Monday, December 21, 2015

SHIRIKA LA NDEGE LA ETIHAD LATANGAZA KUSAMBAZWA KWA BOEING 787S KWA SAFARI ZAKE MWAKA 2016

SHIRIKA la ndege la Etihad, ndege rasmi ya taifa kwa Falme za kiarabu limetangza kuanzisha mipango ya kurusha ndege aina ya boeing 787s kwa safari za kwenda Dusseldorf, Perth, Shanghai, Istanbul na Johannesburg kwa mwa mwaka 2016.

Matarajio ya kuwasili kwa ndege hizo mpya aina ya Boeing 787s ni ndani ya miezi saba ijayo, kuanzia Mei 2016, ndege hizo “Dreamliners” zenye uwezo wa kubeba abiria 299 zitaanza kutoa huduma kwenda Dusseldorf, Perth, Shanghai, Istanbul na Johannesburg kutoka Abu Dhabi zikichukua nafasi ya ndege zinazotumika sasa.

Kwa sasa Shirika la ndege la Etihad lina ndege tano tu aina ya 787s ambazo zinafanya safari zake kati ya Brisbane, Washington, Singapore na Zurich moja kwa moja kutoka Abu Dhabi. 

Matarajio ya Shirika hilo ni kuongeza zaidi ya Boeing 66 ndani ya miaka kadhaa ijayo ambapo ndege hizo aina ya “Dreamliners”zitakuwa ndege rasmi za shirika hilo kwa masafa marefu.

James Hogan, ambaye ni Rais na afisa mkuu wa shirika la ndege la Etihad alisema: “Tangu kuanzishwa kwa ndege aina ya 787 ya kwanza katika huduma za kibishara mnamo februari mwaka huu, tumekuwa tukipata maoni mazuri kutoka kwa abiria wetu  ambayo yamekuwa kama alama ya ubora wa hali ya juu katika kanda na dunia nzima.

“Kuanzia mwezi Mei mwakani, shirika la ndege la Etihad litazindua ndege mpya Boeing 787 aina ya dreamliners zitakazotumika rasmi badala ya hizi zilizopo kwa safari za masafa marefu ambapo zitatoa fursa kwa abiria wetu kupanda ndege za teknolojia mpya.

“Abiria na wateja wetu wa siku hizi wanapenda kusafiri bila kero wala pirika pirika kwenye usafiri wa viwango vya juu, wanataka chaguo zuri zaidi na bei nafuu. Hivi ndivyo vigezo vyao vikuu katika kuchagua na sisi hapa Etihad tunajitahidi kufikia matarajio hayo kwa tafiti na uvumbuzi wa aina mbalimbali kama vile kuleta ndege mpya na kuendelea kuboresha njia zetu za usafiri.

Ndege hizi mpya aina ya 787-S zitajumuisha ubunifu wa ndani ya kabini 28 za “business studios” na siti 271 za “economy smart” zikiwa na utulivu, burudani na uwezo wa kuunganishwa kwa mawasiliano zikiwa angani. 

Upambaji wa ndani na mwanga vimesukwa zaidi kwa ubunifu wa kiarabu zikiendana na ubunifu mpya wa kutoka “Abu dhabi” ulioletwa na shirika la ndege hili katika uzinduzi mpya mwaka jana.
Ratiba ya Boeing 787 kwenda DUSSELDORF, kuanzia Mei mosi 2016 (muda wa Abu Dhabi):
Ndege Na.
Inaanzia
Inaondoka
Itawasili
Muda wa kufika
Mizunguko
EY0023
Abu Dhabi (AUH)
02:15
Dusseldorf (DUS)
07:20
Kila siku
EY0024
Dusseldorf (DUS)
11:50
Abu Dhabi (AUH)
20:25
Kila siku

Ratiba ya Boeing 787 kwenda PERTH, kuanzia Juni Mosi 2016 (muda wa Abu Dhabi):
Ndege Na.
Inaanzia
Inaondoka
Itawasili
Muda wa kufika
Mizunguko
EY0486
Abu Dhabi (AUH)
22:25
Perth (PER)
13:50 siku inayofata
Kila siku
EY0487
Perth (PER)
15:40
Abu Dhabi (AUH)
23:10
Kila siku

Ratiba ya Boeing 787 kwenda SHANGHAI, kuanzia Agosti Mosi 2016 (muda wa Abu Dhabi):
Ndege Na.
Inaanzia
Inaondoka
Itawasili
Muda wa kufika
Mizunguko
EY0862
Abu Dhabi (AUH)
21:55
Shanghai (PVG)
11:10 siku inayofata
Kila siku
EY0867
Shanghai (PVG)
00:30
Abu Dhabi (AUH)
06:25
Kila siku
  
Ratiba ya Boeing 787 kwenda ISTANBUL, kuanzia Agosti 1 2016 (muda wa Abu dhabi): 
Ndege Na.
Inaanzia
Inaondoka
Itawasili
Muda wa kufika
Mizunguko
EY0097
Abu Dhabi (AUH)
09:05
Istanbul (IST)
13:10
Kila siku
EY0096
Istanbul (IST)
14:25
Abu Dhabi (AUH)
20:00
Kila siku
  
Ratiba ya Boeing 787 kwenda JOHANNESBURG, kuanzia Novemba Mosi 2016 (muda wa Abu Dhabi):
Ndege Na.
Inaanzia
Inaondoka
Itawasili
Muda wa kufika
Mizunguko
EY0604
Abu Dhabi (AUH)
10:00
Johannesburg (JNB)
16:40
Kila siku
EY0603
Johannesburg (JNB)
19:40
Abu Dhabi (AUH)
06:00 next day
Kila siku

No comments: