Friday, October 16, 2015

TAWLA YAENDELEZA MIDAHALO YA AMANI KWA WADAU WA UCHAGUZI

 Mwanasheria wa Manispaa ya Ilala, Elizabeth Buwimba, akichangia mada ya wajibu wa mwanamke kushiriki kwenye uchaguzi na umuhimu wakufanya hivyo wakati wa mdahalo wa kujadili amani wakati na baada ya uchaguzi, uliofanyika eneo la Pugu jijini Dar es Salaam.


 Mwanasheria kutoka Chama Cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) Edna Kamaleki, akiwasilisha mada mbalimbali wakati wa mdahalo wa kujadili amani wakati wa uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu, kwa watendaji wa serikali za mitaa jimbo la Ukonga na watendaji wa Halmashauri ya wilaya na Jeshi la Polisi. 
 Baadhi ya Watendaji wa Tawla wakiandika baadhi ya maoni ya washiriki wa mdahalo huo.
 Mjumbe wa Serikali ya Mtaa Pugu jijini Dar es Salaam Jamila Jackson, akichangia hoja ya mjadala huo
 Ofisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Ilala, Victor Mukiza, akichangia mada ya amani wakati wa mdahalo ulioandaliwa na chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) kwa watendaji wa Serikali za Mitaa,Polisi na watumishi wa Halmashauri hiyo jana.



.picha na Emmanuel Massaka

No comments: