Friday, June 10, 2016

RAIS MAGUFULI AFUTA HATI YA MASHAMBA YA HEKTA 5,000

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa John Pombe Magufuli amefuta hati ya mashamba ya Mkonge, yenye hekta zaidi ya 5,000 yaliyokuwa yametelekezwa na kuwa mapori ambayo hayaendelezwi kufuatia malalamiko ya wakazi zaidi ya 2,000 wa kijiji cha Kibaranga kuhangaikia maeneo ya kilimo na kusababisha migogoro ya mara kwa mara baina yao.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kibaranga katika mkutano wa hadhara, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi amesema hili ni shamba la sita kufutwa na kuwapa wananchi na Mheshimiwa Rais katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga kufuatia wawekezaji waliopewa hati ya kuyaendeleza kushindwa kutekeleza makubalino.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigella amesema Serikali ya mkoa wa Tanga imepewa jukumu la kugawa ardhi hiyo na watahakikisha kuwa wanaweka utaratibu utakaowezesha kila mwananchi apate shamba na hati ili yaweze kuwaendeleza wananchi.

Kufuatia hatua hiyo Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayoshughulikia ulinzi na usalama Mheshimiwa Adadi Rajab amesema watahakikisha wawekezaji matapeli hawaruhusiwi kujimegea ardhi kwa manufaa yao na badala yake mashamba hayo yaendelezwe na wananchi waliokabidhiwa ili yaweze kuwapa manufaa.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akiwatangazia wanakijiji wa Kibaranga kuwaelezea uamuzi wa Rais Dk John Pombe Magufuli wa kufuta hati ya Shamba leyenye hekta zaidi ya 5,000 ambalo lililokuwa limetelekezwa na mwekezaji, kwenye kijiji cha Kibaranga kilichopo wilayani Muheza mkoani Tanga.

Mhe. Lukuvi akiwapa muongozo wanakijiji wa Kibaranga jinsi ya kugawana shamba hilo ambalo limerejeshwa kwao na Mhe. Rais baada ya kufuta hati ya Shamba hilo kwenye kijiji cha Kibaranga kilichopo wilayani Muheza mkoani Tanga.

Wakazi wa kijiji cha Kibaranga wakielezea furaha yao kwa Mhe. Lukuvi kwa uamuzi wa Rais Dk John Pombe Magufuli kufuta hati ya Shamba lililokuwa limetelekezwa na mwekezaji kwa muda mrefu.
Mbunge wa Jimbo la Muheza mkoani Tanga kilipo kijiji cha Kibaranga, Mhe. Adadi Rajabu akizungumza baada ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kuwaelezea wanakijiji hao uamuzi wa Rais Dk John Pombe Magufuli kufuta hati ya Shamba lililokuwa limetelekezwa na mwekezaji, kwenye kijiji cha Kibaranga kilichopo wilayani Muheza mkoani Tanga.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akizungumza na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza muda mfupi baada ya kuwasili wilayani humo akitokea Lushoto, Tanga kabla ya kuelekea Kijiji cha Kibaranga kufuta hati ya Shamba lililokuwa limetelekezwa na mwekezaji.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akizungumza na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza muda mfupi baada ya kuwasili wilayani humo akitokea Lushoto, Tanga kabla ya kuelekea Kijiji cha Kibaranga kufuta hati ya Shamba lililokuwa limetelekezwa na mwekezaji.

No comments: