Aliiwezesha timu yake ya JKT Mbweni kuibuka bingwa ligi daraja la kwanza 2010
-Aliibuka mfungaji bora katika michezo ya ligi daraja la kwanza 2010
-Aliiwezesha timu ya Mkoa wa Temeke kuibuka bingwa wa Taifa Cup 2010
-Aliibuka mfungaji bora wa michuano ya Taifa Cup 2010
-Aling’ara katika mashindano ya Singapore mwaka 2010 akiwa ni mmoja kati ya wafungaji bora
-Alikuwa Mfungaji Bora katika mashindano ya nchi za Afrika yaliyofanyika Afrika Kusini mwaka 2010

Kikapu
1:Wanaume: George Otto Tarimo (Savio-DSM)
Mashindano aliyocheza: RBA, NBL, Muungano, Majiji ya Afrika Mashariki, Klabu Bingwa Kanda ya Tano

Mafanikio: Mzuiaji Bora Majiji ya A/Mashariki, Amesaidia timu yake kutwaa ubingwa wa vikombe vitatu na kuwa Mchezaji Bora RBA, NBL na Muungano.

1. Wanawake : Faraja Malaki (Jeshi Stars DSM).

Mashindano: RBA, NBL, Majiji ya A/Mashariki, Klabu Bingwa Kanda ya Tano
Mafanikio:
Mchezaji Bora wa Ligi ya RBA na ameisaidia timu yake kuwa bingwa wa RBA.
Amecheza NBL kwa kiwango cha juu na kuisaidia timu yake kuwa Mabingwa na Mchezaji Bora.
Pia ameisaida timu yake kutwaa kombe la Muungano na kuwa mchezaji bora

SOKA
Wanaume: 1: Shadrack Nsajigwa-Yanga
--Aliisaidia timu ya Yanga kushika nafasi ya pili Ligi Kuu 2009/2010
--Aliisaidia timu ya Taifa ya Tanzania Bara kutwaa Kombe la Chalenji baada ya kulikosa kwa miaka 16.
-Bao lake la penalti mchezo wa fainali kati ya Tanzania Bara na Ivory Coast ndilo lililoipa ubingwaTanzania Bara.
-Alionesha uwezo mkubwa katika michuano ya Chalenji –Alikuwa Mchezaji Bora wa Mashindano ya Chalenji.

2: Wanawake: Asha Rashid
-Alitoa mchango mkubwa kufanikisha Twiga Stars ifuzu fainali za Afrika kwa wanawake
1. Ngumi za kulipwa: Karama Nyilawila
We have picked Karama Nyilawila as our professional boxer for the year 2010, thus qualify to contest for the best sports personality of the year award 2010.

The pugilist is the World Middleweight title holder recognized by World Boxing Federation (WBF). He won the title in Prague, Czech Republic on 3rd day of December 2010 against Albanian Kreshnik Qato on points.


8: Ngumi za ridhaa: .Selemani Kidunda
-Alipata medali ya shaba katika mashindano ya tano ya ngumi ya Jumuiya ya Madola New Delhi, India.
-Alipata medali ya dhahabu katika mashindano ya Taifa ya klabu bingwa ya Taifa Julai 2010
-Alipata medali ya dhahabu katika mashindano ya Taifa ya bingwa wa mabingwa
-Alishiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola New Delhi, India hakupata medali.

9: Baiskeli
Wanaume: Hamis Clement:
-Alikuwa mshindi wa kwanza mashindano makuu ya riadha ya Vodacom 2010 Kilometa 190 yaliyofanyika Mwanza
2: Wanawake:
1:Sophia Anderson-Alikuwa mshindi wa kwanza mashindano makuu ya riadha ya Vodacom 2010 Kilometa 80 yaliyofanyika Mwanza

10:Kriketi
Wanaume: Kassim Nassor
-Helped Tanzania finish fourth in the last year’s ICC World League Division 4 in Italy
-Won Man of the Match award in the ICC World League Division 4 match against Cayman Island
-Led his club, Academy Boys, to win the last year’s Mwalimu Nyerere Memorial Cup tournament
-Helped his team, Twiga Warriors, emerge champions of this year’s Advanced Players League (APL)
-Won the best all rounder award in this year’s APL
Wanawake: Mariam Said
-Helped the national U-19 women cricket team reach the final of the last year’s East Africa U-19 women championship played in Dar es Salaam
-Was the second best all rounder in the last year’s East Africa U-19 women championship played in Dar es Salaam
-Helped Zanaki Secondary School cricket team emerge champions of the TCA Schools league last year.

11: MWANAMICHEZO BORA CHIPUKIZI
Lilian Sylidion-Filbert Bayi
-Aling’ara katika mashindano yaliyofanyika Singapore, ambapo Taifa Queens ilishika nafasi ya tatu kuwania kufuzu michezo ya dunia.
-Aliibuka Mchezaji Bora wa mashindano hayo ya kimataifa ya Singapore.
-Ni mchezaji wa timu ya Filbert Bayi ya mkoani Pwani.

12: MWANAMICHEZO BORA WA NJE ANAYECHEZA TANZANIA
Emmanuel Okwi: Ametoa mchango mkubwa kwa Simba kutwaa ubingwa 200/2010
-Aling’ara mwaka 2010 akichezea Simba michezo mbalimbali.

13:MWANAMICHEZO BORA WA TANZANIA ALIYEPO NJE
Hasheem Thabeet: Amekuwa mstari wa mbele kwa kushiriki katika shughuli za kijamii amechangia ujenzi wa shule za sekondari mkoa wa Pwani kama shule ya Hanasif, Mkuraga.

Amekuwa Balozi wetu nchi za nje ameshiriki katika mipango mbalimbali ya kusaidia huduma za afya na elimu kwa kushirikina na wadau wengine huko Marekani kwa manufaa ya Tanzania.

Agosti mwaka 2010 aliendesha kliniki ya vijana wadogo chini ya umri wa miaka 17, karibu vijana 350 Dar es salaam na kutoa vifaa vya michezo kwa wachezaji wote hao, pia aliandesha kliniki nyingine huko Senegal kwa vijana toka bara zima la Afrika, ambapo Mtanzania Alpha Kisusi nae alishiriki.

Hasheem aliendesha mafunzo kama hayo huko China, Taiwani n.k.
Aliandaa Hasheem Thabeet Basketball Bonanza la kuhamasisha vijana kwa kucheza na timu zote za Dar es salaam, shule za sekondari Dar es Salaam na timu za mitaani kwa siku mbili

14; Judo: Masoud Amour Kombo
-Alichaguliwa Mchezaji Bora wa Judo Afrika Mashariki mwaka 2010
-Alitwaa medali mbili za dhahabu kwa kategoria mbili tofauti mashindano ya Afrika Mashariki mwaka 2010.
Amekuwa akipata medali za dhahabu na kuibuka Mchezaji Bora wa Judo kwa miaka mitatu mfululizo.
Pia alipata medali ya dhahabu katika mashindano ya wazi ya judo mwaka 2010.
Amekuwa bingwa wa judo uzani wa Kilogramu 1000 kwa mwaka 2010 na kuweka rekodi ya kutwaa ubingwa huo kwa mwaka wa nne mfululizo.

15: Gofu:
WANAWAKE
1. Hawa Wanyeche- Ni mchezaji kutoka Klabu ya Gymkhana Dar es Salaam. Nahodha wa timu ya Taifa ya gofu ya Wanawake na mchango mkubwa kuwezesha timu ya taifa kuweka historia ya kushika nafasi ya pili kwenye michuano ya Kombe la Challenge la Gofu la Wanawake Afrika ( All African Challenge Trophy) yaliyofanyika Abuja, Nigeria Novemba, 2010 na kuipa Tanzania heshima kubwa.
Alishika nafasi ya tano kati ya zaidi ya wachezaji 150 kwenye michuano ya wanawake ya Nigerian Open dhidi ya wachezaji wakali Afrika. Alitwaa taji la mashindano ya wanawake ya Coast Open, Mombasa, Kenya Agosti na taji la Wanawake Dar Open Oktoba. Mafanikio yake katika mashindano ya ndani na nje yamemwezesha kupewa tuzo ya Mchezaji Gofu Bora wa Mwaka Mwanawake (Best Lady Golfer of the Year) na Chama cha Gofu Tanzania (TGU) mwaka jana.

WANAUME

2.Frank Roman- Mchezaji wa Klabu ya Gymkhana Moshi.
-Ni nahodha wa timu ya taifa ambaye amekuwa na mwaka mzuri katika mashindano ya ndani. Februari mwaka 2010 Moshi aliibuka bingwa wa michuano ya taifa ya gofu ya Northern Province Open na kuwashinda wachezaji nyota wa timu ya taifa ya Kenya ikiwa ni ushindi wa kwanza kwa Mtanzania mbele ya Wakenya nyumbani. Mafanikio yake kwa kipindi cha mwaka jana katika mashindano tofauti ya taifa yalimuwezesha kupewa Tuzo ya Mchezaji Gofu Bora wa Mwaka wa Kiume (Best Golfer of the Year) na Chama cha Gofu Tanzania (TGU).

16: TUZO YA HESHIMA KWENYE MICHEZO:
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa-ametoa mchango mkubwa kufanikisha ujenzi wa uwanja wa Taifa Dar es Salaam, wakati akiwa Rais.
-Uwanja huu ni sifa kubwa na kielelezo cha namna anavyowathamini wanamichezo.

17: MWANAMICHEZO BORA WA TANZANIA MWAKA 2010 NI- MCHEZA NETIBOLI MWANAID HASSAN.

WANAMICHEZO WA MIAKA ILIYOPITA
2009-MWANAID HASSAN-NETIBOLI
2008-MARY NAALI-RIADHA
2007-MARTIN SULLE-RIADHA
2006-SAMSON RAMADHAN-RIADHA.


VIGEZO:
1.Mchango wa Mchezaji husika kufanikisha ushindi kitaifa/kimataifa
2.Nidhamu Bora ya Mchezaji Ndani na Nje ya Uwanja pamoja na moyo wa kizalendo
3.Uhusiano mzuri wa Mchezaji na Jamii/Kuwa mfano wa kuigwa kimaendeleo
4.Kipaji cha pekee kwa Mchezaji
5.Mwenye mvuto, mchagizaji, mhamasishaji na mwenye ushawishi kwa jamii.

Sifa ya Ziada
1.Awe hatumii dawa zisizoruhusiwa michezoni/dawa za kulevya