Saturday, January 20, 2018

UVCCM YAVUNA WANACHAMA 350 CHUO KIKUU DAR ES SALAAM


Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Kheri James amepokea jumla ya Wanachma wapya 350 katika Kongamano Maalum lililoandaliwa na Tawi la Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Kheri amewataka Vijana wanaopata nafasi za uongozi kuitumia nafasi hiyo kwa ajili ya kuwakomboa wengine na kuacha kutumika na makundi ya watu.

“Vijana wengi ambao wameaminiwa wameacha kushughulika na matatizo ya Vijana na yenye tija kwa taifa, wamekuwa wakiendeshwa na watu ambao wanamaslahi yao binafsi” amesema Kheri

Amesema kuwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imeweza kuwaamini Vijana, hivyo kila kijana wa CCM  anabudi kuwaunga mkono viongozi wote Vijana ambao wana nia ya dhati ya kutaka kulifikisha taifa hili pale linapotakiwa liwe.

Alimaliza kwa kutoa wito kwa Vijana wote kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Chaguzi ndogo zinazoendelea na kuifanya CCM ishinde kwa kishindo.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Chama Cha Mapinduzi(UVCCM),Kheri James akizungumza na Wanachama wa Umoja huo Tawi la Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam katika ukumbi wa Urafiki leo jijini Dar Es Salaam .
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Chama Cha Mapinduzi(UVCCM),Kheri James, akipokea Risala kutoka kwa Katibu wa Tawi la Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Shaka Hamdu Shaka, akisalimiana na Mmoja ya Wanachama wapya waliojiunga na Chama hicho kupitia Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Sehemu ya Wajumbe wa Uvccm kutoka Wilaya Mbalimbali wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti wa UVCCM Taifa.
Sehemu ya wanachama wapya 350 waliojiunga na Chama cha Mapinduzi Tawi la Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Wakila Kiapo cha Uaminifu.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Chama Cha Mapinduzi(UVCCM),Kheri James, akisalimiana wanachma wa CCM

No comments: