Monday, April 25, 2016

BONANZA LA USALAMA WA AFYA MAHALI PA KAZI.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Bw. Anthony Mavunde, akimkabidhi, Nahodha wa NSSF, Pili Mogola, kombe la mshindi wa kwanza wa Netiboli, wakati wa Bonanza la Usalama na Afya mahali pa kazi, lililofanyika Dar es Salaam juzi na kudhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dar es Salaam juzi.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Bw. Anthony Mavunde (kulia) na Mtendaji Mkuu Mamlaka ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Dk. Akwilina Kayumba, wakishiriki kufanya mazoezi na wakati wa maadhimisho ya Bonzanza la usalama na Afya mahali pa kazi lililodhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),Dar es Salaam juzi. 
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Bw. Anthony Mavunde (aliyesimama katikati), akizungumza na wachezaji wa timu za Netiboli za Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) na Mamlaka ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), wakati wa Bonanza la usalama na Afya hahali pa kazi lililofanyika Dar es Salaam juzi kwa udhamini wa NSSF.
 Wachezaji wa timu ya Netiboli ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), wakishangilia baada ya kutwaa kombe wakati wa bonanza la Usalama na Afya mahali pa kazi, lililofanyika Dar es Salaam juzi na kudhaminiwa na NSSF.
Mshambuliaji wa timu ya soka ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Ali Chuo (kushoto), akimiliki mpira mbele ya mlinzi wa timu ya Wizara ya Kazi, Abdallah Sanga, wakati wa Bonaza la Usalama na Afya mahali pa kazi lililofanyika Dar es Salaam juzi kwa udhamini na NSSF.

No comments: