Friday, May 13, 2016

ETIHAD AIRWAYS YAFUNGUA JUMBA LA KIFAHARI LA MAPUMZIKO KATIKA UWANJA WA NDEGE WA MELBOURNE.

Jumba la kifahari la mapumziko la Shirika la Ndege la Etihad Airways katika uwanja wa ndege wa Melbourne, Australia.

Shirika la ndege la Etihad leo limefungua rasmi jumba jipya la kifahari kwa ajili ya kupumzikia abiria wake katika uwanja wa ndege wa Melbourne, Australia. Jumba hilo ni mahususi kwa kuwapatia abiria mazingira tulivu ambayo wanaweza kupumzika, kuongeza nguvu, kula, kufanya kazi au kuburudishwa kabla ya safari.

Ni eneo ambalo limejawa na nuru ya asili yenye vioo tokea sakafuni hadi katika dari, inatoa mtazamo mpana wa eneo la kurukia ndege. Lina zaidi ya mita za mraba 800 yenye viti vya kukaa hadi kufikia wageni 133, ni nyumba ya kupumzika ya shirika la ndege la Etihad ambayo ni kubwa zaidi iliyoko nje ya Abu Dhabi.

Sehemu ya katikati ya nyumba hii ya kupumzika ni eneo la kulia chakula lenye viti 26 vya ukaribu. Sehemu hii wageni watafurahia alama ya ukarimu ya shirika hili kwa kula katika Mgahawa unaotoa huduma ya chakula cha pekee na buffet la kimataifa.

 Wapishi wenye ujuzi wa hali ya juu huwepo pale muda wote wakipika kila chakula kwa kutumia bidhaa za msimu zilizokusanywa kwa njia ya kawaida. Hii inajumuisha mikate freshi ambayo inaokwa kila siku mara mbili, Grissini bradstick; ya kuchovya kama vile humus, Baba ghanoush na muhammara; piko; labneh; biskuti; na hata ice cream, Jibini, matunda na mboga za majani zinachukuliwa kutoka Victoria suppliers na kahawa inatoka kwa wakaangaji wa kahawa wa Melbourne.

Sifa nyingine ya kipekee ni bar yenye picha za vinyago, iliyojaa mvinyo kutoka kwa watengenezaji wa Victoria na zaidi ya aina 70 ya vinywaji bora vikali, shamapeni na viamsha hamu. Muongozo wa kuagiza Cocktail pia unapatikana. Uchaguzi wa kibunifu, umetengenezwa kwa ushirikiano na washauri wa mambo ya vinywaji wanaoongoza kutoka London Fluid Movement, inajumuisha aina ya kipekee ya Cocktail yenye majina ya vituo mbalimbali kama Melbourne, Sydney, Paris na New York na Mock tail inayoitwa Abu Dhabi, Controlled Airspace na Winglet. Cocktail na Mock tails ya Controlled Airspace na Winglet. Kama ilivyo kwa vyakula vilivyoko katika orodha ya mwongozo iliyoko katika sehemu ya chakula, zote zimetengenezwa kwa mkono kwa kutumia wachanganyaji waliopitia mafunzo, wakitumia syrup na garnishes kama vile Candy floss na rhubarb zilizokaushwa ambazo zimetengenezwa ndani ya jumba hili na wataalamu wa jadi, bar inatoa uchaguzi wa kisasa, kama vile Mach 10 Majito, ambayo imegunduliwa na kutengenezwa na Fluid Movement. Wapenzi wa Negroni watafurahia kufahamu kuwa kiamsha hamu kimechanganywa, kikavundikwa na kuhifadhiwa nyuma ya bar.

Ubunifu wa ndani, kanuni ya mtindo, nafasi na utulivu vimekamilishwa na shirika la ndege la Etihad kutoka kwenye bidhaa zake za kipekee za ‘Facets of Abu Dhabi’ ikiwa na mtindo wake wa kijiometri na rangi ambayo inapewa motisha na mandhari ya UAE, ni mwonekano wa kipekee wa karne ya 21 ya ubunifu wa Abu Dhabi.

Fanicha za kitamaduni – zilizoandaliwa na Boss – zinawapatia wageni wa nyumba hii ya kupumzika uchaguzi wa mtindo wa kukaa, kila mmoja imebuniwa kwaajili ya kuongeza kiwango cha starehe na utulivu wakati wa kula, kufanya kazi na kupumzika.

Pamoja na kuanza kwa huduma za A380 tokea tarehe 01 Juni, wageni katika daraja la makazi watafurahia upekee wa nyumba ya kupumzikia ya binafsi – ambayo imejengwa kwa makini kabisa kando ya lango kuu la kuingilia katika jumba la mapumziko. Ikiwa na viti vyenye mikono iliyofunikwa kwa ngozi ya Kiitalia ya Poltrona Frau, vilivyokamilishwa kwa vitambaa safi laini vya mahameli, chumba cha peke yake cha kupumzika na mlango wa kujitegemea, Nyumba ya kupumzika ya Daraja la Makazi ina huduma za kuagiza za kitajiri na huduma binafsi ambazo zinalingana na ukarimu wa kiwango cha juu wa shirika hili la ndege.

Huduma nyingine katika Nyumba kuu ya kupumzikia inajumuisha vyumba tofauti vya kupumzika kwa ajili ya wanawake na wanaume vyenye mabafu pamoja na bidhaa za Scaramouche + Fandago, vyumba maalumu vilivyotengwa kwaajili ya wanawake na wanaume kuchukulia udhu na vyumba tofauti vya kuswalia na chumba cha watoto kucheza na chumba cha mizigo.

Huduma ya Wi-Fi yenye kasi inakamilishwa na soketi za umeme ambazo zimewekwa kila mahali katika Nyumba ya kupumzikia.
Makamu wa Rais katika Idara ya Masoko wa Shirika la ndege la Etihad bwana Shane O’Hare, aliyekata utepe wa sherehe akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la ndege la Melbourne bwana Lyell Strambi katika ufunguzi rasmi leo alisema:

“Nyumba mpya ya kupumzika ya kifahari iliyoko Uwanja wa ndege wa Melbourne ni daraja la peke yake – ni nyumba ya kupumzikia ya uwanja wa ndege kama ambavyo inajulikana, ambayo imeboreshwa kabisa.

“Ikiunganisha Mgahawa bora wa chakula na Bar ya Cocktail, Nyumba hii ni maonesho ya ubunifu wa kiwango cha juu na umakini ambao wageni watafurahia kiwango cha juu cha utulivu na starehe, inayokamilishwa na ukarimu wetu wa kiwango cha kimataifa, ubunifu katika mapishi na teknolojia ya kiwango cha juu ya vinywaji.

“Wakati huo huo, inakuletea hisia kali ya kitamaduni kwa jibini freshi na mvinyo – unaochukuliwa kutoka kwa wakulima, watengenezaji na wasambazaji katika jimbo lote la Victoria – ambayo inawapatia wageni wetu ladha ya kusisimua ya utamaduni na umaarufu wa upishi.

“Ufunguzi wa huduma hii ya kustaajabisha na uzinduzi wa huduma yetu kuu ya A380 hapo tarehe 1 Juni, unawapa wageni wetu katika ruti ya Melbourne na Abu Dhabi uzoefu wa ushawishi wa huduma ya hali ya juu kuliko zote.”

Wageni katika Makazi, Apartments za kwanza na Business Studios watakaribishwa kutembelea Nyumba ya kupumzikia kabla ya kusafiri. Wanachama wa Platinum, Dhahabu na Fedha  wa wageni wa Etihad na wanachama wenye sifa wa mashirika ya ndege washirika wa shirika la ndege la Etihad na mpango wa Uaminifu (loyalty) wa mashirika ya ndege washirika wataweza kutumia nyumba hii ya kupumzika wanapokuwa wanasafiri katika Daraja la Economy. Wageni lazima wawe ameorodheshwa katika ndege ya shirika la ndege la Etihad inayofanya kazi siku hiyo.

Iko katika kituo cha 2 karibu na lango la 10, nyumba ya mapumziko itakuwa wazi takribani masaa matatu kabla ya kuondoka kwa ndege za Etihad mara mbili kila siku katika ruti ya Melbourne kwenda Abu Dhabi.

Jumba hili linaongeza orodha inayokuwa ya nyumba za kiwango cha juu za kupumzikia zilizoko Sydney, Abu Dhabi, Dublin, Frankfurt, London Heathrow, Manchester, Paris, Washington DC na New York. Njumba ya kupumzikia ya daraja la kwanza iliyoko katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abu Dhabi na Jumba jipya la kupumzikia la daraja la Kwanza na business huko Los Angeles yatafuata miezi ijayo.

Shirika la ndege la Etihad lilianza safari za ndege za kila siku kwenda Melbourne mwezi Machi mwaka 2009. Leo, inafanya safari zake mara mbili kila siku, safari zisizo na ukomo kwenda Abu Dhabi na nje ya GCC, Afrika na Ulaya. Ni shirika pekee la ndege linalotoa safari zisizo na ukomo za kila siku kutoka Melbourne kwenda katika Umoja wa mataifa ya Kiarabu. Wabebaji wa bendera ya UAE watatambulisha ndege yao kuu ya A380 hapa Melbourne kuanzia tarehe 1 June 2016, jambo ambalo litaleta daraja la Makazi katika ruti hii, vyumba vitatu vya peke yake katika ndege ya kibiashara duniani.

Zaidi ya kufanya safari zake mara mbili kila siku kwenda Melbourne, Shirika la ndege la Etihad inafanya safari zake za kila siku kwenda Brisbane na kwenda Perth na huduma 11 kwa wiki kwenda Sydney. Mashirika ya ndege washirika ya usawa, Virgin Australia, inafanya safari zake tatu nyingeza za kila wiki kati ya Sydney na Abu Dhabi.

No comments: