Wednesday, January 20, 2016

MULTCHOICE TANZANIA YAPATA CHAI YA PAMOJA NA WANAHABARI KATIKA HALFA YA KUKARIBISHA MWAKA MPYA

Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu akiwaongoza wanahabari kupata chai maalum iliyoandaliwa na kampuni hiyo kwa ajili ya kuukaribisha mwaka mpya pamoja na kufahamiana zaidi ikiwemo huduma na utendaji kazi kwa hapa nchini. 

(Picha zote na Andrew Chale, modewjiblog).

Baadhi ya wanahabari wakiwa katika shughuli hiyo maalum iliyoandaliwa kwa ajili yao na MultChoice Tanzania ambao ni wasambazaji wa ving'amuzi vya DSTV kwa Tanzania.
Baadhi ya wanahabari wakipata Chai katika shughuli hiyo maalum iliyoandaliwa kwa ajili yao na MultChoice Tanzania ambao ni wasambazaji wa ving'amuzi vya DSTV kwa Tanzania.

Watendaji wa Multchoice Tanzania wakitoa shukrani zao kwa wanahabari waliofika katika mwaliko maalum wa kuukaribisha mwaka pamoja na kufahamiana zaidi halfa iliyofanyika mapema asubuhi ya leo katika makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam. 
Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu (kulia) akiwa na Shumbana Walwa wa kampuni hiyo akipata picha ya kumbukumbu.


Washindi watatu ambao ni wanahabari wakipata picha ya pamoja na zawaidi zao ambao wamejishindia ving'amuzi vya DStv na hofa za kifurushi cha mwezi mmoja pamoja na kufungiwa bure majumbani kwao.
Wanahabari walioshinda vifurushi vya mwezi vya "Premium" wakipata picha ya pamoja na maafisa wa Multchoice Tanzania 
Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu (kulia) akizungumza na wanahabari kuhusiana na siku hiyo maalum ya kukaribisha mwaka mpya pamoja na kuandaa chai maalum kwa wanahabari.
Wanahabari wakibadilishana mawazo na Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo katika halfa hiyo makao ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.

No comments: