Tuesday, June 12, 2018

BRAC YATOA VIFAA VYA SH MIL 69 KWA WASICHANA TANGA

 Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza kabla ya kukabidhi vifaa vyenye thamani ya ya sh Mil 69 kwa wasichana 924 kwa ajili ya kuanza shughuli za ujasirimali ili kuweza kujikwamua kiuchum ambavyo ni vyerahani na madraya ya saloon na vifaa vyengine kushoto ni Mkurungenzi Mkuu wa Brac Assan Golowa.
Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga DAS Faidha Salimu akizungumza katika halfa hiyo
Mkurungenzi Mkuu wa Brac Assan Golowa akizungumza katika halfa hiyo
PRO wa shirika la BRAC SEcilia Bosco akizungumza katika halfa hiyo
Meneja wa Miradi wa Shirika la BRAC Mkoani Tanga William Manoah akizungumza katika halfa hiyo
Afisa Elimu Msingi Jiji la Tanga Enedy Mzava ambaye pia ni Kaimu Afisa Kilimo na Mazingira akizungumzxa katika halfa hiyo
sehemu ya vyarahani vilivyotolewa
sehemu ya wasichana wanufaika na vifaa wakivitazama kabla ya kukabidhiwa
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akimkabidhi vifaa vya saloni moja wa wasichana waliopatiwa mafunzo na shirika la BRAC
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akiangalia baadhi ya vifaa v ya shuleni kabla ya kuvikabihdhi kwa wahusika 
Sehemu ya wasichana walionufaika na vifaa hivyo wakimsikiliza mgeni rasmi
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kulia akifurahia jmbo na Mkurungenzi Mkuu wa Brac Assan Golowa
mmoja wa wanufaika wa mafunzo hayo akitoa ushuhuda kwa mgeni rasmi



SHIRIKA la Brac limetoa vifaa vya kazi vyenye thamani ya sh Mil 69 kwa wasichana 924 kwa ajili ya kuanza shughuli za ujasirimali ili kuweza kujikwamua kiuchumi .

Vifaa hivyo ambavyo vimetolewa maalum kupitia mradi wake wa kuwajengea uwezo na kujiajiri wasichana ambao wameshindwa kuendelea masomo ya sekondari mkoani Tanga.Akikabidhi msaada huo Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa alisema kuwa vifaa hivyo vitaweza kuwasaidia wasichana hao kuweza kujiendeleza kiuchumi kwa kujihakikishi kipato chao.

“Serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali ili kuweza kufikia uchumi wa viwanda lakini kupitia Brac tunaona walivyofanikiwa kuwawezesha wasichana hao ili waweze kujikwamua kiuchumi”alisema DC Mwilapwa.

Kwa upande wake Mkurungenzi Mkuu wa Brac Assan Golowa alisema kuwa tayari mradi huo umefanikiwa kuwafikia wasichana 240 toka ulipoanzishwa mwaka 2016 mkoani humo.Alisema kuwa mradai huo unatoa fursa ya pili kwa wasichana walioshindwa kuendelea na masomo waweze kujifunza ujuzi wa mikono na kuweza kujiajiri ili kuweza kuwa wazalishaji mali.

“Mradi huu upo katika mikoa 23 hapa nchini lakini kwa mkoa wa Tanga umeonyesha mafanikio zaidi kutokana na muitikio mkubwa wa wasicahna kujivutika kujiunga na mradi huo”alisema Golowa.

No comments: