Wednesday, August 23, 2017

KIKAO CHA URATIBU WA MPANGO KAZI WA TAIFA WA KUTOKOMEZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO WAFANA

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bibi Maimuna Tarishi akifungua mkutano wa siku moja wa wadau kuchangia utekelezaji wa mkakati wa Kitaifa wa  miaka mitano wa kuzuia ukatili dhidi ya wanawake na watoto mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Anna Maembe akifafanua jambo wakati wa mkutano wa siku moja wa wadau kuchangia utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa  miaka mitano wa kuzuia ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wa kutetea haki za wanawake na watoto wakimsikiliza aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Anna Maembe wakati wa mkutano wa siku moja wa wadau kuchangia utekelezaji wa mkakati wa Kitaifa wa  miaka mitano wa kuzuia ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo Jijini Dar es Salaam.
Kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bibi. Sihaba Nkinga, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bibi. Maimuna Tarishi (katikati) na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Dkt. Zainabu Chaula, wakiendelea na mkutano wa siku moja wa wadau kuchangia utekelezaji wa mkakati wa Kitaifa wa  miaka mitano wa kuzuia ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wa kutetea haki za wanawake na watoto wakiendelea na mkutano wa siku moja wa wadau kuchangia utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa  miaka mitano wa kuzuia ukatili dhidi ya wanawake na watoto mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mipango toka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Atupele Mwambene akitoa mada wakati wa mkutano wa siku moja wa wadau kuchangia utekelezaji wa mkakati wa Kitaifa wa  miaka mitano wa kuzuia ukatili dhidi ya wanawake na watoto mapema hii leo jijini Dar es Salaam.

Picha na Eliphace Marwa - Maelezo

No comments: