Friday, December 2, 2016

WILAYA YA KAKONKO MKOANI KIGOMA HATARINI KUPOROMOKA KIUCHUMI KWA KUKOSA FURSA ZA KIUCHUMI WILAYANI KAKONKO

Na Rhoda Ezekiel Globu ya Jamii-Kigoma.

WILAYA ya Kakonko Mkoa wa Kigoma imeelezwa kuendelea kuporomoka kiuchumi kutokana na mzunguko mdogo wa fursa za kibiashara kupelekwa wilaya ya jiran na watumishi wa idara  inayohudumia  wakimbizi katika kambi ya mtendeli kuishi Wilayani Kibondo, hali inayo pelekea shughuli zao zote kufanyika Wilayani humo.

Kufuatia hali hiyo mkuu wa Wilaya Kanali Hosea Ndagala  alitoa  wito kwa watumishi  hao kutoa fursa za kiuchumi kwa wafanya biashara wa Wilaya ya Kakonko wakati wa ujenzi wa nyumba za kudumu za wakimbizi, lengo likiwa ni kuongeza mzunguko  wa kibiashara kwa Wananchi wanao izunguka kambi hiyo na kuacha tabia ya kutoa tenda zote za ujenzi kwa wafanya biashara wa Wilaya ya Kibondo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Wilayani humo, Ndagala alisema watumishi wengi wa Kambi ya mtendeli wamekuwa wakifanya biashara na wafanya biashara wa Kibondo,wakati kambi hiyo inahudumia wakimbizi katika Wilaya ya Kakonko hali inayo pelekea uchumi wa wananchi wa Kakonko waliotegemea kuupata kupitia kambi hiyo kuanzishwa kukosekana na kuhamia wilya nyingine ya Kibondo.

Ndagala alisema halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ni halmashauri ambayo uchumi wake bado upo chini,unahitaji kuinuliwa hivyo akawaomba wafanyakazi wa kambi ya Mtendeli pamoja na shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR kutoa vipaumbele kwa  Wananchi wa Wilaya ya Kakonko ili kuinua uchumi wa Wilaya hiyo kwa kuwapatia ajira za ujenzi na ununuzi wa vifaa vya ujenzi kwa wafanya biashara wa Kakonko.

Hata hivyo Mkuu huyo aliwaomba watumishi wote  wa Kambi hiyo na mashirika yanayo hudumka wakimbizi kurudi kuishi Kakonko kwakuwa sababu iliyo kuwa ikiwapelekea waishi Kibondo ya kukosekana kwa Nyumba  za kupanga Wilayani humo limekwisha Wananchi wamejitahidi kujenga nyumba zenue ubora ambazo wanaweza kupanga na kufanya kazi zao za kuhudumia wakimbizi wakiwa wilayani humo.

"Tenda nyingi za ujenzi wa Nyumba za kudumu za Wakimbizi zimekuwa zikitolewa kwa wafanya biashara wa kibondo jambo ambalo sio zuri ukizingatia Wilaya yetu inakambi yenye wakimbizi wengi shughuli zao za Kijamii zinategemea wilaya yetu ni lazima Wananchi wetu na Wilaya kwa ujumla tunufaike na ujio wa wakimbizi sio wilaya yetu inaadhirikana Wilaya nyingine inanufaika",alisema Ndagala

Aidha mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kakonko ,Juma Maganga  alisema Mpaka sasa Kambi ya Mtendeli ina jumla ya wakimbizi 50,000 ambapo kambi hiyo imejaa na inatarajiwa kuanzishwa kambi nyingine kufuatia hali hiyo Wilaya yetu inawahudumia wote hao na wanategemea huduma nyingine kama vile ukataji wa kuni uchotaji wa maji kutoka kwa Wanakijiji wanao xunguka kambi,endapo fursa za kiuchumi zinapo pelekwa kibondo haileti picha nzuri kwa wanNchi wetu.

alisema kwa sasa ni fursa mojawapo kwa wilaya  ya kakonko kunufaika na ujio wa wakimbizi  kupitia mradi wa uanzishwaji wa majengo ya kudumu kwa wafanya biashara kupata tenda za kuhudumia vifaa vya ujenzi,vyakula kwa Mafundi na wakimbizi mara watakapo kurejea  nchini kwao baada ya kuridhika uwepo wa amani.

Pia tungependa watumishi wote warudi Kakonko kambi haiwezi kuwa katika Wilaya yetu na watumishi wanaishi Wilaya nyingine jambo hilo sio zuri linaweza kupelekea uharibifu Mkubwa ukizingatia wakombizi hao baadhi hutoroka nyakati za usiku  na kufanya vitendo vya kiuhalifu kwa Wananchi wanao izunguka kambi.

Kwa upande wake Mkuu wa kambi ya Mtendeli Inocent Mwaka alisema Suala hilo atalifanyia kazi atazungumza na wahusika iliwaweze kufanya mambo hayo yaliyo pendekezwa na Mkuu wa Wilaya kwa kuwashawishi kuwahamishia watumishi wote wa kambi katika Wilaya ya kakonko na kutoa fursa kwa Wananchi wa Kakonko kunufaika na ujio wa wakimbizi hao.

No comments: